Sanduku La Swali
◼ Ni nini litakalofikiriwa kuwa vao linalofaa unapojitoa kwa ajili ya ubatizo?
Ijapokuwa viwango vya nguo vyatofautiana katika sehemu tofauti za ulimwengu, onyo la Biblia la kujipamba ‘kwa adabu nzuri na moyo wa kiasi’ labaki lilelile kwa Wakristo wote, bila kujali wanakoishi. (1 Tim. 2:9) Kanuni hii yapaswa kutumiwa inapofikiriwa juu ya vao linalofaa kwa ajili ya ubatizo.
Mnara wa Mlinzi wa Agosti 1, 1985, ukurasa 29, latoa shauri hili kwa mtu anayebatizwa: “Bila shaka kiasi chapasa kuonyeshwa na namna ya vazi la majini linalotumiwa. Hilo ni jambo la maana leo wakati ambao wabuni wa mitindo yaelekea wanataka kuonyeshana mambo ya ngono na kutokeza karibu hali ya uchi kabisa. Jambo jingine la kufikiria ni kwamba mavazi mengine yanayoonekana kuwa yenye kiasi yanapokuwa makavu hayawi hivyo yanapolowa na maji. Hakuna yeyote anayebatizwa angependa kuondosha fikira kando au kuwa kikwazo wakati wa tukio zito kama ubatizo.—Wafilipi 1:10.”
Kupatana na shauri hili, wale wanaobatizwa wangependa kuvaa mavazi ya kiasi, wakiweka akilini umaana wa tukio hilo. Hivyo, vazi la kuogelea lililo jembamba au lenye kushikilia mwili linapolowa maji litakuwa vao lisilofaa kwa Mkristo na lapasa kuepukwa. Kanga, au vazi linalofanana nayo, yaelekea itafaa kuliko marinda makubwa au nguo ambazo huelekea kuinuka ndani ya maji. Vivyo hivyo, haitafaa mtu awe mchafu au mzembe katika kuonekana kwake. Zaidi ya hilo, haingefaa kuvaa T-shati zilizo na misemo ya kilimwengu au maandishi ya kibiashara.
Wakati wazee watakapopitia maswali ya ubatizo na wataka kubatizwa, huu ndio utakaokuwa wakati mzuri wa kuongea umaana wa kuvaa vao linalofaa. Kwa njia hii, adhama ya tukio hilo itasitawishwa na tutaendelea kusimama tukiwa tofauti na ulimwengu.—Linganisha Yohana 15:19.