Kusitawisha Kupendezwa Katika Ziara za Kurudia
1 Huduma imefananishwa kwa kufaa na ukulima, na kufanya ziara za kurudia kumelinganishwa na kupalilia na kutia maji. (Mt. 13:23; Lk. 10:2; 2 Kor. 9:10) Tukiwa “wafanya kazi pamoja na Mungu,” tuna wajibu wa kusaidia mbegu yoyote yenye kuchipuka ikue kufikia ukomavu na kuwa yenye kuzaa matunda. (1 Kor. 3:6, 9) Twaweza kutimizaje vema jambo hili?
2 Uwe mwepesi kufanya ziara za kurudia kwa wote walioonyesha kupendezwa. Pitia maandishi yako ya nyumba kwa nyumba, na uamue ni nani utakayemtembelea na mtaongea juu ya nini. Kwa ujumla mazungumzo yako yataamuliwa na yale yaliyozungumziwa katika ziara ya kwanza. Uwe mwenye kunyumbulika, ukiwa na mawazo mengine ya Kimaandiko akilini yanayoweza kutokezwa. Ni vema sikuzote kutumia Biblia, ukitambua nguvu yayo ya kufikia moyo.—Ebr. 4:12.
3 Ikiwa uliacha broshua “Je! Kweli Mungu Anatujali?,” unaweza kuanza kwa kusema hivi:
◼ “Watu wengi wenye mioyo minyoofu wanaamini kwamba Mungu ataharibu dunia, ilhali wengine wanahofu kwamba mwanadamu atafanya hivyo yeye mwenyewe. Wewe wafikirije? [Ruhusu itikio.] Biblia hutuambia kwamba badala ya kuiharibu dunia, Mungu ataisafisha kutokana na ukosefu wa uadilifu, akiifanya iwe mahali pa amani na usalama.” Elekeza uangalifu kwenye ukurasa wa 22, na usome Mithali 2:21, 22, ambalo limenukuliwa hapo. Kisha unaweza kueleza juu ya mpango wa funzo la Biblia la nyumbani au utoe magazeti ya karibuni, na ufanye mpango wa kurudi ili kuzungumza zaidi juu ya ulimwengu mpya ulioahidiwa wa Mungu.
4 Ikiwa uliangusha broshua “Tazama!,” unaweza kusema:
◼ “Katika ziara yangu iliyopita, tulisoma katika Biblia juu ya ahadi ya Mungu ya kufanya dunia iwe paradiso, kama ilivyoonyeshwa kwenye jalada la broshua niliyokuachia. Twaweza kufurahia baraka kwa kujifunza mengi juu ya mapenzi ya Mungu na jinsi yanavyotuathiri.” Soma Yohana 17:3, kisha fungua mafungu 52 na 53 kwenye ukurasa wa 27. Zungumzia kifupi sababu kwa nini kuna uhitaji wa kutwaa ujuzi sahihi wa Neno la Mungu.
5 Unapofuatia angusho la broshua “Kusudi la Uhai” kwa mtu mwenye mwelekeo wa kidini, huenda ukaona inafaa kusema:
◼ “Yamkini umeirudiarudia Sala ya Bwana mara nyingi. Ni wazo gani huja akilini mwako unapoomba Ufalme wa Mungu uje?” Ukifuatia itikio la mwenye nyumba, rejezea kwenye mafungu 5 na 6 ukurasa wa 25, nawe usome mistari yoyote kutoka kwenye Zaburi. Kazia kwamba kuja kwa Ufalme wa Mungu kutamaanisha mwisho wa uovu na kuteseka. Onyesha kwamba ikiwa sisi ni waadilifu machoni pa Mungu, twaweza kufurahia uhai wa milele katika Paradiso kwenye dunia hii.
6 Kumbuka kwamba ziara ya kurudia yaweza kufanywa kwa yeyote aliyekuwa na nia ya kusikiliza, iwe fasihi iliangushwa au la. Jaribu kutenga wakati fulani kila juma ili kufanya ziara za kurudia. Yehova atabariki jitihada zako zenye bidii za kusitawisha kupendezwa unakopata. Na kutokeze matunda kwa sifa yake.—Yn. 15:8.