Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/00 uku. 4
  • Tumia Trakti Kuanzisha Mazungumzo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumia Trakti Kuanzisha Mazungumzo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Kutumia Trakti Ili Kuwa na Matokeo Yenye Manufaa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Tumia Trakti Kueneza Habari Njema
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Kutanguliza Habaris Njema—Kwa Kutumia Trakti kwa Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Sababu kwa Nini Trakti ni Zenye Thamani Katika Huduma Yetu Leo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 1/00 uku. 4

Tumia Trakti Kuanzisha Mazungumzo

1 Je, hutakubali kwamba kutoa ushahidi wenye matokeo hutegemea ikiwa utachukua fursa ya kwanza kuanzisha mazungumzo? Ugumu huwa ni kusema jambo fulani ambalo litaamsha kupendezwa kwa mtu na kumshirikisha. Lakini hili laweza kufanywaje kwa matokeo?

2 Wahubiri wengi wamepata kwamba kwa kutumia maneno machache yaliyochaguliwa vizuri, kutoa mojawapo ya trakti zetu zenye msingi wa Biblia kwaweza kuanzisha mazungumzo. Vichwa vyapendeza na picha zina rangi nzuri na zavutia. Trakti haina mambo mengi yanayofanya mtu aone kana kwamba ana habari nyingi sana ya kusoma. Hata hivyo, habari fupi iliyoko katika trakti huvutia uangalifu na yaweza kuongoza kwenye funzo la Biblia.

3 Hivyo ndivyo Shahidi mmoja alihisi: “Katika ulimwengu huu wenye shughuli nyingi, kwa kawaida watu hawataki kutumia wakati mwingi kusoma, lakini trakti hizi ni ndefu vya kutosha tu kutoa ujumbe muhimu lakini si ndefu sana hivi kwamba zinawafanya watu wasitake hata kuitazama. Nilisoma trakti nyingi hatimaye nikajifunza kweli.” Usidharau kamwe nguvu za Neno la Mungu kama lilivyoelezwa katika ujumbe huo mfupi, uliochapwa.—Ebr. 4:12.

4 Hatua Nne Sahili: Watu wengi wamefurahia matokeo mazuri kwa kutumia mfikio sahili. (1) Mwonyeshe mtu trakti kadhaa na umuulize ni ipi inayompendeza. (2) Akichagua moja, muulize swali lililotayarishwa vizuri ambalo litakazia jambo kuu la trakti hiyo. (3) Katika kujibu swali hilo, soma fungu fulani linalofaa au andiko kutoka kwenye trakti. (4) Ikiwa anaitikia vizuri, endelea kuzungumzia mambo yaliyomo katika trakti au urejezee somo fulani katika broshua Anataka au sura fulani katika kitabu Ujuzi ambayo itatoa maelezo zaidi. Kwa njia hii waweza kuongoza moja kwa moja kwenye funzo la Biblia. Madokezo yafuatayo yatakusaidia utayarishe mambo uwezayo kusema kwa kutumia trakti nne kati ya hizo.

5 Kichwa cha trakti “Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu?” chaweza kutajwa kama swali.

◼ Ikiwa mtu unayezungumza naye anajibu ni “Mungu” au “sijui,” soma sentensi mbili za kwanza kwenye ukurasa wa 2 na fungu la kwanza kwenye ukurasa wa 3. Kazia 1 Yohana 5:19 na Ufunuo 12:9. Iwe mtu huyo anakubali kuwepo kwa Shetani Ibilisi au la au awe anakubali kwamba Shetani ana uvutano kwa ulimwengu, waweza kuendeleza wazo hilo chini ya kichwa “Dalili Katika Hali za Ulimwengu” ili kuendeleza mazungumzo. Ikiwa aonyesha kupendezwa, eleza Ibilisi alitoka wapi, ukitumia hoja zilizo kwenye ukurasa wa 3 na 4 wa trakti hiyo.

6 Ile trakti “Kuna Tumaini Gani kwa Wapendwa Waliokufa?” yaweza kuamsha kupendezwa mara moja. Waweza kuanzisha mazungumzo kwa kuuliza:

◼ “Je, wafikiri tutapata kuwaona wapendwa wetu waliokufa tena?” Mtu huyo akiisha jibu, elekeza kwenye fungu la pili kwenye ukurasa wa 4 wa trakti hiyo na usome Yohana 5:28, 29. Kisha eleza kwamba inasaidia kuelewa habari iliyo katika kichwa kidogo cha kwanza. Jitolee kuizungumzia pamoja naye.

7 Trakti “Furahia Maisha ya Familia” inawavutia wote katika familia. Ukiitumia, waweza kusema:

◼ “Labda utakubali kwamba leo familia inatishwa. Wafikiri ni nini liwezalo kufanywa ili kuimarisha vifungo vya familia?” Mtu huyo akiisha jibu, mwelekeze kwenye hoja zilizo kwenye fungu la kwanza kwenye ukurasa wa 6. Chagua mojawapo ya Maandiko yaliyonukuliwa kwenye ukurasa wa 4 na 5 wa trakti hiyo, na ueleze maana yake. Kisha mtolee funzo la Biblia nyumbani bila malipo.

8 Ile trakti “Sababu kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia” yaweza kutumiwa kwa utoaji huu:

◼ “Watu wengi wamesikia hadithi ya Kaini na Abeli, ambayo yapatikana katika kitabu cha kwanza cha Biblia. Simulizi la Mwanzo pia hurejezea mke wa Kaini. Je, umewahi kujiuliza alitoka wapi? Tumia fungu la mwisho kwenye ukurasa wa 2 wa trakti hiyo kutoa jibu. Eleza kwamba trakti hiyo pia huzungumzia maelezo muhimu ya Biblia kuhusu wakati wetu ujao. Kuanzia na fungu la tatu katika ukurasa wa 5, endeleza mazungumzo, ukitumia maandiko yanayounga mkono.

9 Kugawanya trakti za Biblia ni njia moja yenye matokeo ya kutoa habari njema ambayo imetumika kwa muda mrefu. Kwa sababu ni rahisi kuzibeba popote uendapo, unaweza kuzitumia kwa matokeo katika huduma ya nyumba hadi nyumba na wakati unahubiri kivivi hivi. Trakti huwa na sehemu muhimu katika huduma yetu. Hakikisha unabeba trakti tofauti-tofauti, na uzitumie kwa wingi kuanzisha mazungumzo.—Kol. 4:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki