Sanduku La Swali
◼ Ni utaratibu gani unaopasa kufuatwa maazimio yanapotolewa katika kutaniko?
Azimio latakiwa ikiwa uamuzi utafanywa juu ya mambo muhimu kama vile kununua mali, kurekebisha au kujenga Jumba la Ufalme, kupeleka michango ya pekee kwa Sosaiti, au kutunza kulipia gharama za mwangalizi wa mzunguko, au kuchagua nyakati za mkutano. Kwa kawaida yafaa zaidi kutokeza azimio likubaliwe kila mara fedha za kutaniko zinapotoka
Tofauti yaweza kufanywa katika visa vinavyohusisha mahitaji maalumu yanayohusiana moja kwa moja na miradi au utendaji mbalimbali ulio wa maana. Kwa kielelezo, huenda kutaniko likaazimia mara moja kuchanga kiasi hususa kila mwezi kwa Sosaiti kuelekea kazi ya kuhubiri ulimwenguni pote. Pia, gharama za kawaida za kuendeshea Jumba la Ufalme, kama vifaa vya kazi za kawaida na vya usafi, havihitaji azimio.
Uhitaji uonekanapo, baraza la wazee lapaswa kuongea juu ya jambo hilo kikamili. Ikiwa wote wakubali kwamba jambo fulani lahitaji kufanywa, mmoja wa wazee, labda mshiriki wa Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko, apaswa kutayarisha azimio lililoandikwa litokezwe kwenye Mkutano wa Utumishi.
Mzee anayetenda akiwa mwenyekiti anapaswa kueleza kifupi lakini waziwazi juu ya uhitaji uliopo na jambo ambalo baraza la wazee lapendekeza ili kuutimiza. Kisha kutaniko lapewa fursa ya kuuliza maswali kuhusiana na jambo hilo. Ikiwa jambo hilo ni la kutatanisha, ingefaa kuahirisha uchaguzi hadi Mkutano wa Utumishi ujao ili kumpa kila mtu wakati wa kulifikiria. Uchaguzi wenyewe wafanywa kwa kutaniko kunyoosha mikono.
Kufanya uchaguzi wa azimio ni kwa washiriki wa kutaniko waliojiweka wakfu na waliobatizwa peke yao isipokuwa matakwa ya kisheria yaelekeze vingine, kama vile iwezavyo kuwa wakati mambo ya shirika au mikopo ya Jumba la Ufalme ihusikapo. Haingefaa wageni wa kutoka makutaniko mengine washiriki.
Baada ya azimio kukubaliwa, lapaswa kutiwa tarehe, sahihi, na kuwekwa katika faili ya kutaniko.