Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/94 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Mei 2
  • Juma Linaloanza Mei 9
  • Juma Linaloanzia Mei 16
  • Juma Linaloanza Mei 23
  • Juma Linaloanza Mei 30
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 5/94 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Mei

Juma Linaloanza Mei 2

Wimbo 20

Dak 5: Matangazo ya kwenu na Matangazo yahusuyo kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Pitia mipango yoyote ya kupanua utendaji mbalimbali wa utumishi wa shambani, kama vile kazi ya barabarani au kutoa ushahidi wa alasiri.

Dak 15: “Je! Utashiriki Katika Ushahidi wa Kivivihivi?” Zungumzia na kufanya onyesho la mambo katika makala. Kazia uhakika wa kwamba sisi ni Mashahidi wa Yehova nyakati zote, kwa hiyo twataka kutafuta fursa za kutoa ushahidi. Tayarisha mapema kuwa na maono mafupi mawili ambapo watu mmoja-mmoja walijitia katika kutoa ushahidi wa kivivihivi kwa matokeo mema au ambapo mtu fulani aliingia katika kweli kutokana na ushahidi wa kivivihivi.

Dak 10: “Je! Nahitaji Kubadilibadili?” Mazungumzo kati ya wazee wawili. Kazieni manufaa za kushiriki kwa ukawaida katika utumishi wa shambani.

Dak 15: “Yatumie Magazeti Kuishiriki Kweli.” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Eleza ni nini huyafanya magazeti yetu yawe tofauti na kwa nini hiyo yapaswa kutusukuma tuyatoe kwenye kila fursa. Panga kuwe na maonyesho mafupi mawili.

Wimbo 128 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 9

Wimbo 214

Dak 10: Matangazo ya kwenu. Twapaswa kuwa macho kuona fursa za kupata maandikisho. Twaweza kuyatoa kwa wale walioyakubali magazeti wakati uliopita. Eleza jinsi ya kujaza karatasi za maandikisho zikiwa tatu-tatu.

Dak 20: “Tayarisha Wanafunzi wa Biblia Kwa Ajili ya Huduma.” Maswali na majibu. Kuhusu mafungu 4 na 5, uwe na onyesho fupi likionyesha jinsi ya kusaidia mwanafunzi ajitayarishe kutoa ushahidi mlangoni. Mwanafunzi aanza kwa utoaji sahili akitumia Zaburi 37:11. Mwalimu akatiza, akisema, “Mimi nina dini yangu mwenyewe.” Mwanafunzi hana uhakika aseme nini. Wote wawili wageukia kitabu Kutoa Sababu, kurasa 18-19, wapitia majibu fulani yaliyodokezwa, na kuchagua moja ambalo mwanafunzi ahisi akistareheka nalo. Mwanafunzi arudia utoaji, aitikia vizuri, naye ahisi ametiwa moyo na matokeo.

Dak 15: Utumizi wa Familia wa Kitabu-Mwaka Kipya. Kichwa cha familia aongoza watu wa nyumba yake katika pitio lenye kuchochea juu ya habari za utangulizi katika kurasa 10 za kwanza za Kitabu-Mwaka cha 1994. Amalizia kwa kutoa muhtasari wa mipango kwa familia kusoma kurasa chache za Kitabu-Mwaka kila juma. Ikiwa kutaniko halijapokea Kitabu-Mwaka kipya, basi sehemu hii yaweza kutumiwa kwa mahitaji ya kwenu.

Wimbo 139 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanzia Mei 16

Wimbo 173

Dak 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na shukrani zozote za upaji. Pitia broshua ambazo zingeweza kutolewa, na uelekeze fikira kwenye mambo machache ya kuzungumzia.

Dak 17: “Rudi Ulikopata Kupendezwa.” Maswali na majibu. Uwe na onyesho la njia moja au mbili za utoaji uliodokezwa.

Dak 18: “Kunufaika Kikamili na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakifanywa na mwangalizi wa shule. Watie wote moyo kukubali na kutimiza migawo. Kazia umaana wa kufuatana na usomaji wa Biblia wa kila juma. Eleza jinsi kutaniko zima liwezavyo kunufaika na shauri wapewalo wanafunzi.

Wimbo 53 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 23

Wimbo 192

Dak 15: Matangazo ya kwenu.

Dak 15: “Je! Wewe Huwaheshimu Wengine Utoapo Shauri?” Hotuba ikitolewa na mzee, ikiwa na msingi wa Mnara wa Mlinzi la Februari 1, 1994, kurasa 25-9. Onyesha jinsi kanuni zitumikavyo kwa vichwa vya familia wanapotoa shauri ndani ya familia.

Dak 15: Nufaika Kutokana na Kitabu-Mwaka cha 1994. Akitoa habari katika Kitabu-Mwaka cha 1994, kurasa 10-18, mzee na mtumishi wa huduma wazungumza mambo ya kutia moyo yawezayo kutumiwa kujenga uthamini kwa tengenezo la kitheokrasi. Kwa sababu ya matatizo ya karibuni kuhusu ukavu na mpanuko unaotukia kuhusu miradi ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme vuta fikira kwenye moja la mambo hayo yanayogusa maisha za akina ndugu katika eneo lenu. Ikiwa kutaniko halijapokea Kitabu-Mwaka kipya, basi sehemu hii yaweza kupitia mambo makuu ya kusanyiko la mzunguko la hivi majuzi au programu ya siku ya kusanyiko la pekee.

Wimbo 19 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 30

Wimbo 204

Dak 12: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Pitia makala za kutokeza katika magazeti ya karibuni, upange kuwe na onyesho moja au mawili ya utoaji mfupi.

Dak 15: Pitia toleo la fasihi kwa Juni: Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? au Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya. Elekeza fikira kwenye vielezi vya kuvutia kama vile vilivyo katika kurasa 4, 5, 33, 41, 95, 135, 172. Panga mhubiri hodari aonyeshe utoaji mfupi ulio na msingi wa kimoja cha vielezi hivyo kwa kutumia Ufunuo 21:4. Toa muhtasari wa mipango ya utumishi wa shambani kwa juma linalokuja.

Dak 18: Je! Utafanya Upainia-Msaidizi Miezi Inayokuja? Hoji watu fulani ambao wamefanya upainia-msaidizi katika kipindi hicho miaka iliyopita. Watie moyo vijana na wengine ambao hali zao zaruhusu kufikiria kutumia vipindi vya likizo kwa faida bora zaidi. Huenda wengine wao wakaweza kusaidia kumaliza eneo lenye kufanyiwa kazi mara chache au lililo peke yalo.

Wimbo 12 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki