Programu Mpya ya Siku ya Kusanyiko la Pekee
1 Funzo letu la Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi limeongeza uthamini wetu kwa Yesu Kristo. Kwa kufaa, programu ya siku ya kusanyiko la pekee kuanzia Septemba itakazia kichwa “Kufuata kwa Ukaribu Kielelezo Chetu Kikuu,” ikitusaidia tuelewe kikamili zaidi linalomaanishwa na kumfuata.
2 Bila kujali umri au miaka ambayo mtu amekuwa katika kweli, wote watakaohudhuria kusanyiko watatiwa moyo kuwa mfano wa Kristo. Sehemu ya programu hiyo itakazia shauri kwa vijana hasa. Itawasaidia kukabiliana na hali ngumu kuhusiana na elimu, vitumbuizo, na vitu vya kimwili. Kutakuwako na hotuba, mambo yaliyoonwa, na maonyesho yakikazia jinsi ya kukinza shawishi la ulimwengu na kufuata Kristo.—1 Pet. 2:21.
3 Watu wapya waliojiweka wakfu watakuwa na fursa ya kuonyesha hivyo peupe kwa kubatizwa na kuwa wafuasi wa Kristo. Mazungumzo ya Kimaandiko yenye kuchochea yatatangulia sherehe ya ubatizo. Wale wanaotaka kubatizwa katika siku ya kusanyiko la pekee wanapaswa kumjulisha mwangalizi msimamizi kwa wakati unaofaa ili apange na wazee wapitie maswali ya wataka-kubatizwa.
4 Msemaji mgeni atatoa hotuba kuu, yenye kichwa, “Kufuata Kielelezo Chetu Kikuu—Kwaongoza Kwenye Nini?” Hakikisha umekaribisha wote wenye kupendezwa kwenye programu hii yenye kutia moyo na kutia imani nguvu. Hakuwezi kuwa na sababu kubwa zaidi au yenye kuthawabisha kuliko kumfuata Kielelezo Chetu Kikuu, Yesu Kristo.—Mt. 19:27-29.