Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/95 uku. 4
  • Kila Andiko Ni Lenye Manufaa kwa Kufundisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kila Andiko Ni Lenye Manufaa kwa Kufundisha
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Thamani ya Biblia Katika Ulimwengu wa Leo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Biblia—Kiongozi Ambacho Mungu Amewapa Watu Wote
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari Unazoweza Kutumia Katika Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Neno la Mungu Huandaa Mwongozo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 11/95 uku. 4

Kila Andiko Ni Lenye Manufaa kwa Kufundisha

1 Maoni juu ya thamani ya Biblia ni mengi na ya namna mbalimbali. Hata hivyo, tunasadikishwa kwamba kurasa zayo zina majibu kwa matatizo magumu ya wanadamu na pia zina mwongozo kwa mwendo wetu wa kibinafsi maishani. (Mit. 3:5, 6) Hekima ya shauri layo haina kifani. Viwango vya kiadili iteteavyo havipitiki. Ujumbe wayo ni wenye nguvu, “[ukiweza] kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.” (Ebr. 4:12) Twaweza kusaidiaje wengine waone uhitaji wa kuchukua kitabu hiki kutoka kwenye rafu na kukichunguza kwa uangalifu? Huenda ukataka kujaribu baadhi ya madokezo yafuatayo unapotoa New World Translation pamoja na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? katika Novemba.

2 Kwa kuwa watu wengi huhangaika juu ya kutimiza mahitaji yao ya msingi, labda mfikio huu ungevuta uangalifu wao:

◼ “Watu wengi ambao ninaongea nao siku hizi wanahangaikia kutimiza wajibu wao mbalimbali wa kifedha. Wengi hunaswa katika ufuatiaji wa vitu vya kimwili, na huo hutokeza mkazo wa akilini. Je, ni wapi palipo mahali bora zaidi pa kugeukia ili kupata shauri juu ya mambo ya jinsi hiyo? [Ruhusu itikio.] Nimeona kwamba Biblia hutoa shauri lifanyalo kazi ambalo laweza kutusaidia tuepuke matatizo yasiyo ya lazima. Acha nikuonyeshe kielelezo.” Fungua kwenye ukurasa 163 katika kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? na usome 1 Timotheo 6:9, 10, lililonukuliwa katika fungu 3. Toa maelezo ya ziada juu ya fungu 4, kisha utoe kitabu.

3 Hili ni dokezo jingine ambalo waweza kutumia:

◼ “Kila wakati tusomapo gazeti au tusikilizapo habari twasikia juu ya tatizo jingine lenye kutaabisha ambalo hutufanya tuhangaike. [Taja tukio fulani lenye kusumbua lililoripotiwa majuzi katika habari.] Twaweza kukabilianaje na matatizo kama haya? [Ruhusu itikio.] Huko nyuma katika 1983 yule aliyekuwa rais wa Marekani wakati huo [Ronald Reagan] alisema kwamba Biblia ina ujumbe mkubwa zaidi uliopata kuandikwa wakati wowote na kwamba ‘kurasa zayo zina majibu yote kwa matatizo yote ambayo wanadamu wamepata kujua.’ Kile alichosema chatukumbusha kile ambacho Biblia yenyewe husema. [Soma 2 Timotheo 3:16, 17.] Acha nikuonyeshe ni kwa nini tuna uhakika katika Biblia.” Onyesha mambo fulani makuu kutoka katika trakti Sababu Kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia. Jitolee kurudi baadaye ili kuzungumza juu ya jinsi lilivyo jambo la kutokeza kwamba unabii mbalimbali wa Biblia unatimizwa katika matukio ya ulimwengu ya wakati wa sasa.

4 Ikiwa kuna watu wengi wasio wa kidini katika eneo lenu, waweza kujaribu mfikio huu:

◼ “Watu wengi katika eneo hili huona vitabu fulani vitakatifu kuwa vyenye kujipinga na kuwa ngano tu. Wameona mambo mabaya mengi sana yakifanywa katika jina la dini hivi kwamba hawaitumaini hata Biblia. Kwa kweli, watu wengi zaidi na zaidi wanajiuliza kama Biblia ni Neno la Mungu au la binadamu. Maoni yako ni nini?” Ruhusu jibu. Ikitegemea itikio la mwenye nyumba, fungua kitabu Biblia—Neno la Mungu au Binadamu? kwenye sehemu inayoshughulikia pingamizi au maoni ya mwenye nyumba, na uzungumze juu ya jambo moja au mawili. Kwa kielelezo, huenda ukawa na fursa ya kutumia mafungu 27-29 kuanzia ukurasa 66, chini ya kichwa kidogo “Yesu—Mtu Halisi.”

5 Mfunzi wetu Mtukufu amehakikisha kwamba ujuzi juu ya mapenzi yake unapatikana kwa wote watakao kujifunza. Kusaidia wengine wathamini thamani halisi ya Biblia ni mojapo mambo mazuri zaidi tuwezayo kufanya kuwasaidia; kwaweza kuokoa uhai wao.—Mit. 1:32, 33.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki