Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Wakati wa Desemba
1 Yesu aliwaamuru wanafunzi wake wawe walimu wa habari njema. (Mt. 28:19, 20) Njia yetu ya msingi ya kufundisha wengine ni kwa kuongoza mafunzo ya Biblia. Je! wewe washiriki katika kazi hii? Ikiwa sivyo, waweza kuanzishaje funzo ili ufurahie sehemu kubwa ya kufundisha wengine?
2 Labda tulimpatia mwenye nyumba nakala ya trakti na tukaahidi kurudi ili kuzungumzia yaliyomo.
Tunaporudia mwenye nyumba ambaye tulimwachia trakti “Je Ulimwengu Huu Utaokoka?,” twaweza kusema:
◼ “Nilipokuwa hapa siku chache zilizopita, tulizungumzia umaana wa siku zetu na kwamba Yesu alisimulia kwa usahihi hali zilizopo katika siku zetu. Ningependa kutumia dakika chache na kuangalia kifupi habari fulani kutoka kwa trakti niliyokuachia. Angalia mambo yaliyoandikwa chini ya kichwa kidogo ‘Ile Ishara.’” Fungua ukurasa wa 3 wa trakti hiyo, na uzungumzie mafungu mawili au matatu chini ya kichwa kidogo hicho, ukisoma maandiko yaliyowekwa bila manukuu wakati ukiruhusu. Onyesha jinsi unabii wa Yesu unavyotimizwa leo. Panga ziara ya kurudia na uzungumze mafungu yale mengine chini ya kichwa kidogo hicho. Mtie moyo mwenye nyumba asome habari hiyo kabla hujarudi.
3 Au waweza kusema hivi:
◼ “Wakati uliopita tulipozungumza, nilikuachia trakti Je! Ulimwengu Huu Utaokoka? Wakati huo tuliongea juu ya daraka la Yesu Kristo katika mambo ya ulimwengu. Tulisoma maneno yake yaliyorekodiwa katika Biblia kwenye Yohana 17:3. [Soma.] Kwa kuwa ni muhimu tujifunze juu ya Mungu na Yesu ikiwa twataka uhai wa milele, inafaa kufanya yale tuwezayo tutwae ujuzi huo. Yesu alipokuwa duniani, alionyesha sifa nyingi nzuri ajabu za Mungu. Je! si jambo la kiakili kuamini kwamba kadiri tunavyokuja kumjua Yesu na huduma yake, ndivyo twaja kumjua Baba yake? [Ruhusu itikio.] Angalia vile kitabu hiki, Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi kinavyosema.” Soma fungu la kwanza na la pili katika ukurasa wa kumi wa sura ya 116. Kazia kwamba kitabu hiki kina habari yote iliyo katika masimulizi ya Gospeli nne juu ya Yesu na chaweka habari hiyo katika mpangilio wa vile matukio yalivyotendeka. Onyesha vichwa hususa vya sura, vielezi, na ramani mwanzoni mwa kitabu. Mtolee mtu huyo kichapo hicho.
4 Baada ya kumsalimu mwenye nyumba aliyekubali kitabu “Mtu Mkuu Zaidi,” twaweza kusema:
◼ “Kama nilivyotaja katika ziara yangu iliyopita, kitabu Mtu Mkuu Zaidi kimetayarishwa kwa ajili ya funzo la Biblia. Ningependa kuonyesha kifupi jinsi chaweza kutumiwa kwa matokeo.” Fungua kitabu ukurasa wa 1, “Jumbe Kutoka Mbinguni.” Vuta uangalifu wa mwenye nyumba kwa maswali yaliyochapishwa. Soma swali la kwanza, kisha angalieni mafungu ya kwanza. Unganisha kielezi kwenye ukurasa wa pili. Zungumzia maswali yaliyobaki, na ukazie majibu kadiri wakati uruhusuvyo. Kabla ya kumalizia ziara, panga kurudi na kuendeleza mazungumzo.
5 Kwa kudumisha mwelekeo unaofaa, kutayarisha vizuri, na kutumia kwa manufaa kila fursa, tutajiandaa vema kuanzisha funzo la Biblia wakati wa Desemba.