Habari Za Kitheokrasi
Kuanzia Septemba 1, 1994 ofisi ya tawi mpya katika Ethiopia ilianza kutenda. Kufikia wakati wa uandikaji huu, ofisi hiyo itakuwa inasimamia kazi katika Ethiopia, na nchi zilizo karibu.
Haiti: Mei ulikuwa mwezi wenye kutokeza sana ukiwa na kilele kipya cha wahubiri 9,188, ongezeko la asilimia 13 kuliko wastani wa mwaka uliopita.
Italia: Kulikuwa na kilele kipya cha wahubiri 205,128 katika Mei. Hiki kilikuwa 1,499 zaidi ya kilele kilichopita cha wahubiri mwezi mmoja tu uliopita.
Tanzania: Jumba la Ufalme katika Kiwira liliwekwa wakfu mnamo Juni 20 kukiwa na hudhurio la 239. Jumba hilo lililojengwa kwa saruji lilichukua siku tano na nusu.