Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/95 uku. 1
  • Msifu Yehova Kila Siku

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msifu Yehova Kila Siku
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Enyi Vijana, Msifuni Yehova!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Msifu Yehova Kila Siku
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Unaweza Kuhubiri Isivyo Rasmi!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Chukua Kila Fursa Kutoa Ushuhuda—Sehemu 1
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 12/95 uku. 1

Msifu Yehova Kila Siku

1 Mungu wetu, Yehova, ni wa ajabu, Muumba mwenye upendo, Chanzo cha uhai na furaha yote. Kwa sababu ya ukuu wake, yeye kwa kweli anastahili sifa kutoka kwa viumbe vyake vyote. Tukiwa mtu mmoja-mmoja twataka kusema kama alivyosema mtunga-zaburi: “Nitazidi kuongeza sifa zake zote. Kinywa changu kitasimulia haki na wokovu wako mchana kutwa.” (Zab. 71:14, 15) Ili kufanya hivi, lazima tutafute njia za kumsifu Yehova siku kwa siku na kuchochewa kusema vema juu yake, uadilifu wake, na maandalizi yake ya wokovu.

2 Wakristo wa mapema waliweka kielelezo chema cha kumsifu Yehova. Kulingana na wale 3,000 waliobatizwa kwenye Pentekoste, twasoma hivi kwenye Matendo 2:46, 47: “Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, . . . wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.” Walikuwa wakijifunza kweli za ajabu kuhusu Yehova na Mesiya wake. Shangwe yao ilikuwa yenye kuambukiza, wakitia moyo hata wengine wasikilize na kujifunza na kumsifu Yehova.

3 Fursa Zipo Kila Siku: Leo wengi huona kwamba wanaweza kumsifu Yehova kila siku kwa kutoa ushahidi wa vivi hivi. Kupanga kimbele huwasaidia wawe wenye matokeo zaidi. Dada aliyekuwa ameazimia kutoa ushahidi wa vivi hivi aligundua kwamba mtu fulani alikuwa amevunja madirisha mawili na kuingia kwa nguvu katika gari lake. Aliita watu wa kurekebisha kisha akajitayarisha kumtolea ushahidi fundi. Utayarishaji wake ulitia ndani kuomba mwelekezo wa Yehova. Matokeo yalikuwa kwamba, alimtolea ushahidi huyo fundi kwa saa moja na kumwangushia kitabu Kuishi Milele.

4 Dada mwingine alikutana na jirani kwa ukawaida walipokuwa wakitembeza mbwa zao. Wakati wa kutano moja, walikuwa na mazungumzo yenye uzito juu ya matatizo ya maisha, na hilo likaongoza kwenye mazungumzo zaidi. Halafu, funzo la Biblia likaanzishwa. Kwa kupendeza, baadaye jirani huyo alikiri kwamba yeye asingalisikiliza Mashahidi wa Yehova ikiwa wangalimtembelea mlangoni pake, kwa kuwa hakuamini Mungu wala Biblia.

5 Wengine huona inawezekana kutoa ushahidi wakati wachuuzi au wengine wanapokuja milangoni pao. Dada mmoja katika Ireland alitembelewa na mwanamume aliyekuwa akiuza bima ya maisha. Dada huyo alimwelezea kwamba anatazamia kufurahia uhai udumuo milele. Hili lilikuwa wazo jipya kabisa kwa mwanamume huyu, aliyekuwa amelelewa akiwa Mkatoliki wa Kiroma. Alikubali kitabu Kuishi Milele, akahudhuria mkutano juma lililofuata, akakubali kuwa na funzo la Biblia. Sasa mchuuzi huyu ni ndugu aliyebatizwa.

6 Sisi sote twapaswa kuwa chonjo kuona fursa za kumsifu Yehova kila siku. Ni jambo lenye kusaidia kuwa na magazeti au trakti chache mahali ziwezapo kuonekana na zaweza kutolewa kwa urahisi kwa wageni. Mahali penginepo wakati mchache unaotumiwa kwenye kiti cha bustani waweza kukupa nafasi kadhaa za kutolea ushahidi wengine wanaotua ili kupumzika kwa dakika chache. Baadhi ya vijana Mashahidi walio shuleni huweka fasihi ya Biblia kwenye dawati zao ikiwa njia ya kuanzisha mazungumzo na mtu anayeiona na kuuliza maswali. Kumbuka Andiko moja au mawili unayoweza kutumia. Mwombe Yehova akusaidie. Utabarikiwa kwa kufanya hivyo.—1 Yoh. 5:14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki