Matangazo
◼ Fasihi itakayotumiwa wakati wa Oktoba: Kutoa maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Novemba: New World Translation of the Holy Scriptures pamoja na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapwa kabla ya 1982 ambacho huenda kutaniko likawa na akiba yacho. Makutaniko ambayo hayana vitabu vya zamani akibani yatatoa Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje? TAARIFA: Makutaniko ambayo hayajaagiza vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa yaviagize kwenye Agizo la Fasihi (S-14-SW) lao la kila mwezi litakalofuata.
◼ Moja ya nyongeza katika toleo hili la Huduma ya Ufalme Yetu ni “Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1995.” Yapaswa kuwekwa kwa ajili ya marejezo ya mwaka wote wa 1995.
◼ Makutaniko yapaswa yaanze kuagiza Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—1995 pamoja na agizo lao la fasihi la Oktoba. Vijitabu hivyo vitapatikana kwa Kiarabu, Kifaransa, Kiingereza, Kinyarwanda, na Kiswahili. Vijitabu Kuyachunguza Maandiko ni vifaa vya kuagizwa kipekee.