Mikutano Ya Utumishi Kwa Agosti
Juma Linaloanza Agosti 5
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu.
Dak 20: “Kutoacha Kutangaza Habari Njema.” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tia ndani sehemu kadhaa kutoka Insight on the Scriptures, Buku la 2, ukurasa 673, fungu 1.
Dak 15: “Tangaza Habari Njema za Ufalme Ukitumia Broshua.” (Mafungu 1-5) Tumia fungu la kwanza katika hotuba ya utangulizi. Toa maelezo yenye kutia moyo kuhusu manufaa za kutumia broshua Maisha Duniani na “Tazama!” katika huduma. Panga uwe na maonyesho manne yaliyofanyiwa mazoezi vizuri, kuonyesha jinsi ziara za kwanza na ziara za kurudia ziwezavyo kushughulikiwa kwa kutumia broshua hizi. Panga mhubiri mchanga, akisaidiwa na mzazi wake, aonyeshe utoaji mbalimbali kwa kutumia broshua Maisha Duniani. Watangazaji wanaweza kupatanisha utoaji wao katika broshua nyinginezo kwa kufuata madokezo yanayoonyeshwa.
Wimbo 136 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 12
Dak 15: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Tia ndani maelezo yafaayo juu ya “Njia za Kushiriki,” katika Mnara wa Mlinzi Desemba 1, 1993, kurasa 29-31.
Dak 15: “Tangaza Habari Njema za Ufalme Ukitumia Broshua.” (Mafungu 6-8) Pitia kifupi yaliyomo ya broshua Serikali. Toa wonyesho wa utoaji mbalimbali uliodokezwa kwa ziara za kwanza na ziara za kurudia. Tia moyo wote wafuatie maangusho yao.
Dak 15: “Michango kwa Kazi ya Ulimwenguni Pote ya Sosaiti Yaunga Mkono Upanuzi.” Hotuba yenye idili itolewe na mzee. Tia ndani baadhi ya takwimu juu ya maendeleo ya kazi ya Ufalme katika baadhi ya nchi zilizoonyeshwa, kama inavyoripotiwa kwenye Kitabu-Mwaka. Pia pitia azimio la kutaniko la kutoa mchango kwa ujenzi wa tawi jipya katika Nairobi. Kazi nyingi ingalipo ya kufanywa kabla umalizio ulioratibiwa katika Julai 1997. Wajitoleaji wengi wahitajiwa. Pitia matakwa kama ionyeshwavyo katika barua ya tawi kwenye Huduma ya Ufalme Yetu ya Novemba 1995, ukurasa 1, fungu la 5. Tia moyo wale wanaoweza wafikirie kwa uzito na kwa sala kujitolea kwa ajili ya pendeleo hili lenye shangwe.
Wimbo 9 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 19
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Pitia Sanduku la Swali.
Dak 15: “Ni Nani Anayestahili Kuhubiri?” Mzee azungumzia makala na watangazaji wawili au watatu. Kazia kwamba tunapokea mazoezi bora, yanayotuandaa kikamili kuwa wahudumu wa Mungu. Hatuna sababu ya kuhisi kutostahili kuhubiri.
Dak 20: “Jinsi ya Kufanya Wanafunzi kwa Kutumia Kitabu Ujuzi.” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji juu ya mafungu 17-26 ya nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Juni 1996. Panga mapema kutia ndani mambo yaliyoonwa ya kwenu ya wale ambao wanaongoza mafunzo katika kitabu Ujuzi. Wanaweza kutoa maelezo yanayotia moyo ya jinsi ambavyo wametumia madokezo yanayopatikana katika nyongeza na jinsi wamesaidiwa kuongoza funzo la Biblia lenye maendeleo zaidi. Tia moyo wote waweke vizuri nyongeza hiyo na kuipitia kibinafsi wanapoanzisha funzo jipya.
Wimbo 189 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Agosti 26
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Pitia “Aprili 6, 1996: Itikio Zuri Ajabu!” Ukieleza juu ya kile kilichotimizwa na kutaniko la kwenu. Tia moyo utendaji wa magazeti juma hili ukikazia kifupi makala na matoleo ambayo yanaweza kutolewa.
Dak 20: Kupendezwa na Kusoma kwa Watoto Wako. Hotuba itolewe na mzee. Pitia habari katika broshua Mashahidi wa Yehova na Elimu, kurasa 2-5, ukionyesha sababu inayofanya tuthamini mazoezi mazuri yanayoandaliwa shuleni. Zungumza jinsi ya kueleza walimu kwa busara sababu tunayoweka miradi ya kiroho zaidi badala ya ufuatiaji wa kimwili. Tia ndani mambo kutoka “Umalizio,” kwenye ukurasa 31. Tia moyo wazazi watumie madokezo yaliyo katika Amkeni!, Aprili 8, 1989, ukurasa 11.
Dak 15: Pitia Toleo la Fasihi kwa Septemba. Tutatumia kitabu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha. Toa kielezi cha jinsi kichapo hiki kiwezavyo kutumiwa. Unaweza kusema jambo kama hili: “Je, utakubali kwamba familia ya kisasa hukabiliana na magumu ambayo hayakuwa ya kawaida kwa vizazi vilivyopita? [Ruhusu itikio.] Kulingana na maoni yako, kwa nini inakuwa hivi? [Shukuru kwa itikio. Fungua na usome 2 Timotheo 3:1-3.] Misemo ‘wasiotii wazazi wao’ na ‘wasiowapenda wa kwao’ kwa usahihi yafafanua wengi katika siku yetu. Hata hivyo, Mungu yuleyule aliyetabiri matatizo haya ametupatia pia mwongozo ufaao wa jinsi ya kufanya familia iwe na umoja zaidi.” Soma fungu kutoka “Watangazaji” lililo kwenye ukurasa wa 2. Toa kitabu.
Wimbo 113 na sala ya kumalizia.