Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/10 uku. 1
  • Je, Ninastahili Kuhubiri?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Ninastahili Kuhubiri?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nani Anayestahili Kuhubiri?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tumeandaliwa Kikamili Kuwa Walimu wa Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Habari Njema Hizi za Ufalme Tuzihubiri
    Mwimbieni Yehova Sifa
  • Kigezo cha Kufuata kwa Ukaribu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 1/10 uku. 1

Je, Ninastahili Kuhubiri?

1. Kwa nini hatupaswi kuhisi kwamba hatustahili kuhubiri?

1 Je, umewahi kujiuliza swali hilo? Usife moyo! Ili tustahili kuwa wahudumu si lazima tuwe na elimu au kipawa fulani. Baadhi ya wanafunzi wa karne ya kwanza walitajwa kuwa “watu wasio na elimu na wa kawaida tu.” Hata hivyo, walikuwa na matokeo katika kazi yao ya kuhubiri habari njema kwa sababu waliazimia kufuata kielelezo cha Yesu.—Mdo. 4:13; 1 Pet. 2:21.

2. Eleza jinsi Yesu alivyofundisha.

2 Yesu Alivyofundisha: Alifundisha kwa njia rahisi na yenye kueleweka. Maswali yake, mifano, na tangulizi zake rahisi ziliwavutia wasikilizaji. (Mt. 6:26) Aliwajali watu kikweli. (Mt. 14:14) Isitoshe, Yesu alizungumza kwa uhakika na kwa mamlaka, akijua kwamba Yehova alikuwa amemtuma na kumpa nguvu za kutimiza mgawo wake.—Luka 4:18.

3. Yehova hutusaidiaje kutimiza huduma yetu?

3 Yehova Anatusaidia: Kupitia Neno na tengenezo lake, Mfundishaji wetu Mkuu hutupa mazoezi tunayohitaji ili tufaulu katika kazi ya kuhubiri habari njema. (Isa. 54:13) Kwa kuwa Yehova alihifadhi habari kuhusu njia za Yesu za kufundisha, tunaweza kuzichanganua na kuziiga. Yehova hutupa roho yake takatifu na hutuzoeza kupitia mikutano ya kutaniko. (Yoh. 14:26) Isitoshe, ameandaa wahubiri wenye uzoefu wanaoweza kutusaidia kuwa wenye matokeo zaidi.

4. Kwa nini tuna sababu ya kuhisi kwamba tunastahili kuwahubiria wengine habari njema?

4 Tuna kila sababu ya kuhisi kwamba tunastahili kuhubiri, kwa kuwa “sifa za kustahili vya kutosha hutoka kwa Mungu.” (2 Kor. 3:5) Tunapomtegemea Yehova na kutumia vizuri msaada ambao ametuandalia kwa upendo, tutakuwa na ‘uwezo kamili, tukiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.’—2 Tim. 3:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki