Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/93 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Mei 3
  • Juma Linaloanza Mei 10
  • Juma Linaloanza Mei 17
  • Juma Linaloanza Mei 24
  • Juma Linaloanza Mei 31
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 5/93 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei

Juma Linaloanza Mei 3

Wimbo 209

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.

Dak. 20: “Kushiriki kwa Mafanikio Katika Huduma Yetu ya Kuokoa Uhai.” Hotuba na maonyesho. Baada ya utangulizi mfupi, fanya maonyesho mawili yakitegemea mafungu 2, 3 na 5. Baada ya kila wonyesho, waulize wasikilizaji jinsi mfikio ungeweza kubadilishwa kulingana na hali mbalimbali katika eneo la kwenu. Malizia kwa kutia moyo kushiriki kikamili katika huduma mwisho juma huu.

Dak. 15: Umaana wa Hali ya Kiroho ya Familia. Hotuba ikitolewa na mzee. Zungumzia uhitaji wa familia kuchunguza andiko la siku, ukionyesha jinsi hili laweza kufanywa chini ya hali tofauti-tofauti na ratiba za familia. Pia kazia uhitaji wa sala ya familia angalau mara moja kwa siku. Hili laweza kufanywa wakati wa kwenda kulala. Kanuni hizohizo zinazotumika katika nyuma zenye kugawanyika, familia za mzazi mmoja, na familia zisizo na watoto. Kutayarisha mkiwa familia kwafaa pia ili kunufaika na mikutano ya kundi kila juma na kuweza kutia nguvu imani ya wengine pia.—Ebr. 10:23-25.

Wimbo 104 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 10

Wimbo 27

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Mambo yaliyoonwa karibuni ya kufurahisha kufanyia kazi maandikisho, magazeti na broshua.

Dak. 18: “Kukabiliana na Ugumu wa Huduma ya Nyumba kwa Nyumba.” Maswali na majibu. Soma maandiko yaliyowekwa kando na uonyeshe yanavyohusu.

Dak. 15: Kutoa Ushahidi kwa Watoto. Mwangalizi msimamizi apitia kanuni zilizoonyeshwa kwenye Huduma ya Ufalme Yetu, ya Novemba 1988, ukurasa 8 chini ya “Kutangaza Habari Njema.”

Wimbo 134 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 17

Wimbo 16

Dak. 10: Matangazo ya kwenu, kutia ndani ripoti ya hesabu na shukrani za upaji wa hiari. Pongeza kundi kwa utegemezo wa kifedha wa kundi la kwenu na wa kazi ya Sosaiti ya ulimwenguni pote.

Dak. 20: “Rudi kwa Shangwe ili Kusaidia Wenye Kupendezwa.” Mazungumzo na wasikilizaji na maonyesho. Kazia uhitaji wa kuweka rekodi nzuri za kupendezwa kunakopatikana. Panga maonyesho mawili, kutokana na habari iliyo kwenye mafungu 3-6. Yanapaswa kuonyesha hali za kwenu na zibadilishwe kulingana na uhitaji.

Dak. 15: Eneo Lisilohubiriwa kwa Ukawaida. Mwangalizi wa utumishi azungumzia umaana wa kutoa ushahidi kamili katika sehemu zote za eneo la kundi. (Mdo. 20:24, 26) Omba ushirikiano wa mapainia wa kawaida na wasaidizi na vikundi vya katikati ya juma wajaribu kwa miezi inayokuja kufikia maeneo yasiyohubiriwa kwa ukawaida. Onyesha mipango hususa ya kuhubiri maeneo hayo.

Wimbo 54 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 24

Wimbo 141

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 20: “Vijana—Elekezeni Hatua Zenu kwa Ustadi.” Habari hiyo ipitiwe kwa maswali na majibu. Baada ya fungu la 3, kuwe na wonyesho mfupi ambapo mhubiri kijana anauliza mhubiri mwenye umri mkubwa kufanya kazi naye kwenye utumishi wa shambani. Mhubiri mwenye umri mkubwa akubali kwa furaha na adokeza wapitie utoaji wao mbalimbali kabla ya kufanya kazi pamoja.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Au mzee atoe hotuba juu ya “Kwa Nini Ni Rahisi Sana Kusema Uongo?” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Desemba 15, 1992, kurasa 21-3.

Wimbo 223 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 31

Wimbo 207

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Dokeza mambo ya kuzungumziwa kwenye kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi ambayo yanaweza kutumiwa katika Juni. Watie moyo wahubiri wapitie madokezo ya utumishi wa shambani yaliyo nyuma ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1993.

Dak. 15: Je! Utafanya Upainia Msaidizi Miezi Inayokuja? Hoji baadhi ya wale ambao wamefanya upainia msaidizi kipindi hiki katika miaka iliyopita. Tia moyo vijana na wengine ambao hali inaruhusu wafikirie kutumia vipindi vya likizo kwa manufaa. Wengine huenda wakaweza kusaidia kuhubiri maeneo yasiyohubiriwa kwa ukawaida au maeneo ya mbali. Tia moyo wale watakaoacha shule wafanye upainia wa kawaida au waweke mradi huo.—2 Kor. 9:6b.

Dak. 15: Je! Mungu Husamehe Makosa Yetu? Wazee wawili wajitayarisha kwa ziara ya uchungaji. Wanazungumza jinsi ya kusaidia ndugu ambaye bado anasumbuliwa na dhambi za wakati uliopita na anajiuliza kama Mungu amemsamehe. Wazee wapitia habari iliyo kwenye kitabu Kutoa Sababu, kurasa 365-9, na pia kitabu Insight, Buku 1, kurasa 861-2. Wanafikiria uhitaji wao wa kushughulikia kwa fadhili ndugu huyo na kuonyesha huruma ya Yehova na utayari wa kusamehe. Pia wanapanga kukazia uhitaji wa jitihada ya binafsi kwa upande wa ndugu; kuungama peke yake hakutoshi. Wazee watajitoa kumtembelea ndugu mara kwa mara, wakiwa na msaada wa kiroho.

Wimbo 214 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki