Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/96 uku. 7
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 4/96 uku. 7

Matangazo

◼ Toleo la fasihi kwa Aprili na Mei: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo andikisho halichukuliwi toa magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida au broshua yoyote yaweza pia kutumiwa (isipokuwa broshua Elimu na Shule). Juni: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Julai na Agosti: Yoyote ya broshua zenye kurasa 32 zifuatazo: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Mahali panapofaa, broshua kama vile Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? zaweza kutolewa.

◼ Ofisi ya tawi ina ugavi wa kutosha wa kitabu Kiongozi cha Shule, katika Kiingereza na Kiswahili; mabuku yaliyojalidiwa ya Watchtower na Awake! katika Kiingereza na Kifaransa; pamoja na Kitabu-Mwaka cha 1992 katika Kiingereza na Kitabu-Mwaka cha 1994 katika Kiswahili (vyote vina historia ya tengenezo katika Afrika Mashariki). Hivi ni vifaa bora kwa walio wapya kupata pia kwa ajili ya funzo la kibinafsi na maktaba ya kutaniko.

◼ Rekebisho lafanywa katika utaratibu wa kubadilisha kadi za Kitambulisho cha Utumishi wa Painia. Kuanzia sasa na kuendelea, kadi za kubadilisha kwa mapainia wanaohama, wanaobadili majina yao, wanaopoteza kadi zao, au kuomba badiliko la mgawo zitatolewa na Sosaiti. Kadi zozote zisizotumiwa ambazo huenda mwandishi akawa nazo katika faili zapaswa kuharibiwa. Mabadiliko ya majina na migawo mipya itashughulikiwa katika njia ya kawaida, mwandishi akiandika habari ifaayo nyuma ya Ripoti ya Kutaniko (S-1-SW) ya mwezi. Baadaye, Sosaiti itapelekea kutaniko kadi mpya za mapainia. Hizi kwa kawaida zitakuja na ripoti ya kila mwezi. Mabadiliko yoyote yapaswa kupelekewa Sosaiti mara moja ili kwamba faili zetu ziweze kuwekwa kwa usahihi na ziwe za karibuni. Pia, painia aachapo utumishi huo au akiondolewa, nakala ya fomu S-206-SW yapasa kujazwa na kupelekewa Sosaiti bila kuchelewa.

◼ Maulizo yote yanayohusiana na tarehe za mikusanyiko ya wilaya katika nchi nyingine yapaswa kuelekezwa kwa ofisi zao za tawi. Anwani za ofisi za tawi ulimwenguni pote zapatikana katika ukurasa wa mwisho wa Kitabu-Mwaka.

◼ Mahali panapofaa, ikitegemea saa za mwangaza, wazee wapaswa kufanya mipango kwa kutaniko kutumia wakati kutoa ushahidi wa jioni.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki