Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/95 uku. 4
  • Onyesha Unajali kwa Kufanya Ziara za Kurudia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Onyesha Unajali kwa Kufanya Ziara za Kurudia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Tangaza Habari Njema za Ufalme Ukitumia Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Mwige Yehova kwa Kujali Wengine Kikweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Fanya Ziara za Kurudia kwa Maangusho Yote ya Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Kutumia Vizuri Vitabu Vyetu vya Zamani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 1/95 uku. 4

Onyesha Unajali kwa Kufanya Ziara za Kurudia

1 Kutafuta watu wenye kupendezwa mlango kwa mlango huonyesha tamaa yako ya kuwapa wengine fursa ya kusikia ujumbe wa Ufalme. Hivyo uhakikishe kufuatia maangusho ya fasihi unazofanya wakati wa mwezi wa Januari, kwa kuwa hii ndiyo njia nzuri ya kuonyesha unajali wengine.

2 Ikiwa uliacha kitabu “Ufalme Wako Uje,” unaweza kujaribu kuanzisha tena mazungumzo yako kwa njia hii:

◼ “Wakati uliopita tuliongea juu ya Ufalme wa Mungu na kile utakachotufanyia. Ufalme huo utafanya dunia hii kuwa paradiso karibuni. Kwa kuwa hatujapata kamwe kuona paradiso, huenda ikawa vigumu kuiwazia. Hivi ndivyo vile huenda ikaonekana. [Rejezea kielezi kilicho kwenye kurasa 4 na 5.] Paradiso kama hiyo imeahidiwa katika Biblia.” Soma Zaburi 72:7. Ikiwa kuna upendezi, fungua ukurasa wa 175, mafungu 3 na 4, na uonyeshe yale ambayo ni lazima tufanye ikiwa twataka kuishi katika Paradiso ijayo.

3 Hapa kuna dokezo la kufuatia maangusho yako ya kitabu “Furaha—Namna ya Kuipata”:

◼ “Sisi sote tungependa kuwa wenye furaha. Wengi huhisi kwamba furaha ya kweli haiwezekani katika ulimwengu huu. Wewe wahisije kuhusu hilo? [Ruhusu itikio.] Imesemwa kwamba furaha ni hali ya akili. Akili zetu zikijawa na upendo kwa wengine, heshima kwa Mungu, na tumaini hakika la wakati ujao, twaweza kupata furaha ya kweli yajapokuwa matatizo yetu.” Soma Zaburi 119:1, 2. Eleza kwamba funzo la Biblia hutufunza jinsi ya kupenda wengine, kuonyesha heshima kwa Mungu, na kupata tumaini lenye faraja la wakati ujao.

4 Unaweza kufuatia angusho la kitabu “Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?” na utoaji mfupi wa jambo kama hili:

◼ “Viongozi wa ulimwengu leo wameshindwa kuleta amani na usalama. Yehova Mungu ndiye pekee awezaye kufanya hivyo. Biblia hutuonyesha tunalohitaji kufanya. [Zungumzia mambo yaliyo kwenye mafungu 1 na 2 katika ukurasa 175, kisha usome Isaya 26:4.] Ningependa kukuonyesha jinsi kitabu hiki kinavyoweza kukusaidia.”

5 Unaweza kufuatia angusho la broshua “Je! Kweli Mungu Anatujali?” kwa dokezo hili:

◼ “Wakati uliopita nilikuachia nakala ya broshua hii, inayotokeza swali muhimu: ‘Je! kweli Mungu anatujali?’ Baada ya kupitia broshua hii, ulifikia mkataa gani? [Ruhusu itikio.] Yamkini ulitiwa moyo kwa kusoma maandiko ambayo yaahidi juu ya ulimwengu mpya wa paradiso, ambamo twaweza kuishi kwa amani. [Onyesha vielezi kwenye kurasa 2 na 3, na uonyeshe baadhi ya mambo yenye kuvutia ya ulimwengu mpya.] Nahisi kwamba wewe na wapendwa wako mtapenda kuishi katika ulimwengu kama huo. Angalia yale fungu la 16 kwenye ukurasa 31 linasema kuhusu hili.” Soma fungu hilo, na uonyeshe kwamba kumtafuta Yehova kwamaanisha kujifunza zaidi kumhusu yeye na makusudi yake kwa kujifunza Neno lake, Biblia.

6 Yehova ameweka kielelezo kikamilifu akiwa Mchungaji mwenye upendo anayejali kondoo zake. (Eze. 34:11-14) Jitihada yetu ya unyoofu ya kuiga kujali kwake kwenye upendo humpendeza, huonyesha upendo wetu, na huleta baraka kwa wengine.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki