Tumia Vema Magazeti Yetu
1 Ni gazeti jipi leo ulimwenguni ambalo “hufariji jamii zote za watu kwa habari njema za kwamba karibuni Ufalme wa Mungu utaharibu wale wanaoonea wanadamu wenzao na kwamba utaigeuza dunia iwe paradiso”? Je, kuna gazeti ambalo “hujenga uhakika katika ahadi ya Muumba ya kuleta ulimwengu mpya wenye amani na usalama”? Bila shaka unatambua maelezo haya ya kusudi la magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Naam, magazeti yetu huonyesha kwamba Yehova ameazimia kwamba kutakuwa na ‘amani, wakati ujao, na tumaini’ kwa wale wanaofuata njia Zake.—Yer. 29:11.
2 Twaonyesha uthamini wetu kwa magazeti haya yenye thamani kwa njia nyingi. Tukitambua uandalizi huu wa “mtumwa mwaminifu mwenye akili” kwa ajili ya hali yetu ya kiroho twafanya kila jitihada kusoma kila toleo kutoka jalada hadi jalada. (Mt. 24:45) Wazazi wahakikishe watoto wao wana nakala za kutumia kibinafsi na kwenye kutaniko. Kujitayarisha na kushiriki katika funzo la kila juma la Mnara wa Mlinzi pia huonyesha wazi mwelekeo wa moyo wenye shukrani. Na, bila shaka, kutumia magazeti haya yenye thamani katika huduma ya shambani kwaonyesha heshima kwa vifaa hivi vinavyoelekeza kwenye njia ya uhai. Je, wewe na familia yako huweka wakati kando kwa ukawaida kwa ajili ya kugawanya magazeti?
3 Matayarisho ya Lazima: Ni muhimu kuratibu wakati hususa na wa kawaida kwa ajili ya kutoa ushahidi kwa magazeti. Huenda ikawa ni kutoa ushahidi nyumba kwa nyumba, kutoa ushahidi wa barabarani na katika eneo la kibiashara mahali panapofaa, kutoa ushahidi wa njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida au namna yoyote iliyotangulia kutajwa. Katika majiji na miji mikubwa, Jumamosi imethibitika kuwa siku ya magazeti yenye matokeo. Katika sehemu za mashambani akina ndugu hutumia vizuri siku ya soko. Kulingana na hali za kwenu kila kutaniko laweza kupanga kutoa ushahidi kwa magazeti kwenye pindi ifaayo. Hata hali iweje jambo la maana ni kuweka kando wakati kila juma wa kutoa ushahidi wa magazeti.
4 Baada ya kuratibu wakati wako sasa uko tayari kutayarisha utoaji mfupi wa magazeti usiopita dakika moja au mbili. Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 1994, lilitukumbusha kwamba “utoaji mfupi unaolenga jambo kuu, wafaa zaidi wakati wa kutoa magazeti.” Magazeti ‘yatajisemea’ yenyewe. Kwa hiyo, chagua wazo moja kutoka kwenye makala, liseme kwa maneno machache yenye kulenga na utoe magazeti. Fanya lengo liwe kusema machache, lakini uyaseme vizuri. Jizoeze mapema. Uwe mwenye idili na umvutie mtu huyo.
5 Yaliyo juu ni madokezo machache tu ya kutusaidia tutumie vema magazeti yetu. Twajua jinsi Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yalivyo yenye thamani. Twajua jinsi yalivyo na msaada unaotumika na mwongozo ulio ndani yayo wa kutuwezesha kukabiliana na mfumo wa sasa wa mambo. Na twajua kwamba haya ndio majarida pekee yanayoelekeza kwenye wakati ujao mtukufu ulioko mbele kwa wanadamu watiifu. (Ufu. 21:3, 4) Kwa hiyo, tutaendelea kufanya kila jitihada iwezekanayo kushiriki magazeti haya ya maana pamoja na wenye mfano wa kondoo katika eneo letu.