Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/96 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Aprili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Aprili
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Aprili 1
  • Juma Linaloanza Aprili 8
  • Juma Linaloanza Aprili 15
  • Juma Linaloanza Aprili 22
  • Juma Linaloanza Aprili 29
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 4/96 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Aprili

Juma Linaloanza Aprili 1

Wimbo 132

Dak 12: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Kwa idili tia moyo wote washiriki kikamili katika siku ya pekee ya utendaji wa magazeti katika Aprili 6. Panga kutumia matoleo yote ya zamani yaliyo kwenye akiba ya kutaniko. Ikiwa magazeti ya ziada yahitajiwa kwenye mwezi huu ona kama hayo yaweza kupatikana kutoka kutaniko la karibu. Ikiwa sivyo basi agizeni nakala za ziada kutoka ofisi ya tawi. Fanya matangazo ya waziwazi kuhusu mipango ya utumishi kwa siku hiyo.

Dak 18: “Iweni na ‘Juhudi Katika Matendo Mema’ Mwezi wa Aprili!” Maswali na majibu kwa mafungu 1-10 ikiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Eleza (1) yanayopangwa kwenu kwa ajili ya utendaji uliopanuliwa wa utumishi wa shambani mwezi wa Aprili, (2) jinsi wote wanavyoweza kusaidiwa washiriki, na (3) jinsi wapya na wachanga wanavyoweza kuhusishwa.

Dak 15: “Tafuta Walio na Mwelekeo Ufaao.” Pitia utoaji mbalimbali uliodokezwa, kisha uwe na maonyesho mawili kuonyesha jinsi unavyoweza kutumiwa. Kadiri wakati unavyoruhusu, eleza baadhi ya madokezo ya kutoa magazeti, yapatikanayo katika Huduma ya Ufalme Yetu, Septemba 1995, ukurasa wa 5.

Wimbo 20 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 8

Wimbo 72

Dak 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu; taja shukrani za upaji wa hiari zilizopokewa kutoka kwa Sosaiti. Zungumzia njia zifaazo tunazoweza kusaidia wapya wanaohudhuria Ukumbusho wafanye maendeleo zaidi ya kiroho. Pitia Mnara wa Mlinzi, Aprili 1, 1991, kurasa 9-12. Tia moyo wote washiriki katika utendaji wa magazeti juma hili.

Dak 15: “Toa Utumishi Mtakatifu Usiku na Mchana.” Maswali na majibu. Soma mafungu 5 na 6.

Dak 15: “Iweni na ‘Juhudi Katika Matendo Mema’ Mwezi wa Aprili!” Maswali na majibu kwa mafungu 11-15. Tia moyo wote wachanganue hali zao za kibinafsi na kutafuta njia za kuongeza kuunga mkono kwao katika huduma ya shambani.

Wimbo 113 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 15

Wimbo 133

Dak 10: Matangazo ya kwenu. Kumbusha wasikilizaji kuhusu hotuba ya pekee ya Aprili 21, yenye kichwa “Kudumu Bila Lawama Kati ya Kizazi Kilichopotoka.” Tia moyo wote wafanye jitihada za ziada za kusaidia kila mmoja kuhudhuria.

Dak 15: “Hali Zimebadilika.” Maswali na majibu. Kazia kutoa ujumbe wa Ufalme katika njia inayolingana na mahitaji yenye kukaza watu. Dokeza baadhi ya masuala ya familia na kijamii yaliyo akilini mwa watu wengi, kama ilivyoonyeshwa katika Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 1994, kurasa 22-23.

Dak 20: “Imani Hufuata Jambo Lililosikiwa.” Zungumza jinsi maangusho ya magazeti na maandikisho yanavyoweza kutumiwa ili kusitawisha kupendezwa kunakoweza kuongoza kwenye mafunzo ya Biblia katika kitabu Ujuzi. Uwe na maonyesho mawili au matatu.

Wimbo 204 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 22

Wimbo 6

Dak 15: Matangazo ya kwenu. Pitia mambo makuu ya hotuba ya pekee iliyotolewa mwisho-juma uliopita. Zungumza jinsi hili onyo la upole liwezavyo kuhamasisha watu wenye kupendezwa kuchukua msimamo imara kwa ajili ya ibada ya kweli. Pia, kazia uangalifu kwa “Endeleeni Kuongezeka Katika Ujuzi Sahihi,” na ukazie umaana wa kuhudhuria Funzo la Kitabu la Kutaniko kwa ukawaida.

Dak 12: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee. Eleza sababu kwa nini akina ndugu wanaoongoza mikutano wanapaswa kuepuka kufahamiana kupita kiasi kwa kuita majina ya watu mmoja-mmoja, wakitumia majina yao ya kwanza tu.

Dak 18: “Vuka Uende Makedonia Ukasaidie.” Ishughulikiwe kwa maswali na majibu. Tia moyo wote wafikirie kutumia sikukuu na vipindi vingine ili kutoa ushahidi maeneo ya mbali na maeneo mengine yaliyo pekee na hasa eneo la nyumbani kwako mwenyewe.

Wimbo 143 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 29

Wimbo 144

Dak 12: Matangazo ya kwenu. Wengine hufafanua Mashahidi wa Yehova kuwa “farakano” au “kidhehebu,” wakiongoza wengine vibaya kuhusu utendaji na makusudi yetu. Ukitumia kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 181, eleza kifupi jinsi ya kukanusha shtaka hili. Eleza mipango ya utendaji wa magazeti juma hili. Matoleo ya zamani bado yaweza kutumiwa kwa matokeo.

Dak 15: Kuhubiri Eneo Letu Sawasawa. Hotuba itolewe na mwangalizi wa utumishi. Sehemu zilizotawanyika au zilizoko mbali huenda ikawa hazihubiriwi sana. Wengine huenda wakahepa kuhubiri maeneo ambayo watu ni matajiri au ni wa kidini. Maeneo ya biashara huenda yakaachwa. Watangazaji wengine huenda wakaomba maeneo wanayopenda kibinafsi kuliko yale yanayohitaji kuhubiriwa upesi. Tia moyo wote washirikiane na jitihada za kuhubiri maeneo yasiyohubiriwa. Miezi ya kampeni ya eneo lililo pekee kawaida huandaa fursa nzuri ya kuhubiri sehemu za mbali za mashambani. Hakikisha eneo limehubiriwa kikamili, kutia ndani wasiokuwepo nyumbani, kabla halijarudishwa. Toa madokezo mengine yafaayo kuonyesha jinsi wote wanavyoweza kusaidia kuhubiri eneo lenu vizuri.

Dak 18: Toa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mwezi wa Mei. Toa maandikisho. Katika eneo linalofanywa mara nyingi, toa broshua yoyote ifaayo. Weka rekodi ya maangusho yote, ukiwa na mradi wa kuanzisha watu wa kupelekewa magazeti kwa ukawaida. Kazia manufaa nyingi za ugawanyaji wa magazeti kuwa mojapo njia zenye matokeo za kueneza ujumbe wa Ufalme kwa umma. Tuhakikishe tuna ugavi tunapoenda shambani; yatoe katika kila fursa. Mipango ya kibinafsi ya Siku ya Magazeti ya kila juma ni njia yenye matokeo ya kuongeza maangusho. Ushahidi wa magazeti duka kwa duka na barabarani pia ni wenye matokeo. Fuatia kupendezwa kwa ziara za kurudia zinazokusudiwa kuanzisha mafunzo, ukitumia kitabu Ujuzi. Uwe na wonyesho mmoja au mawili mafupi ya kutoa matoleo ya karibuni, labda ukitumia utoaji mbalimbali upatikanao katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1995, ukurasa wa 3, mafungu 3-5; soma fungu la 6.

Wimbo 195 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki