Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/95 uku. 8
  • Wasaidie Wengine Wajinufaishe Wenyewe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wasaidie Wengine Wajinufaishe Wenyewe
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Fuatia Kupendezwa Kote ili Kunufaisha Wengine
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Unazoweza Kutumia Katika Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Fuatia Kupendezwa Ulikopata
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Hubiri kwa Ufahamu Wenye Kina
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 9/95 uku. 8

Wasaidie Wengine Wajinufaishe Wenyewe

1 Yehova aahidi kutufundisha kile tunachohitaji kujua. Yeye atuhakikishia hivi kwenye Zaburi 32:8: “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; nitakushauri, jicho langu likikutazama.” Uhakikishio huu ni wenye manufaa sana kwetu. Bila ubinafsi, twataka kuonyesha wengine jinsi wanavyoweza kujinufaisha wenyewe kwa kutii shauri lenye hekima kutoka katika Biblia. (Isa. 48:17) Wakati wa Septemba twaweza kufanya hivyo kwa kutoa kitabu Kuishi Milele. Katika kufanya utoaji wetu, kuna njia mbalimbali ambazo twaweza kuonyesha thamani yenye kutumika ya Biblia.

2 Kwa sababu ya mweneo wa matatizo ya ndoa leo, huenda ukachagua kukazia wazo hili kutoka katika kitabu “Kuishi Milele”:

◼ “Watu walio wengi ambao nimesema nao wanahangaikia sana ongezeko kubwa mno katika ukosefu wa furaha katika ndoa na talaka. Wewe wahisije juu ya tatizo hili? [Ruhusu itikio.] Wengi wameshindwa kutambua mambo ya msingi yanayosababisha mambo hayo. Wakijitahidi kwa moyo mweupe, mume na mke waweza kuokoa ndoa yao na pia waweza kupata furaha ya kweli. Ufunguo wa kupata mafanikio wategemea kutumia shauri linalopatikana katika Biblia.” Soma Waefeso 5:28, 29, 33. Fungua kwenye ukurasa 243, zungumza juu ya fungu 16 na 17, kisha utoe kitabu.

3 Watoto huhitaji wakati unaotumiwa vizuri na mazoezi kutoka kwa wazazi wao. Katika kukazia kitabu “Kuishi Milele,” ungeweza kusema hivi:

◼ “Sisi sote twahangaikia hali njema ya wakati ujao ya vijana wetu. Kulingana na maoni yako, ni nini iliyo njia bora zaidi ambayo wazazi wanaweza kusaidia watoto wao wapate wakati ujao ulio salama? [Ruhusu itikio.] Sikiliza shauri hili kutoka katika mithali ya Biblia iliyoandikwa miaka 3,000 hivi iliyopita. [Soma Mithali 22:6.] Ingawa watoto wetu waweza kunufaika sana kutokana na maagizo wanayopokea shuleni, mazoezi yao yenye thamani zaidi yanaandaliwa nyumbani na wazazi wao. Hilo lataka wakati, uangalifu, na upendo, lakini jitihada hiyo yastahili sana.” Fungua kwenye ukurasa 245, zungumza juu ya fungu 20 na 21, kisha eleza jinsi hiki kitabu chaweza kutumiwa kikiwa msingi wa funzo la familia la Biblia.

4 Huenda ukataka kutoa kitabu “Kuishi Milele” kwa kuonyesha jinsi dunia itakavyokuwa paradiso:

◼ “Nina uhakika unahangaikia jinsi maisha yako yatakavyokuwa katika wakati ujao. Katika Sala ya Bwana, Yesu alitufundisha tusali kwamba mapenzi ya Mungu yafanywe duniani kama yalivyo mbinguni. Dunia itakuwaje wakati hilo litendekapo? [Ruhusu itikio.] Hapa pana picha inayoonyesha maoni ya msanii juu ya ulimwengu ulio paradiso. [Onyesha kielezi kwenye ukurasa 12 na 13. Kisha usome Isaya 11:6-9, lililotiwa ndani katika fungu 12.] Je, lisingekuwa jambo zuri ajabu kuishi katika ulimwengu wa jinsi hii? Kitabu hiki kitakuonyesha jinsi wewe na familia yako mwezavyo kuishi katika paradiso kama hii.”

5 Kutayarisha utoaji wako kimbele ndilo jambo la msingi litakaloamua mafanikio yako mlangoni. Kabla ya kubisha mlango, hakikisha una jambo hususa la kusema juu ya wazo la Kimaandiko. Pia, fikiria elezo fupi juu ya jambo lenye kupendeza katika gazeti au trakti unayopanga kutoa ikiwa kitabu hakikubaliwi. Tumia kwa faida yako kila fursa uliyo nayo ya kupanda mbegu za Ufalme wakati wa Septemba. (Mhu. 11:6) Utakuwa ukiwasaidia wengine wavune manufaa zitakazodumu milele.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki