Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/09 uku. 3
  • Msifu Yehova Kila Siku

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msifu Yehova Kila Siku
  • Huduma ya Ufalme—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Msifuni Yehova kwa Shangwe Siku kwa Siku!
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Msifuni Yehova Mungu Wetu
    Mwimbieni Yehova
  • Msifuni Yehova Mungu Wetu!
    ‘Mwimbieni Yehova kwa Shangwe’
  • Enyi Vijana, Msifuni Yehova!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2009
km 7/09 uku. 3

Msifu Yehova Kila Siku

1. Watumishi wa Mungu wanachochewa kufanya nini, na kwa nini?

1 Maneno ya Mfalme Daudi yanaonyesha azimio lake la kumsifu Yehova “mchana kutwa,” hata milele. (Zab. 145:2, 7, 21) Sisi pia tuna sababu nzuri ya kumsifu Yehova kila siku.—Zab. 37:10; 145:14, 18; 2 Pet. 3:13.

2. Familia zinaweza kumsifu Yehova jinsi gani kila siku?

2 Kumsifu Yehova Nyumbani: Tuna vitabu vyenye kujenga ambavyo hutusaidia katika mazungumzo yetu kumhusu Mungu na Biblia wakati tunapofurahia andiko la siku na Ibada ya Familia, na pia tunapojitayarisha kwa ajili ya mikutano ya kutaniko. Familia nyingi hujitahidi kula pamoja angalau mlo mmoja kila siku. Wanapokula pamoja wanaweza kuzungumza kwa starehe na wanapata nafasi za kumsifu Yehova. Mazungumzo hayo ambayo huanzishwa na wazazi yanaweza kuwasaidia sana kuwalea watoto wao “katika nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova.”—Efe. 6:4; Kum. 6:5-7.

3. Tuna nafasi gani za kumsifu Yehova tunapokuwa pamoja na ndugu zetu?

3 Kumsifu Yehova Pamoja na Ndugu Zetu: Tunapokuwa katika utumishi wa shambani au kwenye mikutano ya kutaniko, tuna nafasi nzuri sana za kumsifu Yehova pamoja na ndugu zetu. (Met. 15:30; Flp. 4:8; Ebr. 13:15) Kwa kuwa sote tunampenda Yehova, ni rahisi kwetu kueleza kutoka moyoni kuhusu wema wa Yehova tunapozungumza mtu na mwenzake.—Zab. 106:1.

4. Unaweza kutumia nafasi gani kumsifu Yehova mbali na kushiriki katika huduma ya shambani?

4 Kumsifu Yehova Tunapozungumza na Watu Ambao Si Mashahidi: Ingawa huenda hali hazituruhusu kushiriki katika huduma ya shambani kila siku, mazungumzo mafupi pamoja na wafanyakazi wenzetu, wanashule wenzetu, na majirani wetu kumhusu Yehova na makusudi yake, yanaweza kuwapa watu wenye moyo mnyofu tumaini. (Zab. 27:14; 1 Pet. 3:15) Dada fulani alipokuwa akisafiri kwa ndege alimhubiria abiria mwenzake. Abiria huyo alifarijika na kutiwa moyo sana na mambo aliyosikia hivi kwamba alimpa dada huyo anwani na nambari yake ya simu ili waendelee kuwasiliana. Ulimwengu unapoendelea kukumbwa na matatizo na hali zinazozidi kuzorota, watu wa Yehova wanaendelea kuwahubiria “habari njema za jambo bora” watu walio tayari kusikiliza. Jambo hilo huwapa tumaini na sababu ya kumsifu Yehova.—Isa. 52:7; Rom. 15:11.

5. Kwa nini tunatamani kumsifu Yehova, na hilo linaweza kuwa na matokeo gani?

5 Yehova hufurahi sana kuwasikia watumishi wake wakimsifu kila siku! Kama vile uumbaji unavyomsifu Yehova, sisi pia tunaweza kumsifu kila siku nyumbani kwetu, kutanikoni, na tunapozungumza na watu ambao bado hawajaanza kumsifu Yehova.—Zab. 19:1-4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki