Je! Nahitaji Kubadilibadili?
Kila toleo la Huduma ya Ufalme Yetu huandaa unamnanamna wa utoaji wa Kimaandiko tuwezao kutumia tunapotoa ushahidi. Wahubiri wengi walio watendaji sana wana hamu nyingi ya kupata mawazo mapya na kutumia mifikio tofauti. Huduma ya Ufalme Yetu hujazia mahitaji yao kwa kutoa madokezo kadhaa kila mwezi.
Hata hivyo, huenda ikawa wewe huoni uhitaji wa kubadilibadili utoaji uutumiao. Huenda ikawa wewe hupata muda wa saa chache tu kila mwezi za kushiriki katika kazi ya nyumba kwa nyumba. Kwa muda fulani, huenda ikawa umekuza utoaji fulani ambao wajihisi ukistareheka nao, nawe hupata matokeo mazuri kwa kuutumia. Huenda ikawa wewe hutegemea maandiko fulani yatumiwayo mara nyingi, kutia na Zaburi 37:9-11, 2 Petro 3:13, Ufunuo 21:4, na mengine. Ikiwa ndivyo, huhitaji kuhisi ukiwajibika kuyabadilibadili mara nyingi ili ufanye jambo jinginelo. Mradi wetu wa msingi ni kushiriki tumaini la Ufalme pamoja na wengine na kuwasaidia wajifunze mambo ambayo ni lazima wayafanye ili kustahili baraka ya Yehova. Ukipata utoaji mbalimbali wenye kufaa wakati na wenye kuvutia katika kitabu Kutoa Sababu ambao wapendelea kuutumia na unapata itikio zuri kwa kuutumia, usisite kuutumia.