Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/94 uku. 4
  • Kurudi Ili Kujenga Uthamini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kurudi Ili Kujenga Uthamini
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Jenga Kupendezwa kwa Kufanya Ziara za Kurudia Zenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Saidia Watu Walio Mfano wa Kondoo Wajenge Juu ya Msingi Imara
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Jipe Ujasiri wa Kufanya Ziara za Kurudia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Rudi kwa Shangwe ili Kusaidia Wenye Kupendezwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 1/94 uku. 4

Kurudi Ili Kujenga Uthamini

1 Ziara za kurudia zinazofaa zachochea na kuzidisha kwa kuendelea ukuzi wa mwenye nyumba kuelekea kuwa mwamini. Ni baadhi ya madokezo gani ya kukumbuka unapotembelea tena wale ambao wameonyesha kupendezwa?

2 Kwanza, tayarisha vema. Hilo huanza katika ziara ya kwanza. Jinsi gani hivyo? Kwa kuweka maandishi sahihi ya kupendezwa kulikoonyeshwa. Andika jina la mwenye nyumba, jambo lililozungumzwa, itikio, na chochote kilichoangushwa. Kisha pitia maandishi yako ya nyumba kwa nyumba kabla ya kurudi, na ufikirie kwa sala jambo utakalosema.

3 Sasa uko tayari. Unaweza kusema nini? Ikiwa ulimwacha mwenye nyumba na swali mara ya kwanza, basi waweza kujenga juu ya somo hilo unaporudi. Kwa kielelezo, ikiwa ziara ya kwanza ilikazia baraka za Ufalme wa Mungu, unaweza kutokeza lile swali “Kwa nini Mungu anaruhusu uovu?”

Unaporudi, baada ya kujijulisha, waweza kusema:

◼ “Tulipoongea wakati uliopita, tulizungumza sababu ya Mungu mwenye upendo kuruhusu uovu mwingi leo. Je! umepata kufikiria jambo hilo? [Ruhusu itikio.] Je! wafikiri Mungu kweli anajali ainabinadamu? [Ruhusu itikio.] Fikiria yale ambayo Biblia husema kwenye Yohana 3:16.” Baada ya kusoma mstari huo, waweza kuvuta uangalifu sehemu hususa za sura ya 8 katika kitabu Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele, ambayo inaonyesha sababu za Mungu kuvumilia uovu leo.

4 Swali jingine lenye kunasa fikira unaloweza kuacha katika ziara yako ya kwanza litakuwa: “Ikiwa Mungu alikusudia mwanadamu aishi milele, kwa nini watu wanazeeka na kufa?” Unaporudi, unaweza kuwaonyesha jibu la Biblia kwa swali hilo kama lipatikanavyo kwenye Warumi 5:12. Baada ya kusoma andiko hilo, rejezea fungu la mwisho katika ukurasa wa 34 wa kitabu Je! Uzima Ndio Uu Huu Tu?, ambacho huongea juu ya sababu ya msingi ya mwanadamu kuzeeka na kufa.

5 Ikiwa mlizungumza juu ya njia za kutambua dini ya kweli katika ziara ya kwanza na ukaacha kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, swali zuri ambalo laweza kuwa msingi wa ziara yako ya kurudia laweza kuwa: “Dini nyingi zaidi zilitokeaje?” Unaporudi, waweza kuongea juu ya mambo mahususi katika sura ya 2 ya kitabu hicho.

6 Hapa kuna shauri la tahadhari. Toa uangalifu kwa maswali unayouliza unaporudi. Unapouliza “Ulisoma habari niliyokuachia?” au “Wanikumbuka mimi?” au “Wakumbuka yale tuliongea wakati uliopita nilipokuwa hapa?” humfanya mwenye nyumba ahisi isivyofaa. Maswali kama hayo kwa kawaida hayatokezi matokeo mazuri. Kwa upande mwingine, kuwa mwenye urafiki, mwenye kubadilika, na mwenye ufupizo. Sifa hizi zitachochea ujumbe.

7 Mifikio hii na mingineyo yaweza kutumiwa ili kusitawisha uthamini katika mioyo ya wenye kupendezwa. Kwa nini usiweke mradi wa kibinafsi wa kufanya angalau ziara moja ya kurudia kila juma? Tumia madokezo yaliyotolewa juu, na utafute wahubiri stadi ambao watakusaidia. Shangwe yako itaongezeka ujengapo kwenye kupendezwa kwa mara ya kwanza kwa kufanya ziara za kurudia zenye matokeo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki