Sitawisha Kupendezwa Katika Kitabu Kuishi Milele
1 Tunapozuru nyumbani mwao, sisi kwa kawaida hupata kwamba watu wamejiingiza kabisa katika “shughuli za dunia.” (Mk. 4:19) Tunakabiliwa na ugumu wa kunasa upendezi wao tukiwa na utoaji wenye kuvuta fikira. Mwanzoni, watu wengi huenda wakawa na upendezi mdogo kwa yale tutakayosema. Ikiwa twaweza kusema jambo linaloweza kuathiri maisha zao, huenda tukaweza kuchochea upendezi fulani katika ujumbe wa Ufalme. Ufunguo wa kuanzisha mazungumzo ni kuteuwa mambo yenye kuvutia ya kuongea kutoka kwenye kitabu Kuishi Milele. Ungesema nini?
2 Unaweza kutumia mfikio huu:
◼ “Kama ungekuwa na uwezo, ni tatizo jipi lenye kutaabisha katika siku yetu ambalo ungelirekebisha? [Ruhusu itikio, na ikiwa inafaa, kubali kwamba watu wengi huhisi vivyo hivyo.] Kufikia hapa, binadamu waonekana kuwa na mafanikio haba katika kupata utatuzi wa matatizo mengi yanayotatanisha ya leo. Lakini kuna Mmoja anayeweza naye atamaliza matatizo yote yanayodhulumu wanadamu. Tafadhali ona yale yanayotajwa kwenye Zaburi 145:16. [Soma andiko hilo, na urejezee vielezi vilivyo kwenye kurasa 11-13.] Fungu la 14 kwenye ukurasa 14 latokeza swali ambalo tumelizungumzia tu nalo laendelea kuuliza: ‘Lakini hayo yatatendeka wakati gani?’” Eleza kwamba kitabu hiki kitajibu swali hilo, na kisha mtolee kitabu.
3 Au ungeweza kusema jambo kama hili:
◼ “Labda unajua hisia ya utupu inayotokana na kumpoteza mpendwa katika kifo. Yamkini ilikufanya uhisi huzuni na hoi sana. Huenda ikawa uliyafikiria maswali haya: [Soma maswali katika fungu la 1 kwenye ukurasa 76.] Je, haingefariji kupata majibu ya maswali haya? Unaweza kutiwa moyo kujua kwamba Biblia hutoa tumaini hakika kwa wale ambao wamekufa. [Soma Yohana 5:28, 29.] Kitabu hiki chatusaidia tuelewe hali ya wafu na tumaini lililopo kwa wakati ujao.” Rejezea kifupi sura ya 8 na 20 na umpe mwenye nyumba fursa ya kukichunguza kitabu.
4 Kuna uwezekano mkubwa kwamba utapata fursa za kutoa ushahidi kivivi-hivi. Ikiwa ni hivyo, unaweza kusema jambo kama hili, kwa maneno yako mwenyewe:
◼ “Ulimwengu umejaa matatizo siku hizi, na yaonekana sote tunayashirki. Inahuzunisha kwamba, yaonekana kuwa watu wasio na hatia ndio huteseka zaidi. Wafikiri Mungu atakomesha kuteseka kwote? [Ruhusu itikio.] Acha nikuonyeshe yale ambayo Mungu anaahidi kuwafanyia wale wanaomtumikia. [Soma Zaburi 37:40 kisha ufungue kitabu Kuishi Milele ukurasa 99.] Kitabu hiki chaeleza sababu Mungu ameruhusu uovu na jinsi atakavyoukomesha.”
5 Ikiwa wewe ni mhubiri mchanga, unaweza kutumia utoaji unaotegemea vielezi vinavyopatikana kwenye kurasa 156-8. Unaweza kuanza kwa kuuliza:
◼ “Je, ungependa kuishi katika ulimwengu kama huu? [Ruhusu itikio.] Kila moja ya picha hizi maridadi zategemea ahadi iliyotajwa katika Neno la Mungu, Biblia. [Elekeza kwenye marejezo ya Maandiko.] Kitabu hiki chaweza kukusaidia ujifunze mengi kuhusu ahadi ya Mungu ya kuifanya dunia yote kuwa paradiso. Kina habari yenye kuokoa uhai nacho chastahili wakati unaotumiwa kukisoma.”—Yn. 17:3.
6 Unapofanya utoaji wako, angalia kupendezwa kokote nawe uwe uhakikishe kutoa funzo la Biblia.