Rudi Ili Kuokoa Wengine
1 Ni mapenzi ya Mungu kwamba “watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli.” (1 Tim. 2:4) Twaweza kufanya nini ili kusaidia? Fanya ziara za kurudia ukiwa na lengo la kufundisha kweli. Utasema nini? Madokezo yafuatayo yaweza kukusaidia.
2 Unapozuru mtu aliyekubali kitabu “Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?” waweza kurejezea tena picha iliyo kwenye ukurasa wa 4 na kumuuliza mwenye nyumba:
◼ “Baada ya kuchunguza zaidi kitabu nilichokuachia na kufikiria ahadi ya Mungu ya dunia iliyo paradiso, unahisije kuhusu ahadi hizo nzuri ajabu ambazo Mungu amefanyia wanadamu?” Baada ya kushukuru itikio la mwenye nyumba na kutoa maelezo mafupi juu yalo, unaweza kukazia uangalifu kwenye kurasa 2 na 3 na kudokeza kufikiria kwa nini jitihada za mwanadamu kuelekea amani na usalama, kutia na zile za asili ya kidini, zimeshindwa.
3 Ikiwa uliacha kitabu “Life Does Have a Purpose,” unaweza kuanza tena mazungumzo kwa kusema:
◼ “Nilipokuwa hapa, tulizungumza kuhusu kusudi la Mungu la kuumba ulimwengu mpya wenye amani. Tuliona jinsi tumaini hilo liwezavyo kuleta kusudi na maana halisi maishani mwetu. Sasa swali ni, Lazima tufanye nini ili tustahili baraka hizi? Je, ungejibuje swali hilo?” Ruhusu itikio. Fungua kurasa 181 na 182 na uzungumze mawazo yaliyo katika mafungu 1-3, ukikazia uhitaji wa kujenga imani yenye nguvu kupitia funzo la Neno la Mungu. Eleza jinsi hili linavyoweza kufanywa kwa kutumia kwa manufaa programu yetu ya funzo la Biblia.
4 Unaweza kufuatia angusho la kitabu “Our Incoming World Government—God’s Kingdom” kwa mfikio huu:
◼ “Wakati uliopita nilivuta uangalifu wako kwenye ahadi ya Mungu ya kukomesha kuteseka na jeuri katika ulimwengu. Je, wafikiri Mungu atakomesha mashirika ya kidini na ya kisiasa yanayosababisha taabu nyingi sana kwa wanadamu leo? Labda ulisoma sura ya 11, ‘The Passing of a Divided World.’ Ningependa kuchukua dakika chache tu nichunguze pamoja nawe baadhi ya maandiko yasiyonukuliwa katika sura hiyo.” Mtu huyo akiwa mwenye kupendezwa, unaweza kuyaangalia hayo maandiko na mzungumzie habari iliyo katika mafungu 1-6 kwenye kurasa 175-177.
5 Unaweza kufuatia angusho la kitabu “Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya” kwa kusema:
◼ “Nilitaka kurudi ili nikuonyeshe mengi zaidi kuhusu kusudi la Mungu kwa dunia hii.” Fungua picha iliyo kwenye ukurasa wa 33, soma Ufunuo 21:3, 4, kisha ueleze kifupi jinsi Ufalme wa Mungu utakavyotimiza ahadi hii. Fanya toleo la funzo la Biblia nyumbani bila malipo.
6 Kumbuka kwamba mradi wa kufanya ziara za kurudia ni kuanzisha mafunzo ya Biblia. Kile kitabu kipya, Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, kimeundwa hasa kwa ajili ya kuongoza mafunzo. Tunapofuatia maangusho ya vitabu vya zamani na kuanzisha funzo hasa, ingekuwa vizuri kuelekeza uangalifu kwenye kitabu hiki kipya. Tutapata shangwe nyingi wakati wale wanaojifunza wanapojua kumwitia Yehova ili wapate wokovu.—Mdo. 2:21.