Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/06 uku. 8
  • Nufaika Kikamili na Mikutano ya Utumishi wa Shambani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nufaika Kikamili na Mikutano ya Utumishi wa Shambani
  • Huduma ya Ufalme—2006
  • Habari Zinazolingana
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani Inayotimiza Kusudi Lake
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Mikutano ya Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Sanduku la Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2006
km 10/06 uku. 8

Nufaika Kikamili na Mikutano ya Utumishi wa Shambani

1 Mikutano yenye manufaa ya utumishi wa shambani hututia moyo na kutupa maagizo yanayofaa kabla ya utumishi. Pia hutuwezesha kushiriki mahubiri katika vikundi ili twende na wengine, kutiana moyo na kujifunza kutoka kwao. (Met. 27:17; Mhu. 4:9, 10) Tunapaswa kufanya nini ili tunufaike kikamili na mikutano hiyo?

2 Kiongozi: Kwa kawaida, mambo ya kuzungumzia kwenye mkutano wa utumishi wa shambani hayaelezwi mapema. Kwa hivyo matayarisho mazuri yanahitajiwa ikiwa utaongoza. Usiamue tu kwamba utachunguza andiko la siku, ingawa unaweza kulitia ndani iwapo linahusu utumishi moja kwa moja. Fikiria kile kitakachowafaa wahubiri siku hiyo. Kwa mfano, huenda ukataka kuzungumzia au kutoa onyesho la utoaji huo. Waweza kupitia jambo fulani katika kitabu Kutoa Sababu, kitabu Shule ya Huduma, sehemu ya karibuni ya Mkutano wa Utumishi. Nyakati nyingine unaweza kuonyesha jinsi ya kukabiliana na kipingamizi fulani katika eneo lenu, au unaweza kuzungumzia jinsi ya kusitawisha upendezi na kuanzisha mafunzo ya Biblia, hasa ikiwa kuna wengi watakaokuwa wakifanya marudio. Chochote kile mtakachochunguza, uwe mchangamfu na mwenye kutia moyo.

3 Anzisha mkutano kwa wakati, hata ukijua kwamba wengine watachelewa. Tumia utambuzi unapopanga vikundi, kisha wapatie eneo wale wanaohitaji. Mkutano huo unapaswa kuchukua kati ya dakika 10 hadi 15 au ikiwa unafanywa baada ya mkutano wa kutaniko unapaswa kuwa mfupi zaidi. Kabla ya mkutano kumalizika, wote wanapaswa kujua wataenda na nani na wataenda wapi. Mkutano huo unapaswa kumalizika kwa sala.

4 Unaweza kusaidia: Kama vile mikutano mingine, tunamwonyesha Yehova heshima na kujali wengine tunapofika kwa wakati. Shiriki mazungumzo. Anayeongoza anaweza kupanga ufanye na mtu fulani au unaweza kufanya mipango yako kabla ya mkutano huo. Ukipendelea kufanya mipango yako, jaribu ‘kupanuka’ kwa kwenda na wahubiri tofautitofauti badala ya kwenda na marafiki walewale wa karibu. (2 Kor. 6:11-13) Baada ya mkutano kumalizika usibadilishe mipango, na uondoke mara moja kuelekea kwenye eneo.

5 Kusudi la mkutano wa utumishi wa shambani ni sawa na lile la mikutano mingine. Imepangwa ili “tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri.” (Ebr. 10:24, 25) Tukijitahidi kupata manufaa kutokana na mikutano hii, itatusaidia kutekeleza utumishi wetu, ambao ni ‘kazi njema’ iliyoje!

[Maswali ya Funzo]

1. Mikutano ya utumishi wa shambani inaweza kutusaidiaje?

2. Kiongozi anaweza kuzungumzia mambo gani?

3. Mkutano unapaswa kuchukua muda gani, na ni nini kinachopaswa kutimizwa kwa wakati huo?

4. Ni nini kitatusaidia kunufaika kikamili na mikutano ya utumishi wa shambani?

5. Ni nini kusudi la mikutano ya utumishi wa shambani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki