Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/94 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Juni 6
  • Juma Linaloanza Juni 13
  • Juma Linaloanza Juni 20
  • Juma Linaloanza Juni 27
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 6/94 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni

Juma Linaloanza Juni 6

Wimbo 9

Dak 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo kutoka Huduma ya Ufalme Yetu yanayohusu habari za kwenu. Kumbusha wasikilizaji wachukue nakala za kitabu Creation ili kutumia katika utumishi mwisho-juma huu.

Dak 20: “Je! Wewe Unapanda kwa Wingi?” Maswali na majibu. Wakati ukiruhusu, alika wasikilizaji waeleze maono yao binafsi kuonyesha jinsi wamejitahidi zaidi katika sehemu fulani ya utumishi wao na kubarikiwa kwa jambo hilo.

Dak 15: “Kusaidia Wengine Wamheshimu Mfanyi Wetu.” Zungumza na wasikilizaji. Panga uwe na maonyesho mawili yakionyesha jinsi utoaji uliodokezwa waweza kutumiwa.

Wimbo 30 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 13

Wimbo 28

Dak 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na shukrani za upaji wa hiari za Sosaiti. Tia ndani maelezo mafupi ya kuonyesha jinsi mtu mwenye roho ya ukarimu anavyobarikiwa.—Mit. 11:24a.

Dak 15: “Kujenga Imani Katika Muumba wa Wanadamu.” Zungumza na wasikilizaji. Wakati ukiruhusu, toa mojapo monyesho ya ziara za kurudia zilizopendekezwa.

Dak 20: “Funzo la Kitabu la Kutaniko Huchochea Utendaji Wenye Kuelimisha.” Kiongozi wa funzo azungumza na wasikilizaji. Kazia jinsi makala hiyo inavyotia moyo (1) hudhurio lililoongezeka la funzo la kitabu, (2) wengi wanaotoa maelezo wakati wa funzo, na (3) uungaji-mkono mzuri wa mikutano ya utumishi wa shambani.

Wimbo 65 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 20

Wimbo 31

Dak 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.

Dak 10: Mahitaji ya kwenu. Au utoe hotuba juu ya makala “Napaswa Kuchagua Kazi Gani ya Maisha?” kutoka Amkeni!, Februari 8, 1990. kurasa 12-14.

Dak 10: Sanduku la Swali. Mazungumzo ya maswali na majibu.

Dak 15: “Je! Wewe Unafanya Mapenzi ya Mungu?” Hotuba ikitolewa na mzee ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Machi 1, 1994, kurasa 28-30.

Wimbo 223 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 27

Wimbo 174

Dak 10: Matangazo ya kwenu. Onyesha kifupi jinsi magazeti ya karibuni yawezavyo kutolewa nyumba kwa nyumba mwisho-juma huu.

Dak 15: “Mikutano ya Maana ya Utumishi wa Shambani.” Ikizungumziwa kwa maswali na majibu na mwangalizi wa utumishi. Unapozungumzia fungu la 3, onyesha utangulizi mmoja au mawili kutoka kitabu Kutoa Sababu ambayo yanaweza kutumiwa mwisho-juma huu. Katika fungu la 5 taja matatizo yoyote kuhusu kuongoza utumishi wa shambani ambayo yameonekana kwenu; toa mapendekezo ya fadhili ya kufanyiwa maendeleo.

Dak 20: Pitia Toleo la Julai. Onyesha nakala za vijitabu vilivyoko katika akiba ya kutaniko, kama vile Wakati Ujao Salama—Jinsi Unavyoweza Kuuona, God’s Way Is Love, Je! Mungu Anajali?, There Is Much More To Life!, au “Habari Njema Hizi za Ufalme.” Vijitabu hivi vina msaada wa kuanzisha mafunzo ya Biblia. Pitia mambo fulani yenye kupendeza na vielelezo ambavyo vyaweza kutumiwa kuanzisha mazungumzo. Panga kuwe na maonyesho mawili ya jinsi ya kuanzisha mazungumzo ya somo fulani la Biblia. (Tumia madokezo yaliyo kwenye kitabu Kutoa Sababu juu ya “Wakati Ujao/Usalama,” kurasa 14, na dokezo la pili chini ya “Ufalme,” kwenye ukurasa 12.) Maonyesho yapaswa kumalizia na mipango ya kuanzisha funzo la Biblia.

Wimbo 118 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki