Sitawisha Kupendezwa Katika Ufalme wa Mungu wa Amani
1 Wakati wa mwezi wa Februari, tutakuwa tukitoa kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Kusudi letu lapaswa kuwa kuwasaidia watu wenye moyo mweupe katika eneo letu kusitawisha uthamini kwa Ufalme wa Mungu na lile utakalotimiza. Maswali ya maoni yaweza kutusaidia kwa jambo hilo.
2 Baada ya salamu ya kirafiki, twaweza kusema hivi:
◼ “Mabadiliko ajabu yatukia duniani pote, na mradi wa amani hutajwa mara nyingi. Je! wafikiri amani ya kweli itafikiwa? [Ruhusu elezo.] Ijapokuwa wengi hutumaini binadamu walete amani, ona jinsi Mungu anavyoahidi kuleta amani kama inavyotajwa kwenye Zaburi 46:9. [Soma.] Ni mabadiliko gani juu ya dunia ambayo unafikiri tendo la Mungu litaleta? [Sikiliza itikio la mwenye nyumba, na kisha umwonyeshe trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani.] Je! waweza kuwazia jambo linalopigwa picha hapa?” Angalia habari iliyoko chini ya kichwa kidogo “Uzima Katika Ulimwengu Mpya wa Mungu.” Hali ikiruhusu, waweza kuendelea kutoa kitabu Kuishi Milele ukikazia fikira habari kama hiyohiyo katika kurasa 11-13. Habari zaidi zaweza kupatikana katika kitabu Kutoa Sababu, kurasa 327-332, chini ya swali “Ufalme wa Mungu utatimiza nini?” Mahali ambapo kitabu kimeangushwa au dalili zozote za kupendezwa zimeonyeshwa hakikisha umefanya mipango ya ziara ya kurudia.
3 Au waweza kusema:
◼ “Hangaiko jingi limeonyeshwa juu ya matatizo yenye kusumbua ambayo sisi sote twalazimika kushughulika nayo kila siku. Je! wahisi kama kuna tumaini lolote kwa matatizo haya? [Ruhusu elezo.] Wengine huenda wakahisi kwamba Mungu hajali hali yetu mbaya. Hata hivyo, angalia, analoahidi kwenye Ufunuo 21:3, 4.” Soma mistari hiyo. Kufikia hapa kitabu Kuishi Milele, gazeti la karibuni, au trakti Je! Ulimwengu Huu Utaokoka? yaweza kutolewa. Katika kutoa kitabu Kuishi Milele habari na vielezi kwenye kurasa 156-158 na 161, 162 yaweza kuangaliwa. Hili litakusaidia usitawishe pamoja na mwenye nyumba jambo ambalo Ufalme wa Mungu utatimiza. Kisha kitabu chaweza kutolewa kwa mchango wa kawaida. Ukitoa ile broshua Je! Kweli Mungu Anatujali?, swali laweza kutokezwa “Kwa Nini Mungu ameruhusu kuteseka?” Onyesha sehemu ya 6 katika broshua hiyo, na upange kuzungumzia hiyo katika ziara itakayofuata.
4 Unaweza kuchagua kuangalia makala kutoka moja la magazeti ya karibuni kwa kutoa elezo juu ya jambo hususa katika makala iliyoteuliwa.
Mwenye nyumba akionyesha kupendezwa, toa gazeti, labda kwa kusema:
◼ “Makala hii inakazia kindani jambo hilo. [Soma sentensi moja au mbili zilizoteuliwa.] Makala hiyo yatoa mawazo ya ziada ambayo yatakuwa yenye kutia moyo kwako na kwa familia yako. Kwa kuwa waonekana kupendezwa na jambo hili, tutafurahi kukuachia toleo hili na gazeti jenzi kwa mchango wa .”
5 Leo watu huwa wametatanika inapofika kujua ni wapi kwa kugeukia ili kupata majibu ya matatizo yanayokabili wanabinadamu. Tuna pendeleo la kushiriki nao tumaini lililo wazi la wakati ujao. (Mdo. 17:27) Basi, na tuelekeze kwa bidii uangalifu wa watu kwenye Ufalme wa Mungu, chanzo cha kweli cha amani.