Mpe Heko Mzaliwa wa Kwanza wa Yehova!
1 Jumapili, Nisani 9, 33 W.K., umati mkubwa ukiwa na matawi ya mitende mikononi mwao walimpa heko Mwana mzaliwa wa kwanza wa Yehova, Bwana Yesu Kristo kuwa “Yule ajaye akiwa Mfalme katika jina la Yehova!” (Luka 19:38, NW; Ebr. 1:6) Jumatatu na Jumanne, Nisani 10 na 11, Yesu alijishughulisha zaidi na huduma yake ya peupe, akizifanya ziku hizo za kumalizia ziwe miongoni mwa zile zenye shughuli zaidi katika maisha yake ya kidunia.
2 Leo, umati ulio mkubwa hata zaidi wakiwa na matawi ya mitende ya kitamathali mkononi walia kwa sauti kuu hivi: “Wokovu una Mungu wetu aketiye katika kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo.” (Ufu. 7:9, 10) Katika Machi 26, tutakutana kuadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Kristo. Tarehe hiyo ikaribiapo, je, twaweza kutia juhudi zetu katika huduma na hivyo kuongezea mpaazo huu wa sauti ya sifa tufeni pote?
3 Ongeza Utendaji wa Shambani: Wahubiri wengi wamejiandikisha kuwa mapainia wasaidizi wakati wa Machi. Je! ungependa kujiunga nao? Ikiwa ndivyo, lete ombi lako bila kuchelewa. Mmoja wa wazee atafurahi kujibu maswali yoyote ambayo huenda ukawa nayo kuhusu kazi hiyo.
4 Iwe unaweza kutumikia ukiwa painia-msaidizi au la, utataka kuwa na ushiriki kamili katika huduma wakati wa Machi. Kutaniko huenda likaweza kupanga ushahidi wa kikundi kila siku wakati wa mwezi huo. Eneo la kutosha lapaswa kuwekwa kando kwa ajili ya kusudi hilo.
5 Makutaniko yote yapaswa kupanga mkutano wa pekee kwa ajili ya utumishi wa shambani Jumamosi, Machi 26. Ijapokuwa kuna mengi ya kufanya kujitayarisha kwa ajili ya Ukumbusho, inapendekezwa kwamba kila mtu anayeweza kufanya hivyo ashiriki katika huduma ya shambani Jumamosi asubuhi. Pamoja na kuhubiri nyumba kwa nyumba, hakikisha kwamba wale ambao umealika kuhudhuria Ukumbusho wana usafiri na kwamba wanakumbuka mahali na wakati wa mkutano huo vizuri.
6 Karibisha na Utie Moyo Wengine: Yesu aliamuru wafuasi wake hivi: “Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.” (1 Kor. 11:24) Kwa kuwa wafuasi wa Yesu wapakwa wanaofuata hatua zake wanatii amri hiyo, kila mtumishi wa Yehova anakaribishwa kuhudhuria na kuadhimisha sherehe hii ya Ukumbusho. Miongoni mwa wengine, unapaswa kukaribisha wanafunzi wa Biblia, watu wa ukoo, wale ambao umekuwa na mazungumzo ya Biblia pamoja nao, wenzi wa ndoa wasioamini, na watu unaowajua kutokana na kazi yako. Panga orodha ili kwamba yeyote asisahaulike.
7 Kutakuwa na fursa zaidi za kutia moyo watu wenye kupendezwa katika Ukumbusho wenyewe. Hakikisha unafika mapema ili usalimu wapya wanaohudhuria kwa mara ya kwanza. Ikiwa wanafunzi wako kadhaa wa Biblia watahudhuria, itafaa mhubiri mwingine aketi karibu na wengine wao wakati wa mkutano. Karibisha wapya wahudhurie Mkutano wa Watu Wote wa kawaida unaopangwa na kutaniko. Mzee aliyeteuliwa kutoa hotuba ya watu wote apaswa kujitayarisha vizuri ili kutoa hotuba yenye kuchochea.
8 Kwenye umalizio wa sherehe ya Ukumbusho, tunapoimba pamoja wimbo 105, “Mpe Heko Mzaliwa wa Kwanza wa Yehova!,” na tuweze kutazama nyuma na kuridhika kwamba tulitumia mwezi huo wa utendaji wa kitheokrasi kwa bidii kwa sifa ya Yehova!