Wasaidie Wengine Wajifunze Juu ya Mwana wa Mungu, Yesu Kristo
1 Desemba ni mwezi ambao wengi wanaodai kuwa Wakristo humfikiria Yesu zaidi kuliko wakati mwingine wowote mwakani. Hivyo, ni mwezi mzuri wa kutoa kile kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Kwa kuwa kusoma juu ya mwana wa Mungu kutawapendeza watu wengi katika eneo letu twataka kutoa kichapo hicho kwa wote tukutao. Twaweza kutoaje kichapo hicho?
2 Jaribu kuingia moja kwa moja kwenye mazungumzo ya Biblia yanayokazia uangalifu kwa Yesu.
Baada ya kumsalimia mwenye nyumba, unaweza kusema hivi:
◼ “Leo twauliza jirani zetu wanalofikiria wanaposoma katika Biblia zao juu ya kuishi milele. [Ruhusu itikio.] Ni jambo lenye kupendeza kwa sababu Biblia husema juu ya uwezekano huo karibu mara 40. Maisha hayo yaweza kumaanisha nini kwetu? Angalia yale ambayo Ufunuo 21:4 husema. [Soma.] Je! ulitambua kilichoahidiwa? [Ruhusu itikio.] Twaweza kupataje uhai wa milele?” Soma Yohana 17:3, na ukazie uhitaji wa kutwaa ujuzi wa Mungu na wa Mwanawe, Yesu Kristo. Kisha mwonyeshe mwenye nyumba kitabu Mtu Mkuu Zaidi, ukitumia vichwa vidogo kwenye utangulizi ili kuamsha zaidi kupendezwa kwake.
3 Ikiwa mwenye nyumba hana uwezo wa kuchukua kitabu basi, toa matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! au ile trakti Je! Ulimwengu Huu Utaokoka? Toa uangalifu kwenye jambo moja au mawili hususa katika kichapo kinachotolewa. Jitolee kurudi wakati unaofaa ili kuendelea kuzungumzia jambo hilo naye.
4 Mwenye nyumba akionekana kuwa na shughuli nyingi, lingekuwa jambo la hekima kufupisha utoaji ulio juu. Wahubiri wapya huenda wakaona utoaji unaofuata kuwa rahisi kuutumia.
Baada ya kujijulisha, twaweza kusema:
◼ “Leo twauliza jirani zetu wanalofikiria wanaposoma katika Biblia zao juu ya kupata uhai wa milele. Kwa kielelezo, ona yale Yesu alisema kwenye Yohana 17:3. [Soma.] Kitabu hiki kimechapishwa ili kisaidie watu wajifunze juu ya Yesu Kristo na mambo aliyofundisha.” Fungua kitabu Mtu Mkuu Zaidi kwenye baadhi ya vielezi maridadi. Fungua utangulizi, na usome fungu la pili chini ya kichwa kidogo “Faidika kwa Kujifunza Juu Yake.” Kisha mtolee kichapo hicho.
5 Ukiangusha kitabu hicho, weka msingi wa funzo la Biblia kwa kujitolea kuzungumzia sura ya kwanza, “Jumbe Kutoka Mbinguni,” wakati huo au katika ziara ya kurudia siku chache baadaye. Badala ya kumtajia mwenye nyumba kipindi hususa cha wakati utakaotumiwa katika ziara itakayofuata, sema tu kwamba kwa muda wa dakika chache, anaweza kujifunza habari zaidi yenye kupendeza juu ya Yesu Kristo kutoka kwa Neno la Mungu, Biblia.
6 Acheni sisi sote tutumie sikukuu hii ya kilimwengu kukaza uangalifu juu ya kweli kuhusu Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, ili tusaidie wengine kuelekea barabara ya uhai wa milele.—Mt. 7:14.