Mikutano Ya Utumishi Kwa Desemba
Juma Linaloanza Desemba 4
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo Yaliyoteuliwa kutoka kwenye Huduma ya Ufalme Yetu. Pia shughulikia “Desemba Imefika Tena.”
Dak 15: “Msifu Yehova Kila Siku.” Maswali na majibu. Mafungu yasomwe. Panga uwe na mhubiri mmoja au wawili waeleze mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo walipokuwa wakitoa ushahidi wa vivi hivi.
Dak 20: “Kutoa Kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi.” Kwa idili pendekeza kutoa kitabu hiki, katika Desemba. Pitia utoaji uliodokezwa, na uwe na mmoja au mbili zikitolewa wonyesho.
Wimbo 224 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 11
Dak 13: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Pitia kifupi sababu tunazopaswa kupangia ushiriki kamili na wenye maana katika utumishi wa shambani. Badala ya kuhubiri kwa saa moja tu hivi tunapotoka, kwa nini tusipange kukaa kwa saa mbili au zaidi ikiwezekana? Mafanikio mara nyingi hutegemea kupanga ziara za kurudia mapema na kupanga kuhubiri na wengine ambao wanakusudia kukaa kwa saa mbili au zaidi.
Dak 15: Mahitaji ya kwenu. Au hotuba ikitegemea makala “Thawabu za Udumifu,” kutoka kwenye Mnara wa Mlinzi, Agosti 1, 1995, kurasa 25-29.
Dak 17: “Jitayarishe Kwa Ajili Ya Mikutano ya Kutaniko na Uifurahie.” Hotuba na mazungumzo. Alika mhubiri mmoja au wawili wasimulie wanachofanya kiwasaidie kuifurahia mikutano na kunufaika kikamili nayo.
Wimbo 28 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 18
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Toa madokezo kadhaa ya jinsi ya kuitikia salamu za sikukuu kwa busara. Tangaza mipango ya ushahidi wa pekee wakati wa Desemba 25.
Dak 15: “Fanya Maendeleo Yako Yawe Dhahiri.” Maswali na majibu.
Dak 20: “Rudia Wale Walioonyesha Kupendezwa.” Pitia toaji zilizodokezwa, na upange kuwa na maonyesho mawili mafupi. Tia moyo wote wafanye ziara za kurudia wakiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo.
Wimbo 44 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 25
Dak 5: Matangazo ya kwenu. Ikiwa saa za mikutano yenu zimefikia wakati wa kubadilishwa Januari 1, toa kitia-moyo kwa wote waunge mkono kikamili kwa kufanya marekebisho yoyote yahitajiwayo. (Ona Huduma ya Ufalme Yetu, ya Desemba 1994, ukurasa wa 2.) Tangaza mipango ya ushahidi wa pekee wakati wa Januari 1.
Dak 15: Sanduku la Swali. Mwangalizi wa shule aweza kuzungumza pamoja na mzee mwingine au mtumishi wa huduma. Tia moyo wale waliogawiwa kusoma mafungu kwenye mikutano ya kutaniko walichukue pendeleo hilo kwa uzito na wajitayarishe mapema.
Dak 25: “Kuacha Nuru Yetu Inga’e kwa Uendelevu.” Mzee anayeshughulikia sehemu hii atategemeza utangulizi mfupi kwenye mafungu 1-5. Mafungu 6-16 yashughulikiwe kwa maswali na majibu. Soma mafungu 6-9, 15, na 16. Tumia mafungu 17-19 kuwa umalizio mfupi. Ikishughulikiwa na mwangalizi wa utumishi ikiwezekana.
Wimbo 3 na sala ya kumalizia.