Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/95 kur. 3-5
  • Tumieni Magazeti Yetu Vema Kabisa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumieni Magazeti Yetu Vema Kabisa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Toa Magazeti Katika Huduma
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Magazeti Yatangaza Ufalme
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Weka Kando Wakati kwa Ajili ya Utendaji wa Magazeti
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Toa Magazeti Kwenye Kila Fursa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 9/95 kur. 3-5

Tumieni Magazeti Yetu Vema Kabisa

1 Ufikiapo kibanda cha muuza-gazeti, wewe huona nini? Magazeti. Kwenye duka la pembeni, ni nini kinachokuvutia? Magazeti. Hivyo, ni nini ambacho watu wengi wanasoma? Magazeti. Uchunguzi mbalimbali umeonyesha kwamba vijana 9 kati ya 10 walio kati ya umri wa miaka 10 na 18, na asilimia iyo hiyo ya watu wazima, husoma angalau gazeti moja kila mwezi. Ulimwengu ni wenye utambuzi juu ya magazeti.

2 Je, twaweza kufanya watu wenye moyo wa kufuatia haki wawe wenye utambuzi juu ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!? Ndiyo, ikiwa SISI ni wenye utambuzi juu ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ni nini kiwezacho kutusaidia? Fikiria madokezo haya:

◼ Soma Magazeti: Mwangalizi mmoja asafiriye aliripoti kwamba, kwa wastani, ni mhubiri mmoja tu kati ya 3 katika mzunguko wake asomaye kila toleo la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kutoka jalada hadi jalada. Je, wewe huyasoma? Usomapo kila makala, jiulize mwenyewe, ‘Ni nani angethamini habari hii—mama, mwagnosti (mtu aaminiye kwamba ya Mungu hayawezi kujulikana), mfanya-biashara, kijana?’ Katika nakala yako binafsi, tia alama jambo moja au mawili ambayo waweza kutumia unapotoa hilo gazeti. Kisha ufikirie jinsi waweza kuamsha kupendezwa katika habari kwa kutumia sentensi moja au mbili tu.

◼ Uwe na Agizo Hususa la Magazeti: Toa agizo la kihalisi kwa ndugu anayeshughulika na magazeti ukiomba idadi hususa ya nakala ya kila toleo. Kwa njia hiyo, wewe na familia yako mtakuwa na ugavi wa kawaida na wa kutosha wa magazeti.

◼ Ratibu Siku ya Magazeti ya Kawaida: Makutaniko mengi yameweka kando siku iliyochaguliwa kwa ajili hasa ya utoaji-ushahidi wa magazeti. Je, wewe waweza kuunga mkono Siku ya Magazeti ya kutaniko? Ikiwa sivyo, jaribu kutumia wakati fulani wa utumishi pindi kwa pindi kwa ajili ya utoaji-ushahidi wa barabarani kwa kutumia magazeti na ugawaji wa kibinafsi wa magazeti, kutoka nyumba kwa nyumba na pia kwenye njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida.

◼ Uwe Mwenye Utambuzi Juu ya “Mnara wa Mlinzi” na “Amkeni!”: Chukua nakala za magazeti unaposafiri au kwenda kununua vitu. Yatoe unapoongea na wafanyakazi wenzako, majirani, wanashule wenzako, au walimu. Mume na mke fulani ambao mara nyingi husafiri kwa ndege hutumia jambo katika mojapo magazeti ya karibuni ili kuanzisha mazungumzo pamoja na abiria ambaye ameketi karibu nao. Wamekuwa na maono mengi yenye kufurahia. Vijana wengine huleta shuleni kwa kawaida makala ambazo wamehisi zitapendeza walimu wao au wanafunzi wenzao. Chukua nakala unapofanya shughuli mbalimbali, na uyatoe kwa wauzaji baada ya wewe kumaliza shughuli yako. Wengi wetu hununua petroli kwa kawaida; kwa nini usiyatoe magazeti kwa mfanyakazi kwenye stesheni ya petroli? Yaweke tayari wakati watu wa ukoo wanapotembelea, unapotumia magari ya watu wote, au unapongojea kwa ajili ya miadi fulani. Je, waweza kufikiria pindi nyinginezo zinazofaa?

◼ Tayarisha Utoaji Mfupi wa Magazeti: Panga kusema machache tu, lakini uyaseme vizuri. Uwe mwenye idili. Vutia moyo. Sema kimahususi. Chagua wazo moja kutoka katika makala fulani, eleza juu yalo kwa maneno machache, na uyatoe magazeti. Utoaji ulio bora zaidi hutokeza swali juu ya habari yenye kupendeza kisha huelekeza kwenye makala inayotoa jibu la Kimaandiko. Fikiria vielelezo vichache vya jinsi hilo laweza kufanywa:

3 Ikiwa unakazia makala juu ya kuongezeka kwa kiasi cha uhalifu, ungeweza kuuliza hivi:

◼ “Ni nini kingehitajiwa ili kutuwezesha tulale usingizi usiku bila kuhofu uhalifu?” Huenda mwenye-nyumba asitazamie kwamba mambo yatakuwa bora zaidi. Waweza kujibu kwamba watu wengi huhisi vivyo hivyo na uongeze kwamba una habari ambayo wewe waamini itakuwa yenye kupendeza kwake. Kisha urejezee jambo linalofaa katika hiyo makala.

4 Unapotoa makala juu ya maisha ya familia, waweza kusema hivi:

◼ “Watu wengi huona kwamba ni jambo gumu kwelikweli kupata riziki na kulea familia siku hizi. Vitabu kadhaa vimeandikwa juu ya habari hii, lakini hata wastadi hawakubaliani juu ya masuluhisho kwa matatizo yetu. Je, kuna popote tuwezapo kupata mwongozo wenye kutegemeka?” Kisha uelekeze kwenye elezo hususa katika gazeti linaloonyesha hekima inayopatikana katika Biblia.

5 Waweza kutumia njia hii unapokazia makala juu ya tatizo fulani la kijamii:

◼ “Watu walio wengi wako chini ya mbano leo. Mungu hakukusudia sisi tuishi katika njia hii.” Kisha uonyeshe jinsi habari yenye msingi wa Biblia katika makala iwezavyo kutusaidia tukabiliane na matatizo ya maisha sasa na kuandaa tumaini la suluhisho lenye kudumu katika wakati ujao.

6 Utoaji-Ushahidi wa Barabarani Una Matokeo: Ni katika toleo la Informant (Huduma ya Ufalme Yetu) ya Januari 1940 kwamba wahubiri walitiwa moyo kwa mara ya kwanza kuratibu siku ya pekee kila juma kwa ajili ya utoaji-ushahidi wa barabarani kwa kutumia magazeti. Je, wewe hushiriki katika utoaji-ushahidi wa barabarani mara kwa mara katika maeneo yanayofaa? Ikiwa wewe hufanya hivyo, je, njia unayotumia ni yenye matokeo kwelikweli? Wahubiri fulani wameonwa wakiwa wamesimama kwenye pembe ya barabara yenye shughuli nyingi, wakisemezana huku watu wengi mno wakiwa wamepita bila kuonwa. Badala ya kusimama karibu-karibu mkiwa na magazeti, ni jambo lenye matokeo zaidi kutengana na kufikia watu. Watu msiowajua waweza kusimama na kusikiliza kwa ufupi wakifikiwa na mtu mmoja peke yake, lakini ni wachache ambao wangechukua hatua ya kwanza kufikia kikundi cha watu wanaoshughulika sana katika mazungumzo. Kwa kuwa sisi huvutia uangalifu mwingi barabarani, kuna uhitaji wa pekee wa kuwa wenye kujipamba vema, na tukiwa tumevaa mavazi yenye kiasi kama inavyostahili wahudumu wa Mungu.—1 Tim. 2:9, 10.

7 Njia za Kupelekea Watu Magazeti kwa Ukawaida: Wale walio na njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida huangusha magazeti mengi hata ingawa maeneo yanahubiriwa kwa kawaida. Njia za kupelekea watu magazeti kwa ukawaida ni chanzo bora sana cha kuweza kuanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani.

8 Unapofanya ziara za kurudia za kawaida ili kupeleka magazeti, utaona kwamba uchangamfu na urafiki kati ya wewe na mwenye-nyumba utakua. Kadiri mnavyofahamiana vizuri, ndivyo itakavyokuwa rahisi zaidi kuzungumzia habari za Kimaandiko. Hilo laweza kuongoza kwenye kuanzisha funzo la Biblia nyumbani lenye matokeo. Kwenye ziara ambazo ni wazi kwamba kuna uthamini kwa magazeti, toa andikisho. Na ukumbuke kwamba, kila mara unapowasiliana na mwenye-nyumba wewe waweza kuripoti ziara ya kurudia.

9 Dada mmoja alipeleka magazeti kwa kawaida kwa mwanamke ambaye sikuzote aliyakubali lakini alisema: “Siamini unayoniambia.” Kwenye ziara ya baadaye, dada huyo alimpata mume wa yule mwanamke nyumbani. Baada ya mazungumzo yenye urafiki, mipango ilifanywa ili kuanzisha funzo la Biblia. Dada huyo alifanya urafiki na wana watatu waliokuja kujiunga na funzo hilo. Hatimaye, mama na wana wake waliweka wakfu maisha zao kwa Yehova wakabatizwa. Hadi sasa, washiriki 35 wa hiyo familia wamekubali kweli. Hayo yote ni kwa sababu huyo dada alifuatia njia yake ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida!

10 Kuna njia nyingi za kuanzisha njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida. Waweza kuanzisha njia hiyo kwa kurekodi tu maangusho yako na kupanga kurudi ukiwa na matoleo ya karibuni zaidi. Njia moja ni kutumia habari chini ya kichwa “Katika Toleo Letu Linalokuja.” Unaporudi, mwambie mwenye-nyumba kwamba una makala uliyotaja hapo mbele. Au, unapofanya ziara ya kurudia, ungeweza kusema hivi: “Niliposoma makala hii, nilifikiri ingeweza kukupendeza . . . ” Kisha utoe maelezo mafupi machache juu ya hiyo makala na uitoe. Umalizapo hiyo ziara, andika mambo matano yaliyo sahili kwenye rekodi yako ya nyumba kwa nyumba: (1) jina la mwenye-nyumba, (2) anwani ya mwenye-nyumba, (3) tarehe ya ziara, (4) matoleo yaliyoangushwa, na (5) makala iliyokaziwa. Wahubiri fulani wamekuwa wenye mafanikio sana katika kusitawisha njia za kupelekea watu magazeti kwa ukawaida, wakiwa na ziara zinazofikia 40 au zaidi kwenye orodha zao!

11 Eneo la Biashara: Magazeti mengi yanaangushwa na wahubiri wanaohubiri eneo la biashara. Je, umejaribu kazi ya duka hadi duka? Ripoti zaonyesha kwamba katika makutaniko fulani, si wengi wanaoshiriki katika sehemu hii ya utumishi. Mwanzoni, wengine wanahofu kuwatembelea wafanya-biashara, lakini baada ya wao kujaribu kufanya hivyo kwa mara chache, wanaliona kuwa jambo lenye kupendeza na lenye kuthawabisha. Kwa nini usimwombe mhubiri au painia mwenye uzoefu akusaidie uanze kufanya hivyo?

12 Kuna faida nyingi za kuhubiri kutoka duka hadi duka. Ni wachache sana wasiopatikana, angalau wakati wa saa za biashara! Mara nyingi wafanya-biashara ni wenye hisani, hata ikiwa huenda wasipendezwe sana na Biblia. Anza mapema; yaelekea utakaribishwa vizuri zaidi. Baada ya kujijulisha mwenyewe, waweza kusema kwamba mara nyingi hupati wafanya-biashara nyumbani, kwa hiyo unawatembelea kwa dakika chache tu kwenye mahali pao pa kazi ili kuwatolea matoleo ya karibuni zaidi ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Onyesha kwamba wafanya-biashara wengi huthamini magazeti yetu kwa sababu wanahitaji kwenda sambamba na matukio ya ulimwengu ya wakati wa sasa lakini hawana wakati mwingi wa kusoma. Haya magazeti hutoa habari yenye kuchochea fikira kutokana na maoni mapya, bila upendeleo wowote wa kidini, wa kisiasa, au wa kibiashara. Njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida yaweza kusitawishwa na watu wenye kupendezwa wanaopatikana katika eneo la biashara.

13 Tayarisheni Mkiwa Familia: Wakati fulani waweza kuwekwa kando wakati wa funzo lenu la familia ili kuzungumza juu ya makala katika magazeti ya karibuni zaidi ambazo zaweza kufaa ili kutumiwa katika eneo lenu. Washiriki wa familia—kutia na watoto—waweza kuwa na zamu za kuzoeza utoaji wao mbalimbali na kushinda vizuizi vya kawaida vinavyotokezwa, kama vile: “Nina shughuli,” “Sisi tuna dini yetu wenyewe,” au “Mimi nimeokoka.” Ushirikiano mzuri waweza kuwezesha familia yote iwe na ushiriki wa kawaida katika ugawaji wa magazeti.

14 Viongozi wa Funzo la Kitabu Waweza Kusaidia: Wakati wowote ufaapo, ratibu mikutano kwa ajili ya utumishi katika Siku ya Magazeti kwenye mahali pa funzo la kitabu badala ya kufanya kutaniko lote likutane kwenye Jumba la Ufalme. Wale wanaosimamia mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani wapaswa kujitayarisha vema wakiwa na madokezo hususa kutolea kikundi. Hayo yaweza kutia ndani utoaji wa mfano na jambo moja au mawili kutoka katika matoleo ya karibuni yawezayo kutumiwa ili kuamsha kupendezwa katika mahali hapo. Mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani—kutia ndani kupanga kikundi—yapaswa iwe mifupi, ikichukua muda usiozidi dakika 10 hadi 15. Viongozi wa funzo wapaswa kuhakikisha kwamba kuna eneo la kutosha ili kikundi hicho kiendelee kuhubiri kwa kipindi chote cha utumishi wa shambani.

15 Onyesha Uthamini kwa Magazeti: Makala “Kutumia Vema Mnara wa Mlinzi na Amkeni!” iliyochapishwa katika toleo la Julai 1993 la Huduma ya Ufalme Yetu ilitoa jambo hili la maana: “Mnara wa Mlinzi na Amkeni! hayapotezi thamani yayo, hata kama yote hayajaangushwa kwa mwezi mmoja au miwili ya tarehe yao ya kutolewa. Habari iliyo ndani yayo haipungui umaana wakati unapopita . . . Kuruhusu magazeti ya zamani yarundamane na kutoyatumia kamwe kwaonyesha ukosefu wa uthamini kwa zana hizi zenye thamani. . . . Badala ya kuweka kando matoleo ya zamani na kuyasahau, je, haingekuwa afadhali kufanya jitihada ya pekee kuyaacha mikononi mwa watu wenye kupendezwa?”

16 Leo kuna watu wengi wenye mioyo ya kufuatia haki wanaojitahidi kutafuta kweli. Habari iliyo ndani ya gazeti moja yaweza kuwa jambo wanalohitaji hasa ili kuwaongoza kwenye hiyo kweli! Yehova ametupa sisi ujumbe wenye kusisimua wa kupiga mbiu, na magazeti yetu yana fungu la muhimu katika kupelekea wengine ujumbe huo. Je, wewe utakuwa mwenye utambuzi zaidi juu ya ugawaji wa magazeti katika wakati ujao? Je, utatumia baadhi ya madokezo haya katika mwisho-juma uu huu? Utabarikiwa sana ukifanya hivyo.

Madokezo Yenye Kutumika:

◼ Soma magazeti kimbele, pata kuzifahamu makala.

◼ Chagua makala inayoshughulika na jambo lenye kupendeza watu kwa ujumla katika jumuiya yenu.

◼ Tayarisha utoaji utakaowafaa watu mbalimbali, iwe ni wanaume, wanawake, au vijana. Onyesha jinsi hilo gazeti linavyomhusu mwenye-nyumba na jinsi familia yote itakavyolifurahia.

◼ Panga kushiriki katika utendaji wako wa utumishi wa shambani wakati ambapo watu walio wengi wamo nyumbani. Makutaniko mengine hupangia utoaji-ushahidi wa jioni kwa kutumia magazeti.

◼ Weka utoaji wako ukiwa mfupi na wenye kutaja mambo moja kwa moja.

◼ Usiongee upesi mno. Ikiwa msikilizaji wako hapendezwi, kuongea upesi zaidi hakutasaidia. Jaribu kustarehe, na kumpa mwenye-nyumba fursa ya kuitikia.

Kutoa Magazeti Nyumba kwa Nyumba:

◼ Uwe na tabasamu yenye urafiki na sauti yenye fadhili.

◼ Uwe mwenye idili juu ya magazeti.

◼ Sema polepole na kwa wazi.

◼ Sema juu ya habari moja tu; chochea kupendezwa kwa ufupi, na uonyeshe thamani yalo kwa mwenye-nyumba.

◼ Kazia makala moja tu.

◼ Kazia gazeti moja tu, ukitoa lile jingine likiwa jenzilo.

◼ Mpe mwenye-nyumba magazeti.

◼ Mjulishe mwenye-nyumba juu ya mpango wako wa kurudi.

◼ Uwe na umalizio wenye urafiki, ulio chanya ikiwa magazeti yanakataliwa.

◼ Andika kwenye rekodi ya nyumba kwa nyumba juu ya kupendezwa kote na maangusho yote.

Fursa za Kuangusha Magazeti:

◼ Utoaji-ushahidi wa nyumba kwa nyumba

◼ Utoaji-ushahidi wa barabarani

◼ Kazi ya duka hadi duka

◼ Njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida

◼ Utoaji-ushahidi wa jioni

◼ Wakati wa ziara za kurudia

◼ Kutembelea wale waliokuwa wanafunzi wa Biblia hapo awali

◼ Wakati wa kusafiri, wakati wa kununua vitu

◼ Wakati wa kuongea na watu wa ukoo, wafanyakazi wenzako, majirani, wanashule wenzako, walimu

◼ Katika magari ya watu wote, katika vyumba vya kungojea

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki