Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/96 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Juni 3
  • Juma Linaloanza Juni 10
  • Juma Linaloanza Juni 17
  • Juma Linaloanza Juni 24
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 6/96 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni

Juma Linaloanza Juni 3

Wimbo 181

Dak 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi. Toa maelezo juu ya ripoti ya kila mwezi ya nchi yote na ya kutaniko la kwenu.

Dak 15: “Iga Imani Yao.” Maswali na majibu. Pitia vithibitisho vya imani, vilivyo katika sanduku kwenye ukurasa 13 katika Mnara wa Mlinzi, Septemba 15, 1991. Hoji mtangazaji mmoja au wawili ili kujua ni nini kimewasaidia wadumishe utendaji wao wa kawaida wa Ufalme kwa miaka mingi.

Dak 20: “Kueneza Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.” (Mafungu 1-3) Shughulikia fungu 1. (Tia ndani maelezo kutoka Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 1996, kurasa 12-13, mafungu 11-12.) Eleza kwamba mpangilio mpya wa ukurasa wa nyuma wa Huduma ya Ufalme Yetu umekusudiwa kutusaidia kuwa tayari zaidi kufanya ziara za kurudia. Kwa kuwa sikuzote ni jambo la hekima kufanya ziara za kurudia baada ya siku moja au mbili, badala ya kungoja kwa muda mrefu, tutachunguza utoaji wa nyumba kwa nyumba na ziara za kurudia katika Mkutano wa Utumishi uleule. Pitia kifupi mafungu 2 na 3, kila moja likifuatwa na wonyesho. Toaji zinazobaki katika makala zitashughulikiwa kwenye Mikutano ya Utumishi miwili itakayofuata.

Wimbo 143 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 10

Wimbo 63

Dak 7: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak 8: Kuzoeza Watoto Katika Utumishi wa Shambani. Hotuba itolewe na mzee. Kuanzia umri mchanga, watoto wetu wapaswa kuwa watendaji pamoja nasi katika utumishi. Mazoezi na uzoefu wanaopata utaandaa msingi imara kwa imani yao na bidii miaka ya baadaye. Ni jambo la maana kwamba waelewe uhitaji wa kuona huduma kwa uzito na kujiendesha wenyewe ifaavyo. Ni lazima watoto waepuke mwenendo wenye makelele; utumishi si wakati wa kucheza. Ni vema zaidi kwao kuhubiri pamoja na watu wazima. Wanapaswa kusaidiwa katika kutoa utoaji kulingana na uwezo wao. (Ona Mnara wa Mlinzi, Agosti 1, 1988, ukurasa 15, fungu 20.) Wazazi wana daraka la kuandaa uangalizi; hawapaswi kutuma watoto kwenye mikutano ya utumishi bila mtu mkubwa wa kuwasimamia. Pongeza watoto wafanyapo vema.

Dak 10: “Kueneza Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.” (Mafungu 4-5) Baada ya utangulizi mfupi, toa wonyesho wa toaji za ziara ya kwanza na ziara ya kurudia kwenye mafungu 4 na 5. Tia moyo watangazaji wafuatie mara moja maangusho yote ya kitabu Ujuzi.

Dak 20: “Jinsi ya Kufanya Wanafunzi kwa Kutumia Kitabu Ujuzi.” Toa maelezo mafupi ya utangulizi yanayotegemea mafungu 1-2. Shughulikia mafungu 3-11 kwa maswali na majibu. Eleza kwamba sehemu inayobaki ya nyongeza itapitiwa kwenye Mikutano ya Utumishi katika Julai na Agosti. Tia moyo wote waihifadhi.

Wimbo 92 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 17

Wimbo 157

Dak 10: Matangazo ya kwenu.

Dak 15: “Mazungumzo ya Kirafiki Yaweza Kuufikia Moyo.” Maswali na majibu. Alika mtangazaji mmoja au wawili wasimulie mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo kuonyesha jinsi walivyopata itikio zuri kwa mfikio wa kirafiki.

Dak 20: “Kueneza Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.” (Mafungu 6-7) Kazia miradi ya kufanya ziara ya kurudia: Sitawisha kupendezwa, anzisha funzo, fanya mipango hususa ya kurudi. Baada ya kupitia kifupi utoaji katika mafungu 6 na 7, toa wonyesho wa kila mmoja, kuonyesha jinsi ya kuanzisha funzo. Soma fungu 17 kwenye ukurasa 14 katika Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 1996.

Wimbo 211 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 24

Wimbo 6

Dak 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi.

Dak 15: Mahitaji ya kwenu. (Au toa hotuba juu ya “Kulitumia Sawasawa Neno la Ile Kweli,” inayotegemea Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 1996, kurasa 29-31.)

Dak 20: “Wasaidie Watumikie Tena.” Hotuba na mazungumzo yaongozwe na mzee. Dokeza kutumia makala ya Mnara wa Mlinzi, Agosti 1, 1992 “Nirudieni Mimi, Nami Nitawarudia Ninyi” ili kutia moyo wasiotenda. Taja baadhi ya mambo makuu.

Wimbo 71 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki