Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/99 uku. 4
  • Acheni ‘Tuseme Waziwazi!’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Acheni ‘Tuseme Waziwazi!’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Kushiriki kwa Mafanikio Katika Huduma Yetu ya Kuokoa Uhai
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Wasaidie Wengine Wajifunze Juu ya Mwana wa Mungu, Yesu Kristo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Jinsi ya Kutayarisha Utoaji wa Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Tumia Ile Kanuni Bora Katika Huduma Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 7/99 uku. 4

Acheni ‘Tuseme Waziwazi!’

1 Je, mwenye nyumba amewahi kukatiza utoaji wako uliotayarishwa vizuri kwa maneno haya: “Unataka nini? Sema waziwazi!” Twaweza kujifunza nini na jambo hilo?

2 Watu wengi leo hawana subira. Wanataka kujua sisi ni nani na kwa nini tupo hapo. Wanapotambua kwamba kusudi la ziara yetu ni kuzungumzia Biblia, huenda wakakataa kusikiliza. Usomaji wa Biblia na mazungumzo juu ya mambo ya kiroho si ya maana katika maisha za watu wengi. Twaweza kuwasadikishaje wenye nyumba hao kwamba wanapaswa kuchukua dakika chache kuzungumza habari ya Biblia nasi?

3 Mfikio Wenye Matokeo Zaidi: Jambo la msingi ni kumwonyesha mwenye nyumba kwamba Biblia hutoa utatuzi wenye kutumika kwa matatizo yanayomhangaisha na ufanye hivyo kwa maneno machache iwezekanavyo. Utoaji mbalimbali wenye matokeo zaidi wakazia swali hususa lililokusudiwa kumfanya mwenye nyumba afikiri, na kufuatiwa na andiko ambalo lajibu swali hilo. Huenda ukafurahia kujaribu baadhi ya madokezo yafuatayo. Yamekusudiwa kutusaidia ‘kusema waziwazi’ haraka huku tukiamsha kupendezwa kwa mwenye nyumba.

4 Katika eneo ambapo mara nyingi watu husema kwamba hawapendezwi, tokeza swali linalowahusu binafsi:

◼ “Tunapokaribia milenia ijayo, je, wahisi una tumaini au shaka? [Ruhusu jibu.] Biblia ilitabiri matukio yenye kubabaisha tunayoona leo na pia matokeo yake.” Soma 2 Timotheo 3:1, 2, 5 na Mithali 2:21, 22.

◼ “Hapa nchini watu wanahangaishwa sana na afya. Je, ulijua kwamba Mungu huahidi kuwa atatatua kabisa matatizo yote ya afya?” Soma Ufunuo 21:3, 4.

◼ “Je, wafikiri jamii yetu ingenufaikaje kama kila mtu anayeishi hapa angetumia kanuni za Biblia?” Soma Mathayo 22:37-39.

5 Kwa kuwa utume wetu ni kuhubiri habari njema ya Ufalme, inapowezekana twapaswa kukazia fikira yale ambayo Ufalme utatimiza. Waweza kusema:

◼ “Je, ulipata kujua kwamba kitabu cha kale ulimwenguni, Biblia, kilitabiri kwamba kutakuwa na serikali moja ulimwenguni pote?” Soma Danieli 2:44.

◼ “Unafikiri hali zingekuwaje kama Yesu Kristo angetawala dunia?” Soma Zaburi 72:7, 8.

6 Katika eneo ambapo watu ni wa kidini, waweza kujaribu mojawapo ya utangulizi huu mbalimbali:

◼ “Watu wengi hubaguliwa kwa sababu ya jinsia yao, dini, na rangi ya ngozi yao. Je, wafikiri Mungu huhisije kuhusu ubaguzi huo?” Soma Matendo 10:34, 35.

◼ “Twajua kwamba Yesu Kristo alifanya miujiza mingi katika siku yake. Ikiwa ungemwomba afanye mwujiza mwingine mmoja, ungekuwa upi?” Soma Zaburi 72:12-14, 16.

7 Mwenye nyumba akisitasita kufungua mlango, unaweza kuanzisha mazungumzo kwa kusema:

◼ “Watu wengi leo wamechoka kusikia juu ya matatizo. Wanataka kusikia juu ya utatuzi. Labda ndivyo ilivyo nawe pia. Lakini twaweza kupata utatuzi wa kweli kwa matatizo yetu kutoka wapi?” Ruhusu Jibu. Soma 2 Timotheo 3:16, 17.

8 Kwa Nini Usiujaribu? Mara nyingi swali sahili, lenye kulenga, laweza kuwa tu ndilo linalohitajiwa kuanzisha upendezi wa mwenye nyumba. Mwanamke mmoja ambaye hapo awali alikuwa mpinzani aliwaalika dada wawili nyumbani kwake baada ya wao kumwuliza swali hili: “Waweza kufafanua Ufalme ambao wewe huomba uje katika ile Sala ya Bwana?” Mwanamke huyo alivutiwa sana na swali hilo, naye akakubali funzo la Biblia. Sasa yeye ni mtumishi wa Yehova aliyejiweka wakfu!

9 Unaposema na mwenye nyumba, uwe mwenye ukweli katika maelezo yako. Sema kutoka moyoni. Watu huelekea kuitikia kwa njia nzuri wanaposadikishwa kwamba twapendezwa nao kikweli.—Matendo 2:46, 47.

10 Kazi ya kuhubiri habari njema ni ngumu leo. Wenye nyumba wengine hushuku wageni. Wengine wana maisha yenye shughuli nyingi na wana wakati mchache tu. Hata hivyo, twaweza kuwa na uhakika kwamba bado kuna wengi wanaostahili wanaoweza kupatikana. (Mt. 10:11) Jitihada zetu za kuwatafuta yamkini zitafanikiwa zaidi tukifupisha utoaji wetu mbalimbali na ‘kusema waziwazi!’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki