Matangazo
◼ Fasihi ya kutumiwa wakati wa Februari: Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha au Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Aprili na Mei: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo andikisho halichukuliwi toa magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida au broshua yoyote yaweza pia kutumiwa (isipokuwa broshua Elimu na Shule). TAARIFA: Makutaniko ambayo bado hayajaagiza vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa kufanya hivyo katika Fomu ya Kuomba Fasihi yao ya kila mwezi itakayofuata (S-14-SW).
◼ Tafadhali kumbukeni kwamba barua zinazopelekewa Sosaiti zapaswa kuwa na sahihi ya kawaida ya yule (wale) anayeandika (wanaoandika) kuongezea majina yoyote yaliyochapwa au kuandikwa kwa mkono kwenye umalizio.
◼ Mapainia wa kawaida wanaopendezwa kushiriki katika kampeni ya mwaka huu ya eneo lililo pekee kuanzia Julai hadi Septemba wakiwa mapainia wa pekee wa muda wanaweza kutoa maombi yao sasa kupitia baraza la wazee (au halmashauri ya utumishi) la kutaniko lao. Katika mapendekezo yazo, halmashauri za utumishi zaombwa kutoa sababu za kupendekeza painia na kueleza kama yeye ni mseja au amefunga ndoa, mwanamume au mwanamke (ana watoto wangapi ikiwa anao), na ikiwa mwenye kuomba yuko huru kuhamia maeneo yasiyogawiwa mtu kwa kipindi cha miezi mitatu. Halmashauri za utumishi zitaelewesha wazi mambo hayo na kupeleka barua za maombi pamoja na mapendekezo yazo kwa Sosaiti kufikia Machi 15, 1996.
◼ Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wapaswa kupitia utendaji wa mapainia wote wa kawaida. Ikiwa kuna wowote wanaopata ugumu wa kutimiza takwa la saa, wazee wapaswa kupanga ili usaidizi utolewe. Pitia mambo makuu yaliyo kwenye mafungu 12-20 ya nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1986.
◼ Sherehe ya Ukumbusho itakuwa Jumanne, Aprili 2, 1996. Ijapokuwa hotuba inaweza kuanza mapema, tafadhali kumbukeni kwamba kupitishwa kwa mkate na divai ya Ukumbusho hakupaswi kuanza mpaka baada ya jua kushuka. Pateni habari kutoka kwa vyanzo vya habari vya kwenu ili kujua wakati wa jua kushuka katika eneo lenu. Hakuna mikutano mingine isipokuwa ya utumishi wa shambani ipaswayo kufanywa tarehe hiyo. Ikiwa kwa kawaida kutaniko lenu huwa na mikutano Jumanne, mwaweza kuifanya siku nyingine ya juma hilo ikiwa Jumba la Ufalme lapatikana.
◼ Watangazaji wanaotaka kutumikia wakiwa mapainia-wasaidizi katika Machi, Aprili, na Mei wapaswa kufanya mipango yao sasa na kutoa ombi lao mapema. Kufanya hivi kutasaidia wazee wafanye mipango inayohitajiwa ya utumishi wa shambani na kuwa na magazeti ya kutosha na fasihi nyingine zilizopo.
◼ Pakiti ya habari za kisheria yapatikana ili kusaidia watangazaji wanaohusika na mambo ya kisheria juu ya utunzaji na utembeleaji wa mtoto mahali ambapo dini yetu inashambuliwa. Pakiti hii yapaswa kuombwa na baraza la wazee peke yake ikiwa ni dhahiri kwamba itikadi za kidini za mtangazaji zitatolewa suala. Habari yenye kusaidia kwa wale wanaokabiliana na masuala ya kawaida kuhusu utunzaji au utembeleaji wa mtoto yaweza kupatikana katika Amkeni! la Oktoba 22, 1988, kurasa 2-14 (Kiingereza), na katika chati ipatikanayo katika Amkeni! la Oktoba 8, 1991 ukurasa 9.
◼ Tuna ugavi mwingi wa Kitabu-Mwaka cha 1994 katika Kiswahili. Kichapo hiki kina historia ya Mashahidi wa Yehova katika Afrika Mashariki nacho chastahili kuongezwa kwenye maktaba ya kila familia. Makutaniko yanaweza kutoa maombi yao katika Fomu ya Kuomba Fasihi yao ya kila mwezi itakayofuata (S-14-SW).
◼ Vichapo Vinavyopatikana:
Furahia Milele Maisha Duniani! —Kichina
Je! Kweli Mungu Anatujali? —Kiurdu
Jinsi ya Kuipata Barabara ya Kwenda Kwenye Paradiso (Kwa ajili ya Waislamu) —Kiurdu
Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—1996 —Kiarabu, Kifaransa, Kiingereza
Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa —Kichina
Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje? —Kichina
“Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya” —Kichina
Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele —Kichina, Kichina (Sahili)
◼ Kaseti Zinazopatikana:
Maombolezo, Yeremia (seti ya kaseti nne) —Kifaransa
◼ Vidiokaseti Zinazopatikana:
To The Ends of the Earth —Kiingereza
Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, (Buku la 2) —Lugha ya Ishara ya Marekani