Shiriki Ujuzi Sahihi Juu ya Yesu Kristo
1 Katika huduma yetu ya shambani wakati wa Juni, tutakuwa tukitoa kile kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Utasema nini ili kuanzisha mazungumzo ya Biblia kwa wakati unaofaa, na utatoaje utangulizi wa kitabu hiki bora zaidi?
2 Kutumia Trakti Zetu Mpya: Wahubiri fulani wamepata mafanikio kwa kutumia trakti ili kutambua kupendezwa kwa mtu hata kabla ya kutoa fasihi nyingineyo. Twaweza kusaidiwaje kutimiza jambo hili? Kwa kuzungumzia trakti yetu mpya Je! Ulimwengu Huu Utaokoka?
Baada ya salamu inayofaa, unaweza kusema:
◼ “Tunawauliza watu ikiwa wanakubali kwamba Yesu Kristo alikuwa ndiye yule mtu mkuu zaidi aliyepata kuishi. [Ruhusu wakati wa jibu.] Bila shaka, watu wengi wameathiri mwendo wa mambo ya binadamu, na wengine wamechangia maendeleo ya ainakibinadamu, lakini angalia kinachomtofautisha Yesu Kristo na wengine wote. [Soma Yohana 17:3.] Hakuna mwingineye yote aliye na uwezo wa kuwapa ainabinadamu uhai wa milele. [Fungua ukurasa 3 wa trakti hiyo.] Yesu alipokuwa hapa duniani, alieleza matukio ambayo yangetokea kabla ya mwisho wa ulimwengu. Lakini pia alitia moyo wanafunzi wake washangilie kwa sababu matukio haya yangemaanisha kwamba ukombozi ulikuwa karibu.” Baada kuzungumzia kifupi baadhi ya ishara za kuwapo kwa Kristo, elekeza uangalifu kwenye ukurasa wa nyuma, ambao unaonyesha baraka za utawala wake wa Ufalme.
3 Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani: Kuishi katika ulimwengu mpya wenye amani kwamaanisha nini kwako? Kwa ujumla, watu hufikiri juu ya mandhari zenye kupendeza za mito yenye fahari na mabonde yaliyo shwari, kukiwa na wanyama wanaoishi kwa amani wao kwa wao. Wale wanaotaabishwa na hali za ulimwengu za sasa huenda wakaona taraja la ulimwengu wenye amani kuwa lenye kuburudisha sana.
4 Je! umejitayarisha kutoa jambo fulani la kuburudisha na lenye kupendeza kwa majirani zako, wafanyakazi wenzako, wanashule wenzako, na wale unaokutana nao nyumba kwa nyumba?
Ukitumia trakti “Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani,” unaweza kusema hivi:
◼ “Je! unafikiri inawezekana watu kuishi kwa amani kama inavyoonyeshwa kwenye jalada la trakti hii? [Ruhusu mwenye nyumba ajibu.] Tafadhali angalia sentensi ya mwisho ya fungu la kwanza kwenye ukurasa 2. Inauliza: ‘Lakini je! hiyo ni ndoto tu, au wazo la msisimuko tu, kuamini kwamba hali hizo zitakuja kuwako duniani?’ [Halafu soma fungu linalofuata katika trakti.] Nukuu hilo kuhusu mbingu mpya na dunia mpya linatoka katika Biblia, kwenye 2 Petro 3:13. Ikiwa ni sawa kwako kuchukua Biblia yako, twaweza kusoma Zaburi 104:5 ili tujifunze zadi juu ya wakati ujao wa dunia.” Au unaweza tu kusoma mstari huo kutoka Biblia yako. Mtu huyo akionyesha kupendezwa, elekeza mazungumzo kwenye kitabu Mtu Mkuu Zaidi, sura ya 133.
5 Ziara za kurudia zaidi zitahitaji kufanywa ili ‘kuitia maji’ mbegu iliyopandwa. (1 Kor. 3:6, 7) Makala iliyo chini yadokeza jinsi funzo laweza kuanzishwa katika kitabu Mtu Mkuu Zaidi, iwe ni wakati wa ziara ya kwanza au wa ziara yako ya kurudi.