Fuatia Kupendezwa Kote ili Kunufaisha Wengine
1 Ni nini jambo la msingi linalotusaidia kuamua kama twapaswa au hatupaswi kumwachia mtu fasihi zetu? Kupendezwa! Ndivyo ilivyo kwa habari ya kufanya ziara za kurudia. Wakati wowote mtu aonyeshapo kupendezwa hata kidogo na ujumbe wa Ufalme, twataka kufanya lolote tuwezalo ili kumnufaisha mtu huyo. Kwa hiyo twafanya ziara za kurudia tukiwa na lengo la kusitawisha kupendezwa kwa mtu huyo na kuanzisha funzo la Biblia nyumbani. Huo ni mradi wetu hata wakati tusipoacha fasihi. Hilo laweza kufanywaje?
2 Ikiwa mazungumzo yenu ya wakati uliopita yalikuwa kuhusu mweneo wa matatizo ya ndoa leo na uliacha kitabu “Kuishi Milele,” ungeweza kuanza mazungumzo yenu kwa njia hii:
◼ “Katika ziara yangu iliyopita, tuliongea juu ya ndoa na shauri la Biblia lenye kutumika ambalo laweza kutusaidia tupate furaha kubwa zaidi. Je, si kweli kwamba hata katika familia zilizo bora zaidi, matatizo hutokea mara kwa mara? [Ruhusu itikio.] Biblia hutupa sisi shauri bora kabisa liwezalo kutusaidia kusuluhisha matatizo katika mahusiano ya familia. Familia yaweza kubarikiwa kwa kujifunza Biblia pamoja.” Fungua kwenye ukurasa 246, na uzungumze juu ya fungu 23. Soma Yohana 17:3, na ujitolee kusaidia familia hiyo kuanza kujifunza Biblia nyumbani.
3 Ikiwa ulisema juu ya watoto na uhitaji wao wa kuzoezwa, waweza kuendeleza mazungumzo hayo kwa njia hii:
◼ “Wakati uliopita tulisema juu ya mazoezi ya kiroho ambayo watoto huhitaji na jinsi wazazi wawezavyo kuwasaidia. Wazazi walio wengi ambao nimesema nao wana wasiwasi juu ya mwenendo mbaya wa vijana wengi sana leo. Wewe waonaje juu ya . . . ? [Taja kielelezo cha mwenendo mbaya wa vijana unaoonwa mara nyingi katika jumuiya yenu. Ruhusu itikio.] Acha nikuonyeshe baadhi ya shauri lenye kutumika linalotolewa katika Biblia.” Fungua kwenye fungu 22 kwenye ukurasa 246 katika kitabu Kuishi Milele, zungumza juu ya jambo kuu, na usome Waefeso 6:4. Onyesha kwamba kwa kweli watoto walio wengi wanataka nidhamu na mwongozo. Wazazi wanapokuwa wenye bidii-nyendelevu katika kuandaa mambo hayo, watoto wanakuwa wenye furaha zaidi na wenye staha zaidi katika mwenendo wao. Eleza jinsi tunavyojifunza Biblia pamoja na watoto wetu.
4 Ikiwa habari ya mazungumzo yenu ilikuwa dunia iliyo Paradiso, basi waweza kusema hili ili kuamsha tena kupendezwa:
◼ “Tuliangalia baadhi ya vielezi katika kitabu hiki vilivyoonyesha vile dunia itakavyokuwa wakati Mungu anapoifanya iwe paradiso. Lisingekuwa jambo la maana kwetu ikiwa tusingeweza kuifurahia pamoja na wapendwa wetu. Sivyo?” Ruhusu itikio. Kisha ufungue ukurasa 162 katika kitabu Kuishi Milele. Soma Ufunuo 21:3, 4, na ueleze jinsi wapendwa wetu wawezavyo kuwa nasi sikuzote. Kisha ungeweza kusoma Yohana 5:28, 29 ili kuonyesha kwamba wafu watarudi kwenye uhai. Onyesha jalada la kitabu na useme: “Hakika ni kweli—sisi twaweza kuishi milele katika Paradiso duniani!” Pangia ziara nyingine ili kuzungumza juu ya kwa nini twajua hiyo iko karibu.
5 Kusudi kubwa la ziara ya kurudia ni kusaidia wenye kupendezwa wanufaike kutokana na ujumbe wa Ufalme. Watu walio wengi wanahitaji kichocheo ili kuamsha tamaa yao ya kupata vitu vya kiroho. Elekeza uangalifu wao kwenye mambo hususa yaliyo na thamani yenye kutumika katika fasihi, ukikazia jinsi iwezavyo kuwasaidia kuielewa Biblia vizuri zaidi. Ziara za kurudia zinazotimiza miradi hiyo zitasaidia wengine wajinufaishe kwa njia bora zaidi iwezekanayo.