Je, Ninastahili Kuhubiri?
1. Kwa nini hatupaswi kuhisi kwamba hatustahili kuhubiri?
1 Je, umewahi kujiuliza swali hilo? Usife moyo! Ili tustahili kuwa wahudumu si lazima tuwe na elimu au kipawa fulani. Baadhi ya wanafunzi wa karne ya kwanza walitajwa kuwa “watu wasio na elimu na wa kawaida tu.” Hata hivyo, walikuwa na matokeo katika kazi yao ya kuhubiri habari njema kwa sababu waliazimia kufuata kielelezo cha Yesu.—Mdo. 4:13; 1 Pet. 2:21.
2. Eleza jinsi Yesu alivyofundisha.
2 Yesu Alivyofundisha: Alifundisha kwa njia rahisi na yenye kueleweka. Maswali yake, mifano, na tangulizi zake rahisi ziliwavutia wasikilizaji. (Mt. 6:26) Aliwajali watu kikweli. (Mt. 14:14) Isitoshe, Yesu alizungumza kwa uhakika na kwa mamlaka, akijua kwamba Yehova alikuwa amemtuma na kumpa nguvu za kutimiza mgawo wake.—Luka 4:18.
3. Yehova hutusaidiaje kutimiza huduma yetu?
3 Yehova Anatusaidia: Kupitia Neno na tengenezo lake, Mfundishaji wetu Mkuu hutupa mazoezi tunayohitaji ili tufaulu katika kazi ya kuhubiri habari njema. (Isa. 54:13) Kwa kuwa Yehova alihifadhi habari kuhusu njia za Yesu za kufundisha, tunaweza kuzichanganua na kuziiga. Yehova hutupa roho yake takatifu na hutuzoeza kupitia mikutano ya kutaniko. (Yoh. 14:26) Isitoshe, ameandaa wahubiri wenye uzoefu wanaoweza kutusaidia kuwa wenye matokeo zaidi.
4. Kwa nini tuna sababu ya kuhisi kwamba tunastahili kuwahubiria wengine habari njema?
4 Tuna kila sababu ya kuhisi kwamba tunastahili kuhubiri, kwa kuwa “sifa za kustahili vya kutosha hutoka kwa Mungu.” (2 Kor. 3:5) Tunapomtegemea Yehova na kutumia vizuri msaada ambao ametuandalia kwa upendo, tutakuwa na ‘uwezo kamili, tukiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.’—2 Tim. 3:17.