Jitayarishe Kwa Ajili Ya Mikutano ya Kutaniko na Uifurahie
1 Tukiwa ushirika wa ndugu, kwa hekima sisi hukutanika kikawaida kwa ajili ya mikutano yetu ya kila juma. (1 Tim. 4:15, 16) Tunaweza kuifurahiaje na kupata manufaa zaidi kutokana nayo?
2 Wakati wapaswa kuwekwa kando kwa ukawaida ili kujitayarisha kwa ajili ya mikutano. Wengine huenda wakaweza kutumia wakati mwingi zaidi katika kujitayarisha kuliko wengine. Hata hivyo, haidhuru tuna shughuli jinsi gani, ni jambo la hekima kutafuta wakati fulani ili kujitayarisha kwa ajili ya mikutano. Kujitayarisha pamoja mkiwa familia ni kwenye manufaa hasa.—Efe. 5:15, 16.
3 Kwa Ajili Ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi: Jaribu kwenda sambamba na ratiba ya usomaji wa Biblia kila juma. (Yos. 1:8) Pitia habari itakayoshughulikiwa, na ulete vichapo vihitajiwavyo ili uweze kufuatana na wasemaji. Fikiria njia ambazo waweza kutumia habari hii katika huduma yako.
4 Kwa Ajili Ya Mkutano wa Utumishi: Tazama programu iliyowekwa katika Huduma ya Ufalme Yetu. Soma makala zitakazozungumziwa. Ikiwa habari kutoka kwenye Mnara wa Mlinzi au kichapo kinginecho itachunguzwa, ifungue na uisome pia. Ikiwa utoaji wa utumishi wa shambani utatolewa, pitia hayo mapema ili uwe tayari kuutumia katika huduma yako.
5 Kwa Ajili Ya Funzo la Mnara wa Mlinzi: Soma habari hiyo mapema, ukitia alama majibu ya maswali. Kufungua maandiko yaliyotajwa kutakusaidia upate uelewevu mzuri zaidi. Kutafakari jinsi habari hiyo inalingana na mambo unayojua tayari kutapanua ujuzi wako. Panga kushiriki wakati wa funzo kwa kutayarisha maelezo mafupi kwa angalau fungu moja au mawili. Hii ni njia ya maana ya kufanya “ungamo la tumaini letu.”—Ebr. 10:23.
6 Kwa Ajili Ya Funzo la Kitabu la Kutaniko: Kwanza, angalia kwa ujumla habari; fikiria kichwa cha sura na vichwa vidogo. Kisha, unaposoma, chunguza kwa uangalifu mambo makuu. Pitia mistari ya Biblia yenye kuyaunga mkono. Jaribu kujibu maswali kwa maneno yako mwenyewe. Baada ya kutayarisha habari hiyo, ipitie akilini mwako. Jaribu kukumbuka mambo makuu na njia ya kutoa sababu.—2 Tim. 2:15.
7 Ifurahie Mikutano: Ili uifurahie mikutano kikamili, ni jambo la maana uwahi ili ushiriki sala ya kufungua, ya kuomba roho takatifu ya Yehova. Pia unanufaika na nyimbo za Ufalme zenye kuburudisha. Ikiwa huna watoto wachanga au sababu nyingine ya kukaa nyuma ya jumba, yamkini utaona kwamba ukikaa mbele, kutakuwa na vikengeusha fikira vichache zaidi na utanufaika zaidi na programu. Wazazi walio na watoto wadogo ambao huenda wakahitaji kupelekwa nje wakati wa mkutano waweza kupunguza vikengeusha fikira kwa kuketi karibu na sehemu ya kupitia ya jumba na nyuma.
8 Jitahidi kuangalia maandiko yanayosomwa. Kufanya hivi kutakusaidia kukumbuka unayosikia. Kuzungumza na familia na rafiki zako kuhusu unayojifunza kutakazia habari akilini mwako. Kutumia madokezo haya kutafanya mikutano iwe yenye maana na yenye kufurahisha zaidi, na kwa kweli ‘itatuhimiza katika upendo na kazi nzuri.’—Ebr. 10:24, 25.