Habari Za Kitheokrasi
Albania: Kuanzia Desemba 1991 hadi Desemba 1992, idadi ya wahubiri iliongezeka kutoka 24 hadi 107. Hesabu ya mafunzo ya Biblia ilikuwa juu kutoka 4 hadi 221 kwa kipindi kilekile.
Ethiopia: Programu ya 1993 ya kusanyiko la mzunguko ilimalizika hivi karibuni kukiwa na jumla ya hudhurio 6,151 na 60 wakabatizwa.
Jamuhuri ya Afrika ya Kati: Katika Januari 20, 1993, serikali ilitoa amri ya kuruhusu kuanzishwa tena kwa utendaji kamili wa Mashahidi wa Yehova. Akina ndugu huko wanaonea shangwe kwa kuweza kutumia Majumba ya Ufalme yao na kuweza kuwa na “Wachukuaji Nuru” Mkusanyiko wa Wilaya waziwazi. Jumla ya 4,739 walihudhuria mikusanyiko sita iliyofanywa, na 121 wakabatizwa.