Kutumia Vizuri Vitabu Vyetu vya Zamani
1 Yehova ametuandalia wingi wa chakula cha kiroho. Kingi chacho kimekuwa kwa namna ya vitabu vyenye kurasa 192 ambavyo vimechapishwa miaka ya majuzi. Wakati wa Januari tutakuwa tukitoa kitabu chochote chenye kurasa 192 ambacho kilichapishwa kabla ya 1982. Je, una baadhi ya hivi nyumbani ambavyo bado viko katika hali nzuri? Je, kutaniko linavyo akibani? Ikiwa ndivyo, ingekuwa vizuri kupitia mambo yaliyomo na kuchagua baadhi ya mambo ya kuzungumzia unayoweza kutumia katika utoaji wako.
2 Ikiwa unatumia kitabu “Ufalme Wako Uje,” unaweza kuanza kwa kusema:
◼ “Wakristo wamesali kwa ajili ya kuja kwa Ufalme wa Mungu kwa karibu miaka 2,000. Unafikiri Ufalme utafanyia wanadamu nini? [Ruhusu itikio. Fungua sanduku kwenye ukurasa 25, na uonyeshe baadhi ya baraka zitakazopatikana chini ya utawala wa Ufalme.] Kitabu hiki huzungumzia mambo ambayo Ufalme utatimiza na hueleza jinsi wewe na wapendwa wako mnavyoweza kunufaika. Ikiwa ungependa kukisoma, nitafurahi kukuachia nakala moja.”
3 Ikiwa unatoa kitabu “Furaha—Namna ya Kuipata,” unaweza kujaribu mfikio huu:
◼ “Watu walio wengi wana ugumu wa kupata furaha katika ulimwengu huu kwa sababu kuna matatizo mengi sana. Unafikiri inawezekana kuwa na furaha chini ya hali za sasa? [Ruhusu itikio. Fungua ukurasa 41, na uonyeshe matatizo fulani ya kawaida ambayo hutupa sababu ya hangaiko.] Biblia huonyesha jinsi tunavyoweza kukabiliana na matatizo haya na hatimaye kufurahia furaha isiyokoma katika ulimwengu mpya wenye amani. [Fungua ukurasa 190, na usome Isaya 32:17, 18.] Biblia hutupa shauri hususa ambalo laweza kutusaidia kupata furaha nyingi zaidi katika kuishi. Kitabu hiki hupitia shauri hilo nacho hueleza jinsi tunavyoweza kulitumia.”
4 Ikiwa unatumia kitabu “Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?,” unaweza kutaka kujaribu huu:
◼ “Kila mtu angependa kuishi katika ulimwengu ambamo kuna amani na usalama. Inasikitisha kwamba, hatujaona hilo katika maisha yetu. Unafikiri twahitaji kufanya nini ili tufanyize amani na usalama viwe uhalisi? [Ruhusu itikio.] Mungu ana uwezo wa kuleta amani kwenye dunia hii, naye ameahidi kwamba atafanya hivyo.” Fungua kwenye picha katika ukurasa wa 98, kisha usome Mika 4:3, 4. Kukiwa na itikio zuri, eleza zaidi juu ya tumaini la Ufalme, toa kitabu, na ufanye mipango kwa ajili ya ziara ya kurudia.
5 Unaweza kuchagua kutumia broshua “Je! Kweli Mungu Anatujali?” Ikiwa ndivyo, unaweza kusema hivi:
◼ “Watu wengi hushangaa kwa nini Mungu huruhusu kuteseka kwingi ulimwenguni. Kwa kuwa yeye ni mweza-yote, kwa nini hafanyi kitu fulani ili akomeshe kutaabika kwetu? Wewe wahisije? [Ruhusu itikio.] Biblia hutuhakikishia kwamba Mungu hajatuacha.” Fungua ukurasa 27, fungu 22, na usome Zaburi 37:11, 29. Onyesha kielezi chenye kuvutia kinachoonyesha yale tuwezayo kutazamia. Broshua ikikubaliwa, jitoe kurudi ili uonyeshe jinsi inavyoweza kutumiwa kwa funzo la Biblia.
6 Fasihi zetu zimehamasisha maelfu ya watu wachunguze Biblia kwa ukaribu zaidi. Waliyojifunza yamewaletea tumaini la wakati ujao wenye furaha. (Zab. 146:5) Ni pendeleo letu kuwasaidia.