Kushiriki kwa Mafanikio Katika Huduma Yetu ya Kuokoa Uhai
1 Mtume Paulo alibadilisha utoaji wake wa habari njema ili ‘apate kuwaokoa watu.’ (1 Kor. 9:19-23) Vivyo hivyo, tutakuwa wenye mafanikio sana katika huduma yetu ikiwa tunakuwa chonjo kutambua kupendezwa kwa mwenye nyumba na tunakuwa tayari kubadilisha mazungumzo yetu kulingana na mahitaji yake. Hilo halipasi kuwa jambo gumu tunapotoa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! au mojawapo broshua zetu.
2 Baada ya kujijulisha, unaweza kuanza kwa kusema hivi kwa maneno yako mwenyewe kwa mtu anayesema yeye ni Mkristo:
◼ “Tunawauliza jirani zetu swali fulani na tungethamini maelezo yako juu ya hilo. Kwa kuwa Yesu alitufundisha kusali kwa ajili ya Ufalme wa Mungu uje na mapenzi Yake yafanywe duniani kama mbinguni, je! wewe unafikiri kwamba mapenzi ya Mungu yatafanywa kwelikweli hapa duniani?” Ruhusu jibu, halafu ufungue Isaya 55:10, 11 na umwambie mwenye nyumba aone jinsi ahadi zote za Mungu zitakavyotimizwa.—rs-SW, uku. 12-13 utangulizi wa pili chini ya “Ufalme.”
3 Mwenye nyumba akionyesha kupendezwa, unaweza kuendelea kwa kusema:
◼ “Mojapo makusudi ya gazeti Mnara wa Mlinzi ni kuvuta uangalifu kwenye utimizo wa unabii wa Biblia. Ona makala hii.” Halafu elekeza fikira kwenye makala “Je! Wewe Utatii Onyo la Mungu?” katika toleo la Machi 1 la Mnara wa Mlinzi. Rejezea jambo moja au mawili kwenye sanduku ukurasa wa 5 halafu utoe uangalifu kwenye mafungu ya mwisho chini ya kichwa kidogo “Wakati Mtukufu Baada ya Uharibifu.” Halafu toa uandikisho. Ikiwa toleo la kawaida halichukuliwi unaweza kutoa magazeti hayo mawili na broshua kwa mchango wa kawaida.
4 Ikiwa mwenye nyumba haonyeshi imani katika Mungu, unaweza kurejezea Waebrania 3:4 halafu ufungue ukurasa wa 4 wa broshua Je! Kweli Mungu Anatujali? Soma mafungu 1 na 2 na uulize swali lililo chini ya ukurasa huo. Au unaweza kuunganisha habari inayofaa kutoka gazeti la karibuni.
5 Ikiwa mwenye nyumba ni kijana, unaweza kusema kama ifuatavyo baada ya kujijulisha:
◼ “Nawatia moyo vijana kama wewe wafikirie wakati ujao mtukufu ambao Biblia inatuahidi. (Soma andiko, kama vile Ufunuo 21:3, 4.) Je! hilo lakupendeza?” Halafu tunaweza kutumia habari inayopatikana katika toleo la Aprili 15 la Mnara wa Mlinzi kuonyesha jinsi magazeti yetu yanavyotoa mwongozo madhubuti kwa vijana. Vijana wengi huandikisha magazeti yetu.
6 Pia unaweza kutumia mfikio wa juu kwa vijana pamoja na fungu la mwisho la ukurasa wa 5 na 6 wa trakti Je! Ulimwengu Huu Utaokoka?
7 Kwenda kwako kwa mara ya kwanza hakutafanikiwa kabisa ikiwa hautaamsha hamu ya mwenye nyumba kwa ajili ya ziara nyingine. Kwa hiyo, hakikisha umeuliza swali lenye kupendeza na uahidi kulijibu ukirudi.
8 Chagua unalohisi huru kusema, kutokana na habari iliyo juu. Badilisha madokezo hayo kulingana na eneo lenu. Zizoelee broshua, trakti, na makala za magazeti ambazo utatumia ili uweze kubadilisha mara moja mazungumzo yako kulingana na mahitaji ya mwenye nyumba. Kwa bidii nyendelevu sisi sote na tutayarishe utoaji wetu “kwa ajili ya Injili” na hivyo tushiriki kwa mafanikio katika huduma hii ya kuokoa uhai.—1 Kor. 9:23.