Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/96 uku. 11
  • Sanduku La Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku La Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Uchunguzi Wenye Kuendelea wa Kazi Yenye Uharaka ya Kufanya Wanafunzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Jinsi ya Kufanya Wanafunzi kwa Kutumia Kitabu Ujuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Pili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 10/96 uku. 11

Sanduku La Swali

◼ Funzo rasmi la Biblia pamoja na mtu katika kitabu Ujuzi liongozwe kwa muda gani?

Yehova analibariki tengenezo lake leo. Twaona uthibitisho wa hilo kila mwaka wakati maelfu ya wapya wachukuapo msimamo kwa ajili ya kweli. Kitabu Ujuzi kinathibitika kuwa chombo chenye matokeo katika kutimiza hilo. Toleo la Januari 15, 1996, la Mnara wa Mlinzi lilionyesha kwamba kitabu hicho kimekusudiwa kimsaidie mwanafunzi wa Biblia afanye maendeleo ya haraka ya kiroho, labda hata kufikia hatua ya ubatizo katika miezi michache.

Kwa sababu hiyo, gazeti lilo hilo la Mnara wa Mlinzi, kwenye ukurasa wa 17, lilishauri hivi: “Baada ya mtu kumaliza funzo lake la Biblia katika kitabu Ujuzi naye amebatizwa, huenda lisiwe jambo la lazima kuongoza funzo la rasmi pamoja naye katika kitabu cha pili.”

Namna gani mtu ambaye habatizwi baada ya kumaliza kitabu Ujuzi? Huduma ya Ufalme Yetu, ya Juni 1996, ukurasa wa 6, fungu la 23, ilitukumbusha juu ya hoja iliyotolewa kwenye Mnara wa Mlinzi juu ya kutojifunza vitabu vya ziada pamoja na mwanafunzi yuleyule baada ya kumaliza kitabu Ujuzi. Je, hilo lamaanisha kwamba hatupendezwi na kumsaidia mwanafunzi wa Biblia baada ya hatua hiyo? La. Twataka watu wapate ujuzi wa msingi juu ya kweli. Hata hivyo, yatarajiwa kwamba katika muda mfupi kwa kulinganishwa, mwalimu mwenye matokeo ataweza kumsaidia mwanafunzi wa kawaida mwenye moyo mweupe apate ujuzi wa kutosha ili kufanya uamuzi wenye akili wa kumtumikia Yehova. Yawezekana kwamba kwa sababu ya hali zao za kibinafsi, wanafunzi fulani wa Biblia hata watakuwa na hamu ya kujifunza zaidi ya mara moja kwa juma.

Yakubaliwa kwamba, wanafunzi fulani watafanya maendeleo polepole kuliko wengine. Lakini ikiwa baada ya kujifunza kitabu Ujuzi, funzo ambalo huenda lilichukua muda mrefu kuliko kawaida, huyo mtu hajaamua kwamba anataka kushirikiana pamoja na kutaniko, mtangazaji apaswa kuzungumzia hali hiyo pamoja na mmoja wa wazee katika Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko. Ikiwa hali zinazopunguza uzito au zisizo za kawaida zinahusika, msaada wa ziada waweza kutolewa. Hilo lapatana na ile kanuni iliyotajwa kwenye fungu la 11 na la 12 kwenye ukurasa wa 17 wa Mnara wa Mlinzi la Januari 15, 1996.

Uthamini wa kujifunza hata ujuzi wa msingi juu ya kweli wapaswa kumhamasisha mwanafunzi ahudhurie mikutano ya Kikristo. Hilo laweza kumwongoza mwanafunzi atoe uthibitisho ulio wazi wa tamaa yake ya kumtumikia Yehova. Ikiwa uthamini huo wa kiroho hauonekani baada ya funzo katika kitabu Ujuzi kuongozwa kwa kipindi kilichorefushwa, huenda ikafaa kukomesha hilo funzo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki