Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/96 uku. 7
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 6/96 uku. 7

Matangazo

◼ Toleo la fasihi kwa Juni: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Julai na Agosti: Yoyote ya broshua zenye kurasa 32 zifuatazo: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Mahali panapofaa, broshua kama vile Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? zaweza kutolewa. Inadokezwa kwamba kitabu Kuishi Milele kitolewe tunapohubiri eneo lililo pekee na lisilohubiriwa mara nyingi. Septemba: Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha.

◼ Kuanzia juma la Septemba 9, 1996, hadi juma la Februari 10, 1997, tutamaliza mazungumzo yetu juu ya kitabu Upeo wa Ufunuo kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko.

◼ Kuanzia toleo la Mei 1, 1996, funzo la Mnara wa Mlinzi katika kila kutaniko litakuwa sawia na ratiba ya ulimwenguni pote kama ionyeshwavyo kwenye ukurasa 2 wa kila toleo la gazeti hilo. Kwa mfano, makala ya funzo ya kwanza katika toleo la Mei 1, 1996, yenye kichwa, “Mungu na Kaisari,” imeratibiwa kwa funzo katika juma la Juni 3 na kuendelea. Kwa hiyo, kuanzia na toleo hili la Huduma ya Ufalme Yetu hatutachapisha tena ratiba ya funzo la kila juma la Mnara wa Mlinzi. Habari zaidi juu ya jinsi ya kushughulikia makala za funzo zisizotumiwa katika matoleo ya Aprili 1, 1996, na Aprili 15, 1996, yaweza kupatikana katika barua ya Sosaiti “Kwa Makutaniko Yote,” ya Aprili 3, 1996.

◼ Kuhesabiwa kwa fasihi kwa kila mwaka hakutafanywa tena Septemba 1 kila mwaka. Rekebisho fulani limefanywa la kutaka habari hii Januari 1 kila mwaka. Hivyo fomu ya S-AB-18-SW, Orodha ya Fasihi kuanzia Januari 1, 1997 itapelekwa kwa makutaniko mwezi wa Novemba. Tafadhali panga kuwe kuhesabu kihalisi fasihi zilizopo mwishoni mwa Desemba na si Agosti kulingana na rekebisho hili.

◼ Rekebisho lililo juu kuhusiana na kuhesabu fasihi hakuhusu S-10-SW, fomu ya Ripoti ya Mchanganuo wa Kutaniko, ambazo bado zapaswa kupelekwa kwa ofisi ya tawi kabla ya Septemba 6.

◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu aliyegawiwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko mnamo Juni 1 au upesi baada ya hapo iwezekanavyo. Tangazieni kutaniko jambo hili lifanywapo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki