Mikutano Ya Utumishi Kwa Septemba
Juma Linaloanza Septemba 4
Dak 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi.
Dak 15: “Msifuni Yehova kwa Shangwe Siku kwa Siku!” Maswali na majibu.
Dak 20: “Wasaidie Wengine Wajinufaishe Wenyewe.” Pitia utoaji mbalimbali uliodokezwa, kisha uwe na maonyesho mafupi mawili.
Wimbo 204 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 11
Dak 5: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak 22: “Kudumisha Maoni Yenye Usawaziko Kuhusu Tekinolojia ya Kompyuta.” Nyongeza. Maswali na majibu. Soma mafungu makuu, kama vile 4-8 na 12-13, kadiri wakati uruhusuvyo.
Dak 18: “Umewawekea Watoto Wako Miradi Gani?” Maswali na majibu. Uwe na kijana mmoja au wawili wenye kielelezo chema au watu wenye umri mkubwa zaidi ambao wamemtumikia Yehova kutoka ujana wao wasimulie kwa ufupi jinsi wazazi wao walivyowasaidia wachague miradi inayofaa inayokazia masilahi ya Ufalme.
Wimbo 187 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 18
Dak 10: Matangazo ya kwenu.
Dak 15: “Tumieni Magazeti Yetu Vema Kabisa.” Hotuba ya kutolewa kwa idili na mwangalizi wa utumishi, inayotegemea fungu 1 hadi 13 la nyongeza.
Dak 20: “Fuatia Kupendezwa Kote ili Kunufaisha Wengine.” Pitia utoaji mbalimbali uliodokezwa kwa ajili ya ziara za kurudia. Ndugu anayeshughulikia sehemu hii azungumze na wahubiri wawili au watatu juu ya yale watakayosema kisha awaombe waonyeshe utoaji wao mbalimbali.
Wimbo 162 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Septemba 25
Dak 5: Matangazo ya kwenu.
Dak 15: “Fanyeni Yote kwa Utukufu wa Mungu.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yanayoongozwa na mzee. Kadiri wakati uruhusuvyo, toa maelezo ya ziada yanayotegemea Mnara wa Mlinzi la Agosti 15, 1992, kurasa 15-20.
Dak 10: “Kuchunguzwa na Yehova—Kwa Nini Kwanufaisha?” Hotuba yenye kutia moyo ikitolewa na mzee.
Dak 15: “Tumieni Magazeti Yetu Vema Kabisa.” Zungumza pamoja na wasikilizaji fungu 14 hadi 17 la nyongeza. Kazia kufanya jitihada ya pekee ya kugawa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! wakati wa Oktoba. Kwa kuwa magazeti yanachapishwa katika lugha mbalimbali, twapaswa kuwaambia watu wanaosema lugha za kigeni kwamba magazeti yanapatikana katika lugha ya kwao. (Kutaniko la lugha ya kigeni la mahali hapo ambalo limegawiwa eneo hilo lapaswa kujulishwa.) Katika eneo lililohubiriwa mara nyingi, kugawa magazeti yetu kwaweza kuwa njia yenye matokeo zaidi ya kusitawisha kupendezwa, kwa kuwa yanaandaa habari mpya kila juma. Uwe na kikundi cha familia kikionyesha kipindi cha mazoezi, kama vile kifafanuliwavyo katika fungu 14. Pia, elekeza kwenye baadhi ya madokezo yenye kutumika ya kuongeza maangusho.
Wimbo 193 na sala ya kumalizia.