Mikutano Ya Utumishi Kwa Februari
Juma Linaloanza Februari 7
Dak 15: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Pitia mambo makuu katika Sanduku la Swali.
Dak 18: “Sitawisha Kupendezwa Katika Ufalme wa Mungu wa Amani.” Mazungumzo ya makala pamoja na wasikilizaji. Maonyesho mawili. Baada ya kuangalia fungu la 2, onyesha jinsi ya kutoa trakti kwa mwenye nyumba aliye na shughuli nyingi. Acha mhubiri aulize kwa busara swali ambalo litaweka msingi wa ziara ya kurudia. Toa wonyesho wa utoaji katika fungu la 3 ambamo mwenye nyumba aonyesha kupendezwa na mhubiri atumia kitabu Kuishi Milele. Hapo tena, msingi wapaswa kuwekwa kwa ajili ya ziara ya kurudia.
Dak 12: Mahitaji ya kwenu. Juma hili laweza kutumiwa kushughulikia habari iliyopitwa wakati kutaniko lilipoipitia programu ya “Ufundishaji wa Kimungu.”
Wimbo 137 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 14
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Eleza wonyesho wa Sosaiti wa uthamini kwa upaji wa hiari uliopelekwa, na pongeza kutaniko kwa utegemezo mshikamanifu wa mahitaji ya kutaniko. Tia moyo kushiriki katika utendaji wa shambani wa mwisho-juma.
Dak 20: “Chochea Ukuzi kwa Ziara za Kurudia za Maana.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Toa wonyesho wa ziara ya kurudia ikitegemea utoaji katika fungu la 2. Onyesha uhitaji wa kuwa na utambuzi kwa kutoangalia habari nyingi mno wakati wa ziara ya kurudia, na ukazie umaana wa kukaza kikiki kupendezwa na ziara ifuatayo.
Dak 15: “Yanufaisha Kama Nini Kukumbuka Yale Ambayo Yehova Amefanya!” Mazungumzo ya maswali na majibu ya mafungu 1-11 makala hiyo ya nyongeza. Uwe na maelezo mawili yaliyotayarishwa na kina ndugu ambao wana programu ya binafsi au ya familia ya kusoma kitabu hicho. Waombe wataje jambo ambalo walithamini kujifunza.
Wimbo 122 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 21
Dak 5: Matangazo ya kwenu.
Dak 15: “Mpe Heko Mzaliwa wa Kwanza wa Yehova!” Kupitia makala kwa maswali na majibu. Ikitolewa kwa uchangamfu, kwa idili na mzee, akitia moyo wote wafanye orodha ya watu mmoja mmoja watakaowaalika kuhudhuria Ukumbusho na hotuba ya watu wote ya kawaida itakayofuata. Toa wonyesha wa mambo yaliyo kwenye fungu la 7. Panga mhubiri amfikie mtu ambaye anaingia kwenye Jumba la Ufalme na atazama huku na huku. Mhubiri apata kujua kwamba mtu huyo alitiwa moyo kuhudhuria na mtu wa ukoo anayeishi katika jiji jingine. Mhubiri amkaribisha mtu huyo akae pamoja naye na familia yake ili washiriki naye Biblia na kitabu cha nyimbo. Mhubiri ajitolea kujibu maswali yoyote ambayo mtu huyo huenda akawa nayo baada ya mkutano. Malizia sehemu hiyo kwa kutangaza wakati ambao kutaniko litaadhimisha Ukumbusho.
Dak 10: Biblia—Chanzo Chetu Bora Zaidi cha Kitia-Moyo. Kitabu Kutoa Sababu, kurasa 106-110. Hotuba ikitolewa na mzee. Wengi walio ndani na nje ya kutaniko wanahitaji kitia-moyo. Onyesha jinsi kila mhubiri katika kutaniko anavyoweza kutumia Neno la Mungu kuwatia wengine moyo.
Dak 15: “Watu wa Kuchukiwa na Mataifa Yote.” Hotuba ikitolewa na mzee mwenye maarifa.
Wimbo 208 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 28
Dak 8: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Toa wonyesho wa magazeti ukitegemea matoleo ya karibuni.
Dak 12: “Yanufaisha Kama Nini Kukumbuka Yale Ambayo Yehova Amefanya!” Nyongeza izungumziwe kwa maswali na majibu ya mafungu 12-20. Uwe na maelezo yaliyotayarishwa kutoka kwa wahubiri ambao wamenufaika kwa kukisoma kitabu.
Dak 15: “Unga Mkono Kikamili Programu ya Mkutano wa Watu Wote Inayopangwa na Kutaniko Lenu.” Hotuba, lakini yaweza kutia swali moja au mawili yakielekezwa kwa wasikilizaji. Eleza jinsi watu wenye kupendezwa wanaohudhuria hotuba ya watu wote kwa mara ya kwanza wanavyoweza kuhisi wamekaribishwa. Uwe na elezo moja lililotayarishwa kutoka kwa mhubiri akieleza jinsi amenufaika kwa kuhudhuria hotuba ya watu wote kwa ukawaida.
Dak 10: “Linda Dhidi ya Fadhili Itumiwayo Vibaya.” Hotuba.
Wimbo 197 na sala ya kumalizia.