Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Katika Kitabu Mtu Mkuu Zaidi
1 Kuwa na funzo la Biblia nyumbani kungekuwa kwenye kufurahisha zaidi na kuthawabisha kwenu nyote, wewe na mwenye nyumba. Hakuna jambo lolote la kulinganishwa na shangwe ya kushiriki pamoja na wengine ujuzi wa Biblia.—Mit. 11:25.
2 Ishara ya Siku za Mwisho: Ikiwa ulitumia dokezo la makala iliyo juu na kuanzisha mazungumzo na ile trakti Je! Ulimwengu Huu Utaokoka?, sasa unaweza kuanzishaje funzo ukitumia sura ya 111, ya kitabu Mtu Mkuu Zaidi? Fungua kitabu hicho sura ya 111, na usome mafungu matatu ya kwanza. Kisha unaweza kuuliza swali la kwanza la mwisho wa sura hiyo: “Ni kitu gani kinachowasukuma mitume waulize swali lao, lakini kwa wazi ni kitu gani kingine walicho nacho katika akili zao?” Saidia mwenye nyumba atoe sababu ya hilo jibu, na utumie kielelezo kufundisha. Baada ya kusoma fungu la nne hadi sita, uliza swali la pili: “Ni sehemu gani ya unabii wa Yesu inatimizwa katika 70 W.K., lakini ni nini hakitukii wakati huo?” Mwenye nyumba akionekana anapendezwa na ana wakati, endeleza mazungumzo yako.
3 Mwenye nyumba akiona ingefaa wakati mwingine, unaweza kusema: “Je! ungependa kujua zaidi kuhusu ni lini kutakuwa na mwisho wa mfumo huu wa mambo?” Basi unaweza kupanga kurudi ili kujibu hilo swali.
4 Je! Dunia Yenye Amani Yaweza Kuwapo? Ikiwa ulitumia trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani ili kuelekeza kwenye kitabu Mtu Mkuu Zaidi, sura ya 133 yaweza kuwaje msaada katika kuanzisha funzo la Biblia?
Baada ya kusoma 2 Petro 3:13, unaweza kutoa muhtasari wa fungu la pili kwenye ukurasa wa 3 wa trakti kisha useme:
◼ “Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, atakuwa Mfalme wa Ufalme wa Yehova. Angalia jinsi kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi kinavyoeleza juu ya Yesu na kutujulisha juu ya atakalotimiza wakati ujao.” Kisha usome sura yote. Mwuulize mwenye nyumba swali la kwanza kwenye mwisho wa sura hiyo: “‘Ni nini litakalokuwa pendeleo lenye furaha la waokokaji wa Har–Magedoni na watoto wao?’ [Ruhusu itikio. Maswali mengine yanaweza kuzungumziwa kwa njia iyo hiyo.] Je! ungependa kuwa sehemu ya dunia mpya ambayo Yesu atatawala akiwa Mfalme? Ningependa kuwa na fursa kila juma ya kukusaidia uone kwenye Biblia jinsi unavyoweza kuona jambo hilo.”
5 Watu wengine pia huenda wakapendezwa na mazungumzo zaidi juu ya Yesu Kristo katika ziara hii ya kurudia.
Unaweza kusema:
◼ “Jitihada imefanywa katika kitabu hiki kusimulia maisha ya Yesu ya kidunia kama ilivyoandikwa katika gospeli nne. Ungependa kujifunza mengi juu ya maisha ya Yesu akiwa duniani?” Mwenye nyumba akikubali, unaweza kuzungumza juu ya mojapo miujiza ya Yesu, katika sura ya 15.
6 Bado kuna watu wengi wenye mioyo minyoofu ambao wanapenda uadilifu na wanaotafuta utatuzi wa matatizo wanayokabili. Kwa kweli, kujitolea kushiriki mafundisho ya Yesu Kristo kupitia funzo la Biblia ni jitihada yenye kuthawabisha.