Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/96 uku. 1
  • Ni Nani Anayestahili Kuhubiri?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nani Anayestahili Kuhubiri?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Ninastahili Kuhubiri?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Njema Hizi za Ufalme Tuzihubiri
    Mwimbieni Yehova Sifa
  • Tumeandaliwa Kikamili Kuwa Walimu wa Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Jinsi Habari Njema Inavyohubiriwa
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 8/96 uku. 1

Ni Nani Anayestahili Kuhubiri?

1 Kuhusu huduma, je, umepata kuhisi kama Musa? Yeye alisema: “Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako.” (Kut. 4:10) Ikiwa wahisi hivyo, huenda ukaepuka kuhubiri. Hata hivyo, Yesu ‘alituagiza tuwahubiri watu na kushuhudia.’ (Mdo. 10:42) Kwa hiyo tutakuwaje wahubiri wastahilio wa habari njema?

2 Si kadiri ya elimu yetu ya kimwili inayotustahilisha kwa huduma. Paulo alisema kwamba ‘si wengi wenye hekima ya mwilini walioitwa’ na kwamba “hekima ya dunia hii ni upuzi mbele za Mungu.” (1 Kor. 1:26; 3:19) Yesu aliteua mitume wake kutoka miongoni mwa wafanyakazi wa mikono—angalau wanne wakiwa wavuvi. Viongozi wa kidini wenye kiburi waliwaona kwa madharau kuwa “watu wasio na elimu.” Kulingana na viwango vya kilimwengu, mitume hawakustahili kuhubiri. Hata hivyo, hotuba ya Petro yenye ustadi iliyotolewa siku ya Pentekoste ilichochea watu 3,000 kubatizwa!—Mdo. 2:14, 37-41; 4:13.

3 Yehova Hutustahilisha Kuhubiri: Paulo alitangaza: “Kuwa kwetu na sifa za ustahili wa kutosha kwatoka kwa Mungu.” (2 Kor. 3:5, NW) Yehova, Chanzo cha hekima, amefundisha mamilioni kuhubiria wengine kweli ya Ufalme. (Isa. 54:13) Matokeo ya kazi hii yaweza kuonekana katika wale 338,491 waliobatizwa mwaka uliopita wakiwa ‘barua iliyoandikwa.’ (2 Kor. 3:1-3) Tuna kila sababu ya kuhubiri tukiwa na ujasiri na usadikisho kuhusu mambo ambayo tumejifunza kutoka kwa Yehova.

4 Tengenezo la Mungu limesitawisha programu ya kimataifa ya kuzoeza wahudumu. Kupitia Maandiko na misaada mingi mbalimbali ya Biblia, tunafundishwa na kuzoezwa kuwa ‘kamili, tumekamilishwa’ kuhubiri. (2 Tim. 3:16, 17) Wengi wamependezwa na usomi unaopatikana katika vichapo vya Sosaiti. Kwa mfano, jarida moja la Kisweden lilisema: “Kwa kuunga mkono imani inayohubiriwa na Mashahidi wa Yehova kuna usomi wa Biblia wa hali ya juu na wa kimataifa.”

5 Kwa mwelekezo unaotolewa katika mikutano yetu mitano ya kila juma, programu yetu ya usomaji na funzo la Biblia, ushauri katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, usaidizi wa kibinafsi kutoka kwa wengine walio wahudumu wenye uzoefu, na zaidi ya yote, utegemezo wa roho takatifu ya Yehova, twaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova hutuona kuwa tumestahilishwa kabisa kuhubiri. “Kama kutoka kwa Mungu, mbele za Mungu, twanena katika Kristo.”—2 Kor. 2:17.

6 Tukitwaa manufaa kamili ya mazoezi ya kitheokrasi yanayoandaliwa na Mungu kupitia tengenezo lake, hatuna sababu ya kurudi nyuma au kuogopeshwa. Twaweza kuhubiria wengine kwa shangwe, tukihakikishiwa kwamba Yehova atabariki jitihada zetu.—1 Kor. 3:6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki