Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/94 uku. 8
  • Chochea Ukuzi kwa Ziara za Kurudia za Maana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Chochea Ukuzi kwa Ziara za Kurudia za Maana
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Kusitawisha Kupendezwa Katika Ziara za Kurudia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Kutumia Kitabu Kuishi Milele Katika Ziara za Kurudia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Rudi Usitawishe Kupendezwa Katika Ujumbe wa Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Ziara za Kurudia Sahili na Zenye Matokeo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 2/94 uku. 8

Chochea Ukuzi kwa Ziara za Kurudia za Maana

1 Ili kusaidia wale ambao wameonyesha kupendezwa, ni muhimu tuendelee kuwaandalia mtiririko wa chakula cha kiroho kwa ziara za kurudia za ukawaida. Ziara zetu zitachochea hatua kwa hatua ukuzi wao wa kiroho. (1 Kor. 3:6-9) Hata hivyo, ili ziara zetu ziwe za maana, ni lazima tutayarishe mapema, tukimfikiria mtu huyo.

2 Kuwarudia Wale Tulioachia Trakti: Labda trakti ya Ulimwengu Mpya Wenye Amani iliangushwa katika ziara ya kwanza.

Baada ya kurudia kifupi jambo lililozungumzwa, twaweza kuuliza hivi:

◼ “Ni nani awezaye kuleta mabadiliko hayo? [Ruhusu elezo.] Bila shaka wewe pia utafurahia kuishi katika hali kama hizo. Sisi binafsi twaweza kufurahiaje hali kama hizo?” Kisha habari iliyoko chini ya kichwa kidogo “Jinsi Jambo Hilo Linavyowezekana Kwako Wewe” yaweza kuangaliwa. Mahali ambapo kupendezwa kumeonyeshwa, uangalifu waweza kuelekezwa kwenye kitabu Kuishi Milele, sura 15, “Kuwa Raia wa Serikali ya Mungu.” Twaweza kuzungumzia mafungu mawili ya kwanza kisha tuulize swali hili: “Kujifunza juu ya Mungu kwapaswa kutuathirije?” Mipango yaweza kufanywa ya kujibu swali hilo na kuzungumzia mengi zaidi ya sura hiyo kwenye ziara ifuatayo.

3 Tunapowarudia wale tulioachia broshua “Je! Kweli Mungu Anatujali,” twaweza kusema:

◼ “Nilipokutembelea wakati uliopita tuliongea juu ya matatizo mengi yanayokabili ainabinadamu na yale ambayo Mungu anaahidi kufanya kuyahusu. Lakini, kwa nini Mungu ameruhusu kuteseka kwa muda mrefu sana hivyo? Jibu linalopendeza lapatikana katika sehemu ya 6 ya broshua tuliyotazama.” Mwombe mwenye nyumba alete nakala yake ikiwezekana. Baada ya kuangalia mafungu machache, twaweza kuuliza: “Twahitaji kufanya nini ili tunufaike na ahadi za Mungu?” Habari iliyo chini ya sehemu ya 11, “Msingi wa Ulimwengu Mpya Sasa Unafanyizwa,” kwenye kurasa 28-31, yaweza kukaziwa kwa ajili ya mazungumzo kwenye ziara ifuatayo.

4 Kurudia Wale Tulioachia Magazeti: Ikiwa uliteua makala hususa iliyompendeza mwenye nyumba, sitawisha mambo ya ziada kutoka kwenye makala hiyo unaporudi, ukikazia maelezo yaliyo kwenye andiko moja la msingi na habari inayozungumzia hilo. Ikiwa kuna kupendezwa kwenye kuendelea, faida za magazeti zaweza kuzungumzwa. Pia, uangalifu waweza kutolewa kwa toleo linalofuata la magazeti ikiwa lina makala inayozungumzia jambo sawa na hilo. Au sivyo, twaweza kuelekeza uangalifu kwenye habari iliyo kwenye kitabu Kuishi Milele juu ya jambo hilo na kufanya mipango ya kulizungumzia katika ziara yetu ifuatayo.

5 Kuonyesha kwetu kupendezwa binafsi na kuendelea na ziara za kurudia za maana kutaonyesha upendo wetu kwao na kwa Yehova. (Yoh. 13:34, 35) Na tuendelee kuchochea ukuzi wa kiroho wa wale walio katika eneo letu kwa kufanya ziara za kurudia za maana kwa ukawaida.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki