Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/93 uku. 4
  • Uwe Mwenye Nafsi Yote Katika Utumishi Wako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe Mwenye Nafsi Yote Katika Utumishi Wako
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Ripoti Utumishi wa Shambani kwa Usahihi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Wahudumu wa Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
  • Kutoa Utegemezo kwa Mapainia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2009
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 8/93 uku. 4

Uwe Mwenye Nafsi Yote Katika Utumishi Wako

1 Tukiwa wanafunzi wa Yesu, tumepewa mgawo wa kuhubiri habari njema juu ya Ufalme wa Mungu na kufanya wanafunzi wa Yesu Kristo. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Hakuna kazi yoyote katika dunia hii ambayo yalingana na uharaka na umaana wayo. Maisha za mamilioni za watu zahusika. Inahitaji juhudi zetu za pekee. Onyo la upole la Paulo latumika: “Lo lote mfanyalo, lifanyeni kwa moyo [nafsi yote, NW], kama kwa Bwana [Yehova, NW].” (Kol. 3:23) “Nafsi yote” inafafanuliwa kuwa na “idili yenye shauku au ujitoaji wa nia-moja.” Je! wewe hujitoa kwa nafsi yote katika utumishi wako?

2 Kuwa wenye nafsi yote kunataka nini kwa upande wetu? Yehova alirejezea utumishi wenye kukubalika kuwa zaka, au sehemu ya kumi. (Mal. 3:10) Badala ya kuonyesha kiwango hususa, sehemu ya kumi hufananisha wakati na nishati tunazotoa kwa utumishi wa Yehova kuwa wonyesho wa upendo wetu kwake na kutambua wakfu wetu kwake. (w92-SW 12/1 uku. 15) Utendaji wetu wapaswa kuonyesha kina cha ujitoaji na upendo wetu kwa Yehova. Mtu aliye mwenye nafsi yote huhisi akisukumwa kumtumikia Yehova kikamili iwezekanavyo kadiri afya na hali yake inavyoruhusu.

3 Paulo aliongea vizuri juu ya Wakristo ‘wanaojitaabisha na kujitahidi’ kwa sababu ya tumaini. (1 Tim. 4:10) Wanathawabishwa kwa baraka za Yehova, ambazo ‘huwatajirisha.’ (Mit. 10:22) Kwa kinyume, wale ambao hutoa wakati na nishati zao kwa uhaba au kwa unyimivu wanakosa kuona furaha inayotokana na kutoa. (Mdo. 20:35) Kupuuza kutoa yaliyo bora kwa kweli humnyang’anya Yehova ‘sehemu ya kumi’ tunayodaiwa naye.—Mal. 3:8.

4 Kutoa Yaliyo Bora Zaidi: Tunaposhiriki katika utumishi wa shambani na kutoa ripoti yetu, je, ripoti hiyo huwa sahihi? Kitabu Huduma Yetu, ukurasa 104, husema: “Wakati wako wa utumishi wa shambani umepasa uanze unapoanza kazi yako ya kutoa ushuhuda na kwisha unapomaliza ziara yako ya mwisho katika kila kipindi cha kutoa ushuhuda. Wakati unaotumiwa kupata viburudisho au vyakula wakati wa kipindi cha utumishi wa shambani si wa kuhesabiwa.” Upangaji mzuri na jitihada vyahitajiwa ili kutimiza mengi zaidi wakati tupo katika utumishi wa shambani.

5 Kutoa yaliyo bora zaidi kwamaanisha kwamba tufanye mengi tuwezayo tunaposhiriki katika huduma ya shambani. Mtu mwenye nafsi yote hatapunguza kimakusudi kuhubiri kwake kwa kujaribu tu kutoa ushahidi wa vivi-hivi badala ya kushiriki katika mlango kwa mlango. Kijana mwenye nafsi yote, aliye mhubiri asiyebatizwa, hataenda kuhubiri tu kwa kusisitizwa na wazazi wake, akionyesha kupendezwa kidogo kwenda milangoni au kushiriki katika kufanya utoaji.

6 Paulo atusihi tudumishe bidii yetu ili tusiwe wazembe. (Ebr. 6:11, 12) Ni shangwe kama nini kuweza kupitia utumishi wetu binafsi na kutokuwa na sababu ya kuaibikia—kwa sababu tumekuwa wenye nafsi yote! (2 Tim. 2:15) Shangwe yetu kubwa zaidi itatambuliwa tunapoona watu tuliosaidia wenyewe wakiwa miongoni mwa waokokaji wa dhiki kuu. Hakika, Yehova huthawabisha sana wale wanaomtumikia kwa nafsi yote.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki