Kutumia Magazeti Yetu Nyumba kwa Nyumba
1 Kusudi la Amkeni! lasemwa waziwazi kwenye ukurasa 4 wa kila toleo: “Gazeti hili hujenga uhakika katika ahadi ya Muumba ya kuleta ulimwengu mpya wenye amani na usalama kabla kizazi kilichoona matukio ya 1914 hakijapitilia mbali.” Kwelikweli gazeti kama hilo lastahili mwenezo mkubwa kadiri iwezekanavyo katika huduma yetu ya nyumba kwa nyumba!
2 Amkeni! ni njia bora sana ya kuamsha kupendezwa kwa watu ambao huenda wasiwe na mbetuko wa kiroho. Unaposoma kila toleo, tafuta mambo yafaayo ya kushiriki na wengine. Wahubiri fulani huandika habari katika nakala zao binafsi, na kabla ya kuenda katika utumishi wa shambani na toleo hilo hususa, wao hupitia mambo waliyoandika ili kuwa na mambo hususa akilini ya kushiriki na wenye nyumba.
3 Huenda tukachagua kuanza utoaji wetu kwa kutoa maelezo ya moja kwa moja juu ya habari iliyozungumzwa katika toleo la Amkeni! tunalotumia.
Ikiwa mwenye nyumba aonyesha kupendezwa, twaweza kujulisha gazeti, labda kwa kusema hivi:
◼ “Makala hii ya Amkeni! inazungumzia kirefu juu ya habari hiyo.” Halafu soma sentensi moja au mbili ulizotangulia kuchagua, na uendelee hivi: “Kwa kuwa waonekana kupendezwa na habari hii, je, ungependa kusoma makala hii kutia na makala zile nyinginezo za wakati unaofaa katika toleo hili la Amkeni!? Ikiwa ndivyo, ningefurahi kukuachia hili pamoja na gazeti jenzilo Mnara wa Mlinzi, kwa mchango wa ——.”
4 Ikiwa mwenye nyumba aonyesha kupendezwa waziwazi na mambo ya kiroho, huenda tukasoma andiko fulani, kama vile 2 Timotheo 3:1-5 juu ya siku za mwisho. Baada ya hilo, ili kuamsha kupendezwa kwake na magazeti yetu, tungeweza kusoma moja kwa moja ile sehemu katika ukurasa wa 2 wa toleo la karibuni la Mnara wa Mlinzi inayosema: “Kusudi la Mnara wa Mlinzi . . .” Baadaye, mpe matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kwa mchango wa kawaida.
5 Ukikutana na mtu anayependezwa kikweli, huenda ukataka kusema jambo kama hili:
◼ “Katika jumuiya hii, twakutana na watu wa dini mbalimbali zilizo tofauti kabisa na yetu. Jitihada ya ainabinadamu ya kutafuta Mungu imechukua pande nyingi tofauti-tofauti. [Soma Matendo 17:26, 27.] Je! unakubali kwamba watu kwa kawaida hufuata dini ya wazazi wao, badala ya kutafuta Mungu wao wenyewe? [Ruhusu elezo.] Hilo ndilo jambo linalosemwa katika sura ya kwanza ya kitabu hiki, Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu. [Kazia habari katika fungu la 12 kwenye ukurasa wa 8.] Kujifunza zaidi juu ya dini nyinginezo kunafundisha na pia kuelimisha. Kitabu hiki hueleza asili, mazoea, na mafundisho ya dini mashuhuri za ulimwengu.” Kadiri wakati uruhusuvyo, onyesha mwenye nyumba orodha ya sura na kielezi kimoja au viwili katika kitabu.
6 Tuendapo nyumba kwa nyumba, acheni tukumbuke kwamba tuna viwili kati ya vifaa bora zaidi ulimwenguni kuwasaidia watu wafanye maendeleo ya kiroho, yaani Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Na tujitahidi kuchochea kupendezwa kwa wenye nyumba katika magazeti hayo na kuyaangusha katika kila fursa.