Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/93 uku. 8
  • Thamani ya Biblia Katika Ulimwengu wa Leo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Thamani ya Biblia Katika Ulimwengu wa Leo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Habari Zinazolingana
  • Kulipendekeza Neno la Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Biblia—Kiongozi Ambacho Mungu Amewapa Watu Wote
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Weka Msingi Katika Ziara Yako ya Kwanza
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Kitabu Kiandaacho Mwongozo wa Kweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 11/93 uku. 8

Thamani ya Biblia Katika Ulimwengu wa Leo

1 Wengi leo huona Biblia kuwa ya kale na isiyo halisi. Ingawa hicho ni kitabu chenye kugawanywa kwa mweneo mkubwa zaidi na kutafsiriwa zaidi katika historia yote, ni wachache sana kwa kulinganishwa wakisomacho, na wachache hata zaidi wanaofuata mwelekezo wacho.

2 Kinyume cha hilo, twathamini Biblia kuwa Neno la Mungu. Mambo hakika yaonyesha kwamba hiyo ni ya kweli kihistoria. Isitoshe, upatano wayo wenye kutokeza, unabii wayo mwingi, hekima yayo, na kuwa kwayo kani yenye kuchochea inufaishayo maisha za watu yote hayo yaonyesha kwamba Biblia ni yenye “pumzi ya Mungu.” (1 Tim. 3:16) Ono letu la kibinafsi na uthamini wetu kwa ajili ya zawadi hiyo nzuri ajabu wapasa kutusukuma kuwatia moyo wengine wachunguze thamani yayo ya kweli.

3 Mfikio mmoja waweza kuwa:

◼ “Kwa sababu ya matatizo makubwa yakabiliyo ainabinadamu, watu wengi huona vigumu kuwa na maoni yafaayo juu ya wakati ujao. Wewe wahisije juu ya hilo? [Ruhusu itikio.] Angalia kichwa cha trakti hii, Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani.” Vuta fikira kwenye kielezi katika jalada, halafu usome fungu la kwanza na la pili kwenye ukurasa 2. Hakikisha kuzungumzia Maandiko yaliyotajwa ukikazia kwamba hiyo ni ahadi ya Mungu. Ikiwezekana, jaribu kuzungumzia mafungu yote kufikia kichwa kidogo cha kwanza. Fanya mipango ya kurudi ili kuzungumzia trakti hiyo zaidi—labda ukitumia kimojapo vichwa vidogo, katika namna ya swali, ili kuchochea kupendezwa.

4 Mfikio mwingine waweza kuwa jambo linalofanana na hili:

◼ “Je! hukubali kwamba ainabinadamu yahitaji mwelekezo katika kushughulikia matatizo ya maisha? [Ruhusu itikio.] Zamani, mara nyingi watu waliitegemea Biblia ili kupata mwongozo, lakini nyakati zimebadilika. Je! wafikiri kwamba Biblia ni yenye thamani ifaayo leo? [Ruhusu itikio.] Angalia yanayosemwa kwenye 2 Timotheo 3:16. [Soma.] Neno la Mungu lililoandikwa halitusaidii tu kufanya maamuzi yenye hekima bali pia huandaa tumaini lenye kutegemeka kwa ajili ya wakati ujao.” Soma Yohana 17:3. Halafu waweza kutaja jambo moja au mawili hususa ambayo umetangulia kuchagua kutoka kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? ili kutoa kielezi cha thamani ya Biblia ifaayo.

5 Huenda ukaona kuwa jambo lenye msaada kutumia baadhi ya matangulizi yaliyoonyeshwa katika ukurasa 9 wa kitabu Kutoa Sababu chini ya kichwa kidogo “Biblia/Mungu.” Habari zaidi imetolewa kwenye kurasa 40-49 ambayo yaweza kusaidia katika kujibu maswali ya wenye-nyumba au katika kushinda vipingamizi vyao.

6 Kutoa Biblia New World Translation: Biblia New World Translation yaweza kutolewa katika mahubiri ya kwanza au katika ziara ya kurudia. Huenda ukauliza kama mwenye nyumba ana nakala ya Biblia na kama yeye huona ikiwa rahisi kuisoma. Ikitegemea jibu, vuta fikira kwenye baadhi ya mambo yenye kusaidia ya Biblia New World Translation. Waweza kukazia jambo moja au mawili kutoka kurasa 248-52 za kitabu Kutoa Sababu.

7 Uwe macho kuona fursa za kutia watu moyo wasome Biblia. Saidia watu wenye kupendezwa wakuze staha na upendo kwa Neno la Mungu lililoandikwa. Kwa kutumia kanuni zayo katika maisha zao binafsi na kuja kwenye ujuzi wa kweli, wao watapata manufaa nyingi sasa na katika wakati ujao pia.—Zab. 119:105.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki